Tag: africa

mageuzi ya Intaneti (iot) katika biashara na maisha. Jihudumie leo kutoka Rednet Technologies. Kwanini mteja akuchague wewe?

IFAHAMU AINA MPYA YA UDALALI WA MTANDAONI (DROPSHIPPING)

Dunia inakwenda kasi sana na Teknolojia inazidi kusambaa na kuteka sekta za kiuchumi. Mwandishi mmoja alinukuliwa akisema “In this modern world, prepare to change your career.” Umeshafikiria kuwa Dalali smart? Leo sasa ifahamu aina mpya ya udalali wa mtandaoni (Dropshipping) kwa undani. Ni nini na inafanya kazi vipi? Makinika mpaka mwisho wa makala hii..

Kwa Afrika yenye watumiaji wa huduma za internet wanaokadiriwa kuzidi milioni 400, tafiti zinaonyesha fursa za kuongezeka kwa biashara za mtandaoni (e-commerce) sasa ni kubwa kuliko wakati mwingine wowote. Shirika la Statista linakadiria sekta ya e-commerce kufikia thamani ya US 29$ milioni kufikia mwaka 2022.

DROPSHIPPING NI NINI?

Hii ni aina ya Udalali wa kimtandao ambapo Mtu wa kati (Dalali) huchukua Oda kutoka kwa Mteja kisha huituma Oda hio kwa Mwenye Mali (Muuzaji) ambaye hukamilisha mauzo kwa Mteja na kumwachia Dalali Kamisheni yake stahili.

Lakini wakati mwingine hasa barani Afrika huyu Mtu wa Kati huchukua Oda kutoka kwa mteja kisha huenda kwa Mwenye mali na kuchukua Bidhaa na kisha kwenda kuiuza yeye moja kwa moja kwa Mteja. Hii ndio kitu inafanyika sana Afrika kama ulikua hujui.

Hata hivyo msingi Mkuu wa Dropshipping ni kuwa namna hii ya Biashara hufanywa na Mtu wa kati ambaye hana stock kabisa (haihitaji uwe na mtaji wa fedha au bidhaa ili kufanya dropshipping). Kwa hiyo Dropshipping ndiyo kinara katika aina za biashara za mtandaoni (e-commerce).

Hii Dropshipping ni biashara moja ambayo mtu yeyote hasa kijana anaweza kabisa kuifanya kwa kuwa haihitaji uwe na mtaji wa kifedha ama bidhaa (stock). Hata hivyo, kama zilivyo biashara zingine, sio biashara rahisi wala sio biashara ambayo inaweza kukutajirisha mara moja.

Unahitajika kuwa mbunifu, mwenye juhudi na mvumilivu ili uweze kufanikiwa kwenye aina hii ya biashara kwa kuwa:

1. KIWANGO CHA FAIDA NI KIDOGO: Kiwango cha faida hutegemea kamisheni au “cha juu” ambacho mara nyingi hakiwi kiwango kikubwa. Hivyo ili uweze kupata Faida kubwa inakubidi pia uhakikishe bidhaa/huduma nyingi zimemfikia mteja kupitia wewe.

KUMBUKA: Kila mauzo unayoyafanya hapa, kiwango kikubwa cha pesa humwendea Mwenye Mali, kile “Cha juu” ndio hubaki kuwa halali yako.

udalali wa mtandaoniongea na watu uvae viatu

ZINGATIA: Waswahili wanasema, “Ongea na watu uvae viatu” Ukitafsiri vizuri hii nafasi ya kufanikiwa ni kubwa kwa sababu kadiri unavyokuwa na watu wengi zaidi katika mtandao wako basi nafasi yako ya kutengeneza faida inazidi kuwa kubwa.

2. USHINDANI NI MKUBWA: Hii ni aina ya bishara ambayo ushindani wake ni mkubwa kweli kweli. Fikiria haihitaji mtaji wa Kifedha wala bidhaa(stock) ili kuanza kuifanya, watu wangapi wanaweza kuifanya? wangapi tayari wanaifanya sasa hivi? Hivyo ili ufanikiwe, lazima ukomae kweli.

3. UHALALI/UBORA WA BIDHAA: Mara nyingi hii sio kesi kubwa lakini huwa inatokea. Ni mara ngapi imetokea mteja ameona bidhaa fulani kupitia ukurasa wako(mtu kati) wa mtandaoni, halafu vile umeenda kwa Mwenye Mali ukakuta ile bidhaa iliyoonekana kwenye picha mtandaoni sio ile halisi uliyoikuta kwa Mwenye Mali. Hili jambo ni baya na linaumiza sana watu wa kati na wakati mwingine hushusha heshima na uaminifu ambao wameutengeneza kwa wateja wao kwa muda mrefu sana.

Wakati mwingine hutokea hata mwenye mali si halali kisheria au/na wewe (dalali) hufahamu hata bidhaa unazozichukua ili kupeleka kwa mteja zinatoka wapi. Swala la bidhaa feki linaathiri sana kipengele hiki ambapo hutokea bidhaa iliyoonekana mtandaoni kuwa na logo fulani inayoaminika, lakini ile iliyo kwa ground inakuwa logo ya kughushi/feki. Hivyo lazima uwe mwangalifu.

4. UGUMU WA KUTENGENEZA BRAND: Ukiwa mfanyabiashara wa aina ya Dropshipping, fahamu kuwa sifa ya ubora wa bidhaa mara zote itakwenda kwa Mwenye Mali tu. Kitachokufanya uendelee kubaki kwenye game ni namna yako nzuri ya kuhudumia wateja wako wote bila ubaguzi na kwa ubora wa juu.

Kutengeneza Brand ni muhimu sana. Brand haijengwi kwa siku moja hata hivyo, ni mchakato wa muda mrefu. Sasa kuelewa zaidi kuhusu Brand (ni nini na inafanyika vipi) gusa link hii hapa Branding vs Marketing, kipi ni kipi?

Kumbuka: sio Logo yako iliyo kwenye bidhaa. Hivyo tengeneza SUMAKU yako kwa kutumia aina ya maneno yanayoweza kuuza bidhaa (copywriting), matumizi mazuri ya mitandao ya kijamii pamoja na website bora na ambayo imeunganishwa na huduma za S.E.O.

Hizo ni baadhi ya Changamoto ambazo unategemea kukutana nazo katika aina hii ya biashara mtandaoni. Hata hivyo, kuna namna ambayo unatakiwa ujipange ili kuhakikisha Biashara yako inakuwa na mafanikio zaidi na uwezo wa kupambana na changamoto.

Kipi cha kufanya ili ufanikiwe katika Udalali huu wa Mtandaoni (Dropshipping)?:

1. CHAGUA HADHIRA YAKO: Haya ni mazingira na aina ya watu ambao unajihusanisha nao kila siku mtandaoni. Fahamu kuwa aina ya watu unaojihusanisha nao ni muhimu katika kutengeneza Aina ya soko linalofaa kwa bidhaa zako. Pia aina ya watu inaweza kukuambia ni aina gani ya bidhaa itawafaa kulingana na changamoto unaziziona zikiwatatiza kutoka kwao. Hapa lazima uwe na jicho zuri la kuona kile watu wengi hasa wafanyabiashara wenzako hawakioni. Kuwa Mchunguzi kidogo, hala hala usije kuwa mbea tu. Kwa vyovyote unapokua dalali hasa wa mtandaoni lazima ujitangaze, Kwanini ujitangaze sasa fuatana na makala hii hapa kufahamu zaidi..

2. TAFUTA MFANYABIASHARA (MWENYE MALI) WA KUAMINIKA: Hiki ni kipengele muhimu katika kuhakikisha bidhaa zako zinaweza kupatikana kwa wakati bila longolongo wala ujanjaujanja. Mteja mara nyingi hununua kwa uhitaji ambao husukumwa na hisia. Hivyo hisia hizo zinaposhindwa kufikiwa ndani ya muda fulani, basi mteja anaweza kugairi au kununua kwa mtu mwingine.

Hapa ukiwa kama mfanyabiashara lazima ujue namna ya kutengeneza hali ya dharura kwa mteja ili anunue bidhaa yako kwa upesi, lakini zaidi lazima utimize haja ya mteja wako ndani ya muda na kwa uhakika.

3. CHAGUA BIDHAA YA KUUZA: Kabla hujaanza kufanya aina hii ya biashara lazima ujue hizo bidhaa zinazohusika “utamuuzia nani?”. Katika kuchagua unatakiwa uangalie Umri, Elimu, Makundi ya kijamii (wanafunzi, wasomi wa vyuo, wafanyakazi, wazazi, watu wa dini nk). Hivyo lazima ujue ni bidhaa zipi zinawafaa wateja na hadhira yako Kiujumla.

Njia nzuri ya kuchagua bidhaa zinazouzika sana ni kupitia majukwaa kama YouTube kupitia matafuto kama “top 10 products to sell” utajifunza mengi humo.

•Pia unaweza kutumia Majukwaa ya Amazon na AlliExpress kupata bidhaa zinazofaa kufanyia biashara unayotaka kuifanya.

•Chunguza matangazo (sponsored ads) kupitia mitandao kama facebook, instagram na twitter. Kwenye kuchagua aina ya bidhaa jitahidi kuepuka:

•Bidhaa za chakula ambazo zinahitaji uthibitisho wa mamlaka, huna muda wa kupeleka bidhaa ikathibitishwe TMDA/TBS kabla haijamfikia mteja.

•Bidhaa ambazo ni silaha. Hizi mara nyingi soko lake ni la shaka kwa wateja wengi, hivyo kizifanya kutokuwa reliable.

•Mambo ya Fashion: Najua hii ndio watu wengi wanapenda kufanya, lakini jitafakari kuhusu ushindani wake sokoni, Nadhani unawajua wanaouza nguo na viatu katika mitandao ya kijamii.

4. WEKA BIDHAA ZAKO MTANDAONI: Baada yakufanya yote hapo juu, hakikisha bidhaa zako zinaonekana mtandaoni. Njia nzuri zaidi ya kuweka bidhaa mtandaoni ni kupitia Website na Instagram kwa sababu bidhaa inatakiwa kuonekana kwa picha ili kumvutia mteja. Mitandao mingi ya kijamii haikupi nafasi nzuri ya kuonyesha bidhaa zako kwa wateja katika unadhifu unaotakiwa. Hata hivyo ni muhimu pia kutumia mitandao mingine ya kijamii katika kunadi bidhaa zako mara kwa mara kupitia ujuzi wa “Copywriting” vizuri.

Sasa nimekuwekea makala kupitia links hizi hapa chini ili kuhakikisha somo la leo unalielewa vizuri. Zitakusaidia sana ukizimaliza zote.

  1. UKIRITIMBA KATIKA BIASHARA, NI ASALI AU SHUBIRI?
  2. KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE RASMI YA BIASHARA YAKO?
  3. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO

Nadhani leo ume ifahamu aina mpya ya udalali wa mtandaoni (Dropshipping) katika kiwango chake. Unalo lolote la kushare nasi? Tafadhali tujadili kupitia comment hapo chini.

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Ifahamu aina mpya ya udalali wa mtandaoni.

KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE(TOVUTI) RASMI YA BIASHARA YAKO?

Hebu fikiria wewe ni mgeni mahali fulani, baada ya kushikwa na njaa unaelekezwa migahawa miwili, mmoja ukiutafuta mtandaoni unaweza kupata taarifa zake mwingine hauna taarifa yoyote mtandaoni. Uelekeo wako utakuwa upande gani? Leo sasa tutakwenda kufahamu kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako. Makinika mpaka mwisho wa makala hii.

Kuishi katika ulimwengu wa kidijitali, tovuti ni zana muhimu sana katika biashara na masoko ya kidijitali. Cha kushangaza inakadiriwa 35% – 50% ya biashara ndogondogo duniani hazina tovuti zao binafsi, jambo linalozinyima fursa ya kuweka taarifa zao kirahisi mtandaoni na kupata wateja wapya kirahisi.

Kuna wanaosema kuwa matumizi ya Tovuti yanamezwa na uwepo wa mitandao ya kijamii ambayo pia watu wanaweza kuweka na kutangaza biashara zao humo. Ni kweli, aghalabu, kwa kutumia Mitandao ya kijamii hauna uhakika wa kumiliki taarifa na maudhui unayoweka humo muda wote. Watengenezaji ambao pia ni wamiliki wa Mitandao hio wanao uwezo wa kusimamisha/kufuta akaunti au maudhui yako muda wowote ikiwa biashara/maudhui yako yanakwenda kunyume na matakwa na masharti yao.

Vile vile Mitandao ya kijamii unayotumia inaweza kupungua umaarufu au kufilisika muda wowote usioutegemea mfano kuna mitandao ilikua maarufu sana zamani kama Hi5 lakini umaarufu wake kwa sasa umepungua au kupotea kabisa. Hivyo, uwezekano wa kudorora kwa biashara yako kunategemea pia umaarufu wa mtandao wa kijamii unaoutumia, jambo linalichangiwa sana na ujio wa mitandao mipya ya kijamii kama Instagram, Whatsapp na TikTok. Hii kwako unaionaje? Nitaeleza Tofauti katika matumizi ya Mitandao ya Kijamii na Tovuti wakati Ujao.

Faida ni nyingi sana za matumizi ya website katika kuimarisha biashara yako kupitia ulimwengu wa Teknolojia. Tayari tumekuandalia makala maalum kupitia link hii hapa WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?.

Leo hii ntakwambia mambo 10 kuhusu umuhimu wa kuwa na tovuti katika biashara yako:

1. 93% YA MAAMUZI YA MTEJA KUHUSU MANUNUZI HUANZIA MITANDAONI:

Ili kuweza kupata wateja wapya, huna budi kuelewa watu huenda wapi kutafuta vitu kama suppliers, bidhaa na huduma mbalimbali kabla ya kufanya manunuzi. Injini za matafuto mtandaoni zimekuwa kimbilio namba moja huku GOOGLE Ikiziacha mbali Injini zingine kama Yahoo, Bing na Ask. Maana yake hii ni kwamba kama huna tovuti, jua mauzo yako ni 7% tu ya soko zima ambalo hujui kuwa unalo. Upo apo? Yani unapoteza 93% ya mauzo yako kila siku bila hata wewe mwenyewe kujua.

2. UWELEDI (PROFESSIONALISM)

Kama una malengo ya kuifanya biashara yako iwe kubwa duniani, halafu bado huna tovuti rasmi, jua kuna sehemu kubwa ya soko haitakupa kipaumbele watakapokuwa na uhitaji wa huduma/bidhaa ulizonazo. Kwa biashara zenye malengo makubwa kuwa na tovuti huwaweka kwenye nafasi za juu katika kupata tenda na wateja, na huonyesha Uweledi bora katika utendaji wa biashara kuanzia katika muonekano na utendaji wa tovuti. Inakadiriwa 80% ya watu duniani huonyesha kutokua na imani na Biashara ambazo hazina tovuti pale wanapotaka huduma/bidhaa fulani mtandaoni.

3. KUPATIKANA KWA URAHISI

Hebu fikira ila ahueni ya kupata kila unachokihitaji kwa urahisi, tena kupitia katika simu yako tu iliyo kiganjani kwako. Ndivyo ilivyo kwa tovuti ambayo inajieleza kwa kila kitu kama ilivyo tovuti maridhawa ya http://rednet.co.tz . Ile raha ya kupata taarifa, huduma au bidhaa kirahisi kupitia simu yako ya mkononi, hufanya wateja waongezeke maradufu na kusambaza sifa bora kwa uharaka sana katika jamii na katika mitandao ya kijamii hali kadhalika.

Hii huongezwa chumvi ya SEO (Search Engine Optimization) ambayo ni teknolojia iliyowekwa katika Injini za matafuto ya kimtandao inayowasiliana na tovuti yako na kuweka taarifa katika Injini hizo na hivyo kufanya taarifa za tovuti yako kuonekana haraka zaidi katika matafuto. Biashara imerahisishwa sana kupitia SEO kuliko kutumia Mitandao ya kijamii. Kama watu wanakwenda Google kutafuta taarifa, basi fahamu taarifa hizo hupelekwa hapo GOOGLE kwa kutumia teknolojia iitwayo S.E.O. Kufahamu zaidi kuhusu SEO gusa hapa chini

4. TANGAZO LA BURE MUDA WOTE

Tovuti yako inapokuwa hewani, maana yake biashara yako ipo wazi na inajitangaza muda wote na kufika sehemu zote duniani ambapo huduma ya internet inapatikana. Tangazo la bure kabisa hili. Kama tovuti yako ina ubora wa kuvutia zaidi katika muonekano, maudhui na utendaji, basi bila shaka biashara yako ina nafasi kubwa ya kufanya vizuri sokoni na kupata wateja wengi kila siku. Jiulize hivi, unapofunga ofisi/biashara yako wakati wa jioni kila siku, wateja wapya wanaweza vipi kupata taarifa sahihi muda watakaohitaji?turudi kwenye mada yetu, kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako? Hii pia inawezeshwa sana na teknolojia ya S.E.O.

5. KUTENGENEZA MABALOZI (TESTIMONIALS)

Nafahamu wafanyabiashara wengi ambao hulazimika kuonyesha shuhuda/testimonials katika kurasa zao mara kwa mara ili kuendelea kupata wateja wapya zaidi, ni jambo jema kabisa. Kupitia tovuti yako, unaweza kuweka testimonials kwa idadi uitakayo bila kurudia rudia na katika mpangilio maalum na watu wakaweza kuona ushahidi utakaowaridhisha kuendelea kutumia huduma/bidhaa zako. Mara nyingi Mitandao ya kijamii huzuia kuoneka kwa biashara kwa urahisi kutokana na wimbi la watumiaji wenye maudhui tofauti tofauti katika ratiba ya saa (timeline) yako unayopitia katika mitandao hio, hivyo kusababisha usumbufu (distractions) katika biashara yako.

6. UAMINIFU (TRUST)

Hamna kitu muhimu katika uendeshaji wa biashara na kukuza mahusiano na mteja kama UAMINIFU. Ili kupata wateja wa kudumu katika sekta nyingi, kuwa na tovuti hai ni muhimu katika kudumisha mahusianao katika ya mfanyabiashara kwa muda wowte mteja atakaohitaji.

7. POSITIVE ROI

Ikiwa ni Return On Investment (ROI) au Rejesho baada ya Uwekezaji, unapoendesha biashara ambayo ina gharama zake kama umeme, kodi, maji, mafuta n.k, ukijiuliza utaweza vipi kurudisha gharama hizo upate faida? Njia moja nzuri ni matumizi ya tovuti bora yenye uwezo kunasa wateja wapya kwa njia ya mtandao muda wote (24/7) kirahisi kabisa.

8. THAMANI INAYODUMU

Uzuri/Faida moja muhimu kuhusu tovuti ni kwamba, unapoitengeneza una uhakika wa kuimiliki milele na kuifanyia marekebisho muda wowote itakapohitajika kufanya hivyo. Hivyo thamani ya biashara yako itaendelea kuwepo muda wote tovuti yako inapokuwa hewani.

9. HUDUMA BINAFSI YA MSAADA KWA WATEJA

Tovuti yako inapokuwa hewani 24/7 una uhakika na kutoa huduma bora kwa mteja mmoja mmoja kuhusu maulizo ya huduma/bidhaa ulizonazo, bei, ushauri nakadhalika. Hivyo kuimarisha mahusiano na ukaribu wako na wateja wako wakiwa popote duniani kwa urahisi kupitia miundombinu mbalimbali unayoweza kuiweka katika tovuti yako kama matumizi ya chatbots na barua pepe maalum za kibiashara (zenye jina/domain name ya tovuti yako).

10. MASIJALA (DATA CENTER) RAHISI YA MTANDAONI

Tovuti yako inaweza pia kuwa masijala rahisi kwa wafanyakazi, wateja na mtu yeyote anayehitaji kujua taarifa kuhusu huduma/bidhaa unazohusika nazo. Mfano mzuri ni tovuti yetu maridhawa ya http://rednet.co.tz ambayo zaidi tu. ya kwamba inatoa taarifa kuhusu huduma tunazohusika nazo za kutengenza websites, softwares, apps n.k, lakini pia tovuti inatoa taarifa muhimu mbalimbali kuhusu Biashara, Uchumi na Teknolojia. Taarifa hizi zimetengenzwa mahsusi kwa ajili ya kuimarisha Biashara za wateja wakiwa popote duniani. Pia taarifa hizo zinalenga kuhamasisha matumizi ya Teknolojia katika njanja mabimbali za kiuchumi haswa kwa wafanyabiashara waliopo kusini mwa jangwa la Sahara.

NOTE: Katika ulimwengu wa kisasa wa Dijitali, ili kutengeneza nafasi ya kupata wateja zaidi huna budi kuwa na Tovuti hai itakayobeba taarifa muhimu kama jina la biashara, anuani, mawasiliano na maudhui kuhusu huduma na bidhaa zako. Zaidi, weka pia matumizi ya SEO kuongeza kasi.

BONUS POINT: Tovuti yako unapoisajili, unashauriwa pia upate kirurushi cha barua pepe yenye jina/domain name sawa na tovuti yako. Mfano, tovuti yako inapatikana katika anwani ya www.mfano.com, hivyo barua pepe yako ya kiofisi unaweza kuchagua kuwa info@mfano.com au maulizo@mfano.com au jinalako@mfano.com. Kwa kutumia barua pepe zenye jina sawa na anwani ya tovuti yako, unajiweka katika nafasi nzuri ya kuimarisha biashara yako na kuongeza wateja wapya na kazi zenya manufaa haraka zaidi katika biashara/kampuni yako. Hii ni sababu muhimu sana unapojiuliza kwanini ni muhimu kuwa na website (tovuti) rasmi ya biashara yako. Website inakufanya unakuwa official kiukweli kweli.

Pia kuna makala hizi hapa ambazo zitakupa mwanga zaidi kuhusu namna bora za kuimarisha uchumi wa biashara yako kwa kutumia Teknolojia:

  1. UKIRITIMBA KATIKA BIASHARA, NI ASALI AU SHUBIRI?
  2. BRANDING vs MARKETING, KIPI NI KIPI?
  3. KUANZISHWA KWA ENEO HURU LA BIASHARA BARANI AFRIKA (AfCFTA), KUNA MANUFAA GANI KWAKO?
  4. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO.

Umejifunza nini kupitia makala hii ya kuhusu kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako? Tafadhali unaweza kuwasilisha maoni yako kupitia sanduku la maoni (comments box) lililo hapo chini au kuwasiliana nasi kupitia mawasiliano yanayopatikana katika Footer Bar chini kabisa ya ukurasa huu. Pia usisite kuwashirikisha wenzako makala haya kwa kushare link yetu ya https://rednet.co.tz mara zote. Karibu!

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?

FAHAMU ATHARI ZA JANGA LA VIRUSI VYA CORONA (COVID-19) NA JINSI YA KUPAMBANA NALO KATIKA BIASHARA BARANI AFRICA

Ugojwa wa homa ya mapafu unaosababishwa na virusi vya Corona umetangazwa kama janga la kidunia baada ya kuathiri maelfu ya watu duniani kote. Janga hili linatajwa kuzorotesha uchumi wa kidunia. Ugonjwa huu unasambaa haraka na namba ya wagojwa na waathirika inakwenda ikibadilika kila siku. Makala haya yanaakisi takwimu za ugojwa kufikia March 9, 2020.

Takribani wiki kumi na mbili (12) zilizopita nchi ya China iliripoti uwepo wa virusi vipya kwa mujibu wa shirika la Afya duniani (WHO). Virusi hivyo vinavyotambulika kama SARS-CoV-2 Vinavyosababisha ugonjwa wa Corona, COVID-19 ambao ulisambaa haraka sana katika jiji la Wuhan na baadae kusambaa China nzima. Nchi hio imekumbwa na changamoto kubwa katika nyanja ya huduma za kibinadamu ambapo zaidi ya visa 80,000 vimesharipotiwa vikisababisha vifo vya watu takribani 3,000 nchini China peke yake. Uginjwa huo tayari umeshavuka mipaka kufikia maeneo mbalimbali ya dunia kama Asia Mashariki (Korea Kusini iliyoripoti visa 7,000, hali kadhalika Singapore na Japan), Mashariki ya Kati (ikianzia Iran iliyoripoti visa 6500), Bara Ulaya (ikijumuisha eneo la Lombardy Kaskazini mwa Italy lililoripoti visa zaidi ya 7,300 na kusambaa zaidi maeneo mbalimbali mwa bara Ulaya ), Marekani ambapo vimeripotiwa visa zaidi ya 200.

Leo hii uchumi wa china ambao umepata ushawishi mkubwa katika uchumi wa dunia ikichangia kwa 17% ya GDP ya dunia nzima huku sekta ya biashara ikichangia 34% ya GDP ya ndani. takwimu hizo ni zaidi ya hali ilivyokuwa mwaka 2003 wakati ugonjwa wa homa ya mafua ya ndege (SARS) ulipolipuka kwa mara ya kwanza.

Ripoti ya Frost & Sullivan inasema kwamba katika hali mbaya zaidi au janga ambapo ugonjwa utaathiri watu wengi zaidi duniani kabla haujadhibitiwa mpaka kufikia mwezi June-July, pato la taifa (GDP) katika ngazi ya dunia litashuka chini kwa 2%.

Changamoto: Unaweza vipi kufanya biashara kwa kupitia mtandao katika hali ya majanga kama ilivyo sasa?

Kwa mujibu wa taasisi ya NRF (National Retail Federation) ya nchini Marekani, imekadiriwa kwamba biashara za rejareja zitabakia katika hali yake ya ukuaji zikiwa na 3.7% mpaka 4.2% ya kiwango cha ukuaji. Hata hivyo, serikali mbalimbali duniani zimekuwa zikichukua hatua kadhaa wa kadha katika kukabiliana na homa hio ya virusi vya COVID-19 ikiwemo kupulizia dawa katika sehemu mbalimbali zinazohusisha mikutaniko ya watu kamaa vituo vya mabasi, vituo vya treni, viwanja vya ndege, bandari, barabara za mitaani, maofisini, shuleni na vyuoni. hata hivyo, watu wamehimizwa kubakia majumbani mwao na kuwatenga wagonjwa na washukiwa wa ugonjwa huo kwa muda mpaka pale watakapopona.

Unaweza Vipi Kuhamishia Biashara yako Mtandaoni?

Kuanzisha biashara ya mtandaoni kunahitaji juhudi zaidi kukabiliana na changamoto za kisheria na maswala ya fedha ambazo haziepukiki. Ni muhimu sana kupata ushauri wa kisheria kutoka kwa wataalamu ambao ni wanasheria na mawakili pamoja na wahasibu na wabobezi wa maswala ya kifedha kabla hujaanza biashara ya kimtandao. Hata hivyo, utakapofikia utayari wa kufanya biashara katika mtandao, utahitaji kiasi kidogo zaidi cha pesa kumudu gharama za uendeshaji wa biashara kuliko ilivyokuwa awali.

Uzuri wa matumizi ya internet ni kwamba unaweza kuzindua biashara na kujipatia pesa katika mtandao kwa mtaji kiduchu au wakati mwingine bila ya hata kuwa na mtaji wa kuanza nao. Kama ukiuelewa mfumo wa uendeshaji wa masoko ya kimtandao (online marketing), au ukiwa mashuhuri katika mitandao ya kijamii, ni dhahiri utaona wepesi sana kufanya biashara yako katika mitandao ya kijamii na internet. hata hivyo, haikuhitaji kuwa nguli ili kuanza biashara mtandanoni.

1. Chatbot business

Unazifahamu chatbot? Bila shaka. Hii ni njia mpya na bora zaidi ya kuwasiliana na wateja wako ambapo ukifungua tovuti nyingi za kisasa utaona alama ya kuandika ujumbe ambayo mara nyingi huandikwa (chat, chat with us, ) au mara nyingine utaona alama ya kuandika ujumbe. Ujio wa Chatbot umerahisisha sana kuwasiliana kati ya Biashara/Kampuni na mteja moja kwa moja. hivyo matumizi ya Chatbot yamerahisisha sana huduma bora kwa wateja na kuboresha utoaji wa bidhaa zinazoendana na mahitaji ya wateja. Matumizi ya mitandano ya kijamii kama Facebook, Instagram na Whatsapp yamefanya matumizi ya Chatbots kuwa mepesi na rahisi zaidi kutumia.

3. Ad management business

Katika dunia ya leo iliyojaa ushindani mkali wa kibiashara, kama hujajua soko lako liko wapi ni ngumu sana kukabiliana na washindani wako ambao wengine unaweza usiwajue kama hautakuwa makini na kufuatilia taarifa na mienendo ya matakwa ya wateja kwa wakati. Matangazo katika biashara ndio moyo wa kuendesha soko lako katika uelekeo unaotakiwa (wa kutengeneza faida). Sasa ndani ya majanga kama Ugonjwa huu wa Corona ambapo watu wengi duniani wanahimizwa kufanyia kazi zao majumbani. huna budi kutangaza biashara yako kupitia matangazo ya kulipia katika injini kama Google, Bing na Ask pamoja na mitandao kama YouTube, Instagram, Twitter na LinkedIn. Hii inasaidia sana kuwafikia wateja wengi wenye uelekeo na uhitaji wa huduma/bidhaa zako katika muda mchache na hivyo kuongeza wateja wako duniani kote bila ya kulazimika kufanya maonyesho au semina. Kama bado hujajua jinsi utaweza kutangaza biashara yako kupitia huduma kama Google Adsense, tafadhali wasiliana nasi tukupatie ushauri mzuri wa jinsi ya kufanya.

Tizama hapa, kwa mujibu wa ripoti ya eMarketer, matumizi katika matangazo ya kidijitali nchini Marekani peke yake yatayazidi matumizi ya matangazo ya kawaida (traditional ads) kwa mara ya kwanza mwaka huu 2020. Mpaka kufikia mwaka 2023 matumizi ya matangazo ya kidijitali yatayazidi yale ya kawaida kwa theluthi mbili ya jumla ya matumizi ya sekta nzima ya media.

4. SEO business

Huitwa Search Engine Optimization (SEO) ambayo ni huduma inayorahisisha upatikanaji wa taarifa za kibiashara au binafsi kirahisi zaidi katika injini za kutafuta taarifa kama Google, Bing na Ask. Mada hii ya SEO imekuwa ikijadiliwa na kutumika sana duniani lakini sasa ndio wakati mahsusi wa kuhakikisha biashara yako inapatikana kirahisi katika injini za kutafutia taarifa. Ukweli ni kwamba wakati matangazo ya kulipia yanapozidi kushamiri duniani kwa kiwango kikubwa nyakati hizi, uwezo wa taarifa za biashara yako kuonekana kirahisi katika injini za kimtandao kama Google bado hakuna ushindani mkali, hata hivyo eneo hili linabaki kuwa na thamani zaidi katika kuendesha bishara kisasa zaidi na kurahisisha upatikanaji wa taarifa.

Linapokuja swala la kutafuta maneno muhimu (keywords) kupitia injini za kimtandao, thamani ghafi ya SEO huonakana pale taarifa inayotakiwa kuonekana juu zaidi katika majibu baada ya kutafuta. Takribani 40% ya watu hugusa jibu la kwanza katika injini baada ya kutafuta na hivyo ukurasa wa kwanza hujumuisha 91% ya taarifa zilizotafutwa na kusambazwa, ikionekana juu kabisa katika SERPs (Google Search Engine Results Pages) hivyo kufanya njia hii ya SEO kutumiwa zaidi na wadau wa masoko ya kimtandao duniani kote.

5. Vacation rental business

Mahsusi kwa wale wafanyabiashar wa nyumba za kupanga, hoteli pamoja na nyumba za wageni (Guest Houses and Lodges), biashara ya kupangisha nyumba imekuwa ikishamiri sana zama hizi za mapinduzi ya kidijitali. Japokuwa biashara hii haitajwi sana katika mada mbalimbali duniani, inaweza ikakufanya ukafikiri kuhusu makampuni makubwa duniani kama AirBnB au HomeAway, kwingineko kuna biashara ndogondogo zilizopo mtandaoni kama InviteHome ya Michael Joseph na MyDalali ya Emmanuel Njavike kutoka nchini Tanzania na wengine wengi sana waliojikita maeneo mbalimbali duniani. Linapokuja swala la nyumba za kupanga na biashara inayohusu maswala hayo, makampuni huingiza kati ya 10% mpaka 40% katika mapato kulingana na viwango vya kupangisha nyumba duniani ambavyo hutegemea mahali nyumba ilipo na sera za utawala.

Kuanzisha biashara hii ya kukodisha nyumba mtandaoni maarufu kama udalali wa nyumba unahitaji mtaji kiduchu tu ikisaidiwa kwa kiasi kikubwa na uwepo wa miundombinu bora ya kimtandao (softwares and Applications) ambazo zinasaidia kuhifadhi taarifa pamoja na kuelekeza wapi nyumba/hoteli zinapatikana katika namna iliyo rahisi kutumika na mtu yeyote duniani.

6. Webinar business

Najua unachofikiri. Unawaza kwamba utaanzaje kufanya biashara yako kupitia kwa njia ya Webinar? unahisi kwamba huwezi kufanya webinar? Sasa hakujawahi kuwa na njia rahisi ya kuwafikia wateja wako na kuwasiliana nao moja kwa moja kwa njia ya mtandao zaidi ya kutumia Webinar. Hata hivyo, webinar ni nini? Hii ni njia ya kufanya semina au kampeni moja kwa moja kwa njia ya mtandao. Unahitaji camera na Bando tu katika simu yako kufanikisha jambo hili. Jiulize, kuna mtu mwingine anaelewa biashara unayoifanya ikijumuisha huduma na bidhaa kuliko wewe mwenyewe? Sasa hii inakupa nafasi ya kuwakusanya wateja na wafanya biashara wenzako na kuwaelezea nini unachokifanya, offer, kampeni maalum unayoendesha na bidhaa/huduma mpya. Hayo yote unaweza kuyafanyia nyumbani kwako tu na kuwafikia maelfu wa watu ulimwenguni kote. Unaweza au huwezi?

Jambo la kufurahisha zaidi ni kwamba, hulazimiki hata kuwa na bidhaa/huduma zako pekee ndio uweze kufanya webinars. Mtaalamu wa webinars Jason Fladlien ambaye ni muanzilishi mwenza wa kampuni ya Rapid Crush alifanikiwa kutengeneza utajiri wa takribani dola milioni 100 za kimarekani kwa kuuza bidhaa mbalimbali kupitia webinars. Alichofanya ni aliwakusanya watu kama inavyofanyika katika magroup ya whatsapp, then wanapokuwa online anakuw anaendesha vipindi vya mauzo na hivyo kujipatia wateja kirahisi kabisa. Umeshaiona nguvu ya webinars sasa?

Njia bora ya kuanza kufanya biashara kupitia Webinars ni kutafuta bidhaa au huduma utakayoweza kuipigia chapuo, unatafuta watu sahihi wenye uhitaji na bidhaa/huduma hio halafu unawasha kamera yako na kuendesha kipindi kuhusu bidhaa/huduma hio. Kanuni hio iliyoanza kutumiwa na Fladlien na baadaye ikachukuliwa na bwana Russell Brunson ambaye kwa kushirikiana na bwana Jim Edwards walitengeneza software iitwayo Funnell Script, mahsusi kabisa kwa ajili ya kufanyia shughuli za webinars.

7. Business coaching

Business coaching au mafunzo na ushauri wa kibiashara ni kipawa ghafi (skills) sana haswa nyakati hizi za mapinduzi ya kiteknolojia na biashara za kimtandao. Watu wanaohodhi vipawa hivi vya kutoa mafunzo na ushauri wa kibiashara wamekuwa na nafasi muhimu sana nyakati hizi kwa kuzingatia msaaada wa majukwaa mbalimbali na mitandao ya kijamii.

Watu wabobezi kama Dan Lok, Simon Sinek na Joel Nanauka wamekuwa mashuhuri sana katika biashara hii ya mafunzo na ushauri wa kibiashara wakifuatiwa na wataalamu wengine wengi duniani. Mafanikio yao yamejengeka katika matumizi ya mitandao kama YouTube na Zoom ambapo kupitia majukwaa hayo, wafanyabiashara pamoja na watu wengine wanaotaka kujifunza vipawa mbalimbali katika uwanda wa kibiashara hujiunga huko na kupata elimu wakiwa popote duniani. Jinsi nzuri ya kufanikiwa katika biashar hii ni kuhakikisha unaonyesha thamani katika biashara za watu wanaofuatillia maudhui katika chaneli akaunti zako za mitandao ya kijamii, na baadaye wakulipe katika utendaji wao wa kibiashara za kila siku.

Kwa kifupi hizo ni baadhi ya njia ambazo unaweza kuzitumia kuhakikisha biashara yako inaendelea kuwepo karibu na wateja wako haswa katika kipindi hiki cha majanga ya homa ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona (Covid-19). Suluhisho mbadala linapatikana katika mapinduzi ya 4 ya viwanda yanayoendelea duniani yakichochewa na kasi ya ukuaji wa kiteknolojia na internet.

Anza kufanya biashara yako leo kwa kutumia moja kati ya njia zilizoelezewa hapo juu kisha jikinge na Corona pamoja na majaga na matishio mengine yanayoweza kutokea duniani kama vita, tufani, mafuriko na tofauti za kidiplomasia kama ambavyo ilitokea mwaka 2019 nchini Afrika Kusini kulipotoea machafuko na mauaji ya raia wa kigeni yaliyoitwa Xenophobia.

Usisite kuwasiliana nasi katika kubadili biashara yako kuelekea katika miundombinu ya kimtandao, kwa uchache kama ilivyoainishwa katika makala haya. USIBAKI NYUMA!!!

UMUHIMU WA TAKWIMU KATIKA UTOAJI WA HUDUMA BORA KWA WATEJA

Mteja hakosei na mteja ni mfalme. Hizi ni kauli maarufu sana katika biashara duniani, lakini haswa biashara zinazofanyika kusini mwa jangwa la Sahara. Maana yake ni kwamba, Mteja anatakiwa kusikilizwa na kuridhishwa na huduma/bidhaa zinazotolewa na mfanyabiashara. Je, wewe unatumia mbinu zipi ili kuhakikisha huduma/bidhaa zako zinawaridhisha wateja wako? Katika makala yetu ya leo utakwenda kufahamu kwa undani siri na umuhimu wa takwimu katika utoaji wa huduma bora kwa wateja. Twende pamoja mpaka mwisho.

Sasa ripoti ya mwaka 2019 kutoka shirika la kimataifa la ukaguzi wa mahesabu la PwC imeonyesha kwamba 64% ya Wakurugenzi wa Makampuni na Wafanyabiashara barani Afrika hawana data na takwimu kuhusu mwenendo wa wateja wao. Inashangaza eeh?

Kwa upande mwingine ripoti ya McKinsey imeonyesha kwamba makampuni yanayotumia data na takwimu sahihi kuhusu mwenendo wa wateja wao huyazidi yale yasiyofanya hivyo kwa 85% katika ushindani wa masoko na 25% zaidi katika kuingiza mapato kila mwaka.

Zaidi 95% ya wateja huongelea zaidi huduma mbovu walizokutana nazo katika kampuni/biashara fulani (Mtandao wa American Express), hali kadhalika 89% kati yao huacha kabisa kufanya biashara na kampuni/biashara fulani baada ya kukumbana na huduma/bidhaa zisizokidhi mahitaji/viwango walivyotegemea (ripoti ya Huduma kwa wateja ya mtandao wa RightNow). Kama unaijali biashara yako na ungependa kuona inazidi kukua, makala haya ni kwa ajili yako.

Sasa Changamoto; Kuna umuhimu gani katika kumridhisha mteja wako katika biashara unayofanya baada ya kujua takwimu sahihi kuwahusu?

1. KUONGEZA MAHUSIANO MAZURI NA MTEJA; Mteja aliyeridhishwa na huduma/bidhaa zako atabaki kuwa mteja wako kwa muda mrefu zaidi kutokana na huduma bora anazopata kutoka katika kampuni/biashara yako. Hakikisha unamshirikisha mteja kufanya maamuzi katika mchakato mzima wa kuhudumia. Muulize maswali kama Unaonaje ikiwa hivi au ikionekana vile, Unajiskiaje. Mpeti peti mteja wako muda wote kama unataka aendee kutumia huduma/bidhaa zako.

2. Waswahili wanasema, Kauli Njema ni silaha. Yaani unapokuwa na Kauli njema katika kusambaza huduma/bidhaa zako, unaiweka bishara/kampuni yako katika nafasi nzuri ya kuishindani dhidi ya washindani wako katika soko. Kauli njema ni kama sumaku ambayo inawaleta pamoja wateja na huduma/bidhaa zako na hivyo kufanya wateja wako kuendelea kuwa wako, lakini zaidi kauli njema huwavuta pia wateja wapya kuanza kutumia huduma/bidhaa zitokazo katika biashara/kampuni yako.

umuhimu wa takwimu katika utoaji wa huduma bora kwa wateja

3. KUPUNGUZA GHARAMA ZA MATANGAZO; Kampuni/biashara yako inapotoa huduma bora kwa wateja wake huwafanya wateja hao kuwa mawakala ambao hutangaza huduma bora wanazopata katika kampuni/biashara hio. Kama tulivyoona hapo mwanzo, 95% ya wateja duniani hueleza katika jamii zao jinsi walivyokutana na huduma mbovu/dhaifu walizokutana nazo katika kampuni/biashara fulani. 89% kati yao huacha kabisa kujihusisha na bishara/kampuni ambayo haikuwapatia huduma bora au haujali wateja wake. Hata hivyo bado ni muhimu sana uendelee kuitangaza biashara yako. Gusa hapa kufahamu kwanini.

Na njia bora kabisa ya kutoa huduma bora na kwa wakati huo huo ukipunguza gharama za matangazo ni kwa kutumia teknolojia kama website iliyounganishwa na huduma za S.E.O. Kwanini uwe na website? Majibu yanapatikana kwenye makala hii hapa kufahamu kwanini ni muhimu kuwa na website rasmi ya biashara yako.

4. MAFANIKIO KATIKA BIDHAA/HUDUMA ZIJAZO; Kampuni/biashara hujiweka katika nafasi nzuri ya kufanikiwa katika kusambaza huduma/bidhaa zake mpya pale inapokuwa na kumbukumbu nzuri katika kutoa huduma bora kwa wateja wake.

Matokeo yake, kampuni/biashara hulenga wateja wake wa kudumu katika kusambaza huduma/bidhaa zao mpya ambapo hujihakikishia mafanikio kabla ya kuwasambazia wateja wapya. Hata hivyo wateja wanaoridhishwa na huduma bora zitolewazo hupendelea bidhaa/huduma mpya zitokazo katika kampuni/biashara walizowahi kuhudumiwa vizuri hapo mwanzo.

5. MTEJA WA KUDUMU NI LULU; Kwa mujibu wa Ikulu ya Marekani (#WhiteHouse) Ofisi inayoshughulikia maswala ya wateja, kwa wastani, mteja aliyeridhika na huduma/bidhaa (mteja wa kudumu) katika biashara ana thamani mpaka mara 10 zaidi kuliko thamani ya manunuzi yake ya kwanza.

Tafiti zingine zimeonyesha kwamba ni ghali zaidi ya mara 6 mpaka 7 kumpata mteja mpya kuliko kumtunza mteja wa aliyepo/wa kudumu. Taasisi za kifedha, mabenki na makampuni ya simu kwa mfano, yamejifunza sana katika hili, hivyo hawaoni tabu kuchukua hatua za ziada kuhakikisha mteja ambaye hakuridhishwa na huduma anapatitwa suluhu mbadala haraka sana kuendana na mahitaji yake. Hapa ndio utauona umuhimu wa takwimu katika utoaji wa huduma bora kwa wateja.

6. WANAWEZA KUACHA KUWA WATEJA WAKO MUDA WOWOTE; Si jambo la ajabu hasa katika zama hizi za usasa mteja kuhamia kampuni yoyote atakayopenda kutumia huduma/bidhaa zake. Hii huchochewa zaidi na huduma mbovu/dhaifu za wateja wanazopatiwa zikiwemo kusubirishwa muda mrefu katika kupatiwa huduma/bidhaa/mrejesho/maoni kutoka kwenye kapuni/biashara fulani. Ni jambo lisolopendeza kabisa, lakini bado mambo kama hayo yanaendelea kutukia.

“Mteja anapokwambia hitaji lake, hakwambii tu kuhusu maumivu yake, anakwambia pia jinsi ya kutengeneza bidhaa/huduma itakayomfaa pamoja na biashara yenye ubora. Huduma kwa wateja zinatakiwa kubuniwa katika namna inayotambua changamoto hizo.” Anasema Kristin Smaby katika mtandao wa https://alistapart.com.

Huwezi kupata wateja watakaoridhika na bidhaa/huduma zako milele. Hivyo yakubidi kama mfanyabiashara kuzitafuta changamoto zinazowakabili wateja wako kwa; kuzungumza nao, waulize maswali kuhusu vile wanataka kujiskia ukiwahudumia, wape msaada pale watakapohitaji, wape ofa, punguzo la bei na mambo kama hayo. Utakapowahudumia vizuri wateja wako utakidhi mahitaji ya wote; biashara yako na wateja pia. Wao wanapata huduma bora, biashara inapata mapato na kila mmoja anabaki na furaha.

Njia bora zaidi ya kuhakikisha unazipata changamoto zinazowakabili wateja wako ni Kwa kutumia vizuri mitandao ya kijamii. Mitandao ya kijamii ni kiungo muhimu sana cha kuunganisha mfanyabiashara na wateja wake katika kuimarisha viwango vya utaoji huduma. Sasa unawezaje kuitumia mitando hii kwa usahihi? Tafadhali fuatana na link hii hapa.

Ni matumaini yangu leo umefahamu kwa undani umuhimu wa takwimu katika utoaji wa huduma bora kwa wateja. Utakwenda kuzitumia vipi mbinu hizi za leo? Niambie kwenye comment hapo chini..

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo kuhusu umuhimu wa takwimu katika utoaji wa huduma bora kwa wateja.

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu(website design, logo design, Digital consultacy n.k) BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?
mapinduzi ya kiteknolojia katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi

MAPINDUZI YA KITEKNOLOJIA KATIKA SEKTA YA USAFIRISHAJI NA UCHUKUZI

Ubunifu wa kiteknolojia na zama za Kidijitali huathiri karibu kila mchakato katika utendaji na uendeshaji wa mfumo wa Usafirishaji na Uchukuzi duniani kote. Kuanzia njia na namna ya usafirishaji wa majini/baharini, ardhini na angani, usimamiaji wa mizigo pamoja na shughuli za utawala na ugavi zikiwemo utaratibu/usimamizi wa nyaraka na ufuatiliaji mzuri wa malipo. Leo sasa tuangazie mapinduzi ya kiteknolojia katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi. Kuna nini kinaendelea huko? Makinika..

Idadi wa watu duniani itaongezeka kutoka watu bilioni 7.4 mpaka watu bilioni 10.6 kufikia mwaka 2050, vile vile idadi ya mizigo inayosafirishwa kwa njia ya meli peke yake itaongezeka mpaka mara 4 ambayo inatarajiwa kukua kwa ongezeko la 715% kwa nchi za Africa.

Pia kasi ya ukuaji wa miji itakuwa kwa 56% ya idadi ya watu katika Africa mpaka mwaka huo 2050. Ongezeko hili linatarajiwa kuchagizwa na kasi ya ukuaji wa miji, kukua kwa kipato cha mtu mmoja mmoja, kupenya kwa matumizi ya intaneti pamoja na urahisi wa kupata na kutumia Teknolojia mpya.

Hata hivyo mtindo wa uchukuzi wa mizigo kwa kupitia njia ya meli kwa kutegemea nyaraka peke yake unatarajiwa kupungua kwa kiasi kikubwa kufuatia ujio wa matumizi ya nyaraka za kielektroniki na barua pepe. Hii ni kwa mujibu wa Shirika la Kimataifa la EY.

Kufuatia kasi hio ya ukuaji na mabadiliko, makampuni na biashara zilizopo katika sekta ya Usafiri na Uchukuzi yanahitaji kubadilika ili kumudu kuwepo katika ulimwengu ambao ushindani unakuja kutoka pande zote na teknolojia za kidijitali ndio zitakuwa chachu kuu ya mabadiliko.

Sasa Swali; Teknolojia Inaweza vipi kubadili Kesho ya Sekta hii ya Usafirishaji na Uchukuzi kwa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara?

Leo hii sehemu kubwa ya shughuli za kiuchumi na kijamii hufanyika mtandaoni na haswa haraka zaidi kupitia katika simu janja (smartphones). Ukuaji huu wa kiteknolojia unanufaisha maeneo yote yaliyomo kwenye Sekta hii ya Usafirishaji na Uchukuzi kama; usafiri wa magari ya mizigo (malori), usafiri wa kimataifa (njia ya anga na majini), usimamiaji wa shughuli za ugavi na kuratibu safari za majini, nchi kavu na angani. Yafuatayo ni mapinduzi ya kiteknolojia katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi barani Afrika;

1. MFUMO WA KURATIBU SAFARI/ONLINE TRACKING SYSTEM (Magari ya mizigo, Meli na Anga): Imezoeleka mteja kuhifadhiwa nafasi ya kusafirisha mizigo yake kwa kujaza fomu fulani ya usafirishaji, halafu anaachwa gizani mpaka siku mzigo wake unamfikia asipoamua kufuatilia kwa kupiga simu. Lakini leo, kwa kutumia huduma za intaneti na programu za kompyuta mteja anao uwezo wa kuagiza na kufuatilia kwa ukaribu zaidi mizigo yake muda wowote akihitaji kufanya hivyo.

Usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika.Mapinduzi ya kiteknolojia katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi

Hii si tu kwamba imerahisisha matumizi ya intaneti kisasa zaidi lakini zaidi teknolojia hii inaokoa muda na gharama za ziada kwa kampuni ya usafirishaji na mtu binafsi.

2. TEKNOLOJIA YA INTERNET OF THINGS (IoT) na RADIO FREQUENCY IDENTIFICATION (RFID): Ulishawahi kufikiria siku fulani una uwezo wa kuwasha feni yako nyumbani kwa kutumia simujanja yako? Sasa leo hii vifaa vingi vya kielektroniki vimeundwa na uwezo wa Wi-Fi na vifaa vya kuhisi mazingira mbalimbali. IoT inafungua nafasi nyingi sana katika kurahisisha shughuli za ugavi kama kupunguza gharama za uendeshaji. Vifaa vya kuhisi mazingira (sensors) pia hufungwa katika magari madogo na makubwa, meli za mizigo, treni na kadhalika. Vifaa hivi hufungwa mfumo wa kengele au mfumo wa GPS ambayo hufuatilia na kuratibu mwenendo wa mzigo kumfikia mteja.

Hali kadhalika teknolojia ya RFID ambayo imeshatumika miaka kadhaa hutumiwa na makampuni ya uchukuzi na usafirishaji kufuatilia mwenendo wa hesabu za bidhaa zao (Inventories). Kwenye teknolojia hii hujumuisha pia matumizi ya barcode za kwenye bidhaa, pamoja na matumizi ya rimoti za televisheni na redio, teknolojia ambayo imetumika kwa miaka mingi zaidi, hivyo kuyafanya makampuni mengi kutumia zaidi RFID’s. Vile vile RFID’s hutumika kusambaza bidhaa katika maghala yao na kuratibu mienendo ya makontena.

3.MAGARI/ MALORI YA KUJIENDESHA NA DRONES: Katika ulimwengu ambao unaendeshwa na matumizi ya kompyuta kutoka mahali fulani kwenda mahali kwingine, utajihisi vipi siku unapokea mzigo kutoka kwenye chombo kinachoruka angali mfano wa helikopta ndogo? Sasa huko ndipo tunapoelekea. Magari ya kujiendesha tayari yanaonekana duniani ambapo kampuni za UBER na EMBARK wametengeneza magari yanayojiendesha japokuwa bado miradi hiyo haijarasimishwa kwa wateja. Ni swala la muda tu kutoka sasa kabla matumizi yake hayajawafikia wateja ulimwenguni kote.

4. MITANDAO YA KIJAMII: Nani ambaye hapitii kwenye mitandao ya kijamii angalau mara moja kwa siku? Nguvu ya mitandao hii ya kijamii inaboresha kwa namna ya kipekee sana sekta hii ya Usafirishaji na Uchukuzi kwa ujumla wake. Mitandao hii inarahisisha sana katika kutangaza huduma za usafirishaji na uchukuzi pamoja na kampuni kuwasiliana na wateja wake kwa ukaribu na urahisi zaidi katika kutoa taarifa muhimu, dharura na mrejesho kutoka kwa wateja.

Kwa mujibu wa Hootsuite, 59% ya Wamarekani ambao ni watumiaji wa mitandao ya kijamii wamekubali kwamba huduma kwa wateja kupitia mitandao ya kijamii imerahisisha kujibu maswali na huduma husika.

Zaidi ya yote, miundombinu ya uchukuzi katika nchi za Afrika bado ipo nyuma sana kimaendeleo ukilinganisha na sehemu zingine za dunia. Nchi ya Afrika Kusini ndiyo inaongoza barani kwa kuwa na miundombinu ya kisasa zaidi ya kiuchukuzi ambapo kasi ya ukuaji wa miundombinu kwa mwaka ni ndogo kwa 3% katika kipindi cha mwaka 2012 hadi 2017. Hii ni kwa mujibu wa takwimu za Shirika la Fedha duniani (IMF).

Kwa upande mwingine nchi za Kenya na Nigeria zinaongoza kwa kuwa na ukuaji mkubwa katika miundombinu yake ya kiuchukuzi na usafirishaji kwa 6.2% na 6.8% katika kipindi hicho hicho (2012-2017). Kwa wafanyabiashara na makampuni ya usafirishaji na uchukuzi; Kuwekeza vema Afrika kunahitaji uelewa mzuri wa maeneo muhimu pamoja na uelewa wa masoko ya wenyeji.

Afrika si tu kwamba ni kubwa mno, lakini zaidi Kuna mtawanyiko mkubwa wa jamii za watu na rasilimali. Hata hivyo, zaidi ya 70% ya makampuni makubwa zaidi duniani yanayozalisha bidhaa za watumiaji tayari zinafanya kazi Afrika. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya shirika la kimataifa la PwC.

Usipitwe na Ofa Yetu katika msimu huu wa Nane Nane. Makala haya ya leo yamelenga wafanyabiasha kujidhatiti kidijitali kwa kutumia teknolojia za kisasa katika biashara zao za kila siku ili kuweza kunufaika vyema na masoko pamoja na fursa kede ndani na nje ya nchi. Umejifunza nini leo kuhusu mapinduzi ya kiteknolojia katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi? Share nasi mawazo yako kwenye comment au tucheki kwa kugusa WhatsApp namba yetu hii hapa 0765834754.

Makala hizi hapa zitakupa mwanga zaidi katika kuwekeza katika Biashara zinahohusiana na sekta ya Usafiri na Chukuzi hasa katika eneo la kusini mwa Jangwa la Sahara:

  1. FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA
  2. USAFIRISHAJI NA MIUNDOMBINU KATIKA USTAWI WA BIASHARA AFRIKA
  3. FAHAMU KUHUSU TEKNOLOJIA KATIKA SEKTA YA HABARI NA BURUDANI