Kwa mara ya kwanza katika Historia ya mwanadamu, zaidi ya nusu ya watu wote duniani wanatumia huduma za internet. Na katika maeneo yote, imeonekana huduma hizo zinakua kwa kasi zaidi barani Africa. Idadi ya watu wanaotumia internet imeongezeka sana barani Afrika kutoka 2.1% mwaka 2005 mpaka 24.4% mwaka 2018. Sasa leo nataka u fahamu mchango wa ICT katika maendeleo ya sekta binafsi barani Africa. Twende sambamba.
Huduma hizi za internet zimekuja kurahisisha shughuli za kiuchumi kama kurahisisha njia za malipo (bank, MPESA, tigopesa nk), matumizi ya drones katika matibabu kama inavyofanyika nchini Rwanda, matumizi ya smartphones katika kuongeza maarifa ya kitaaluma na kiufundi stadi na kuongezeka kwa biashara za mtandaoni (e-commerce businesses, network marketing and online businesses). Bill Gates amewahi kuandika katika moja ya tweets zake “If your business is not on the Internet yet, Your are out of the Business.” Mwenye macho haambiwi ona.
SEKTA BINAFSI, INJINI YA UCHUMI AFRIKA
Kama ulikua hufahamu, basi sekta binafsi ndio imetawala Uchumi wa Afrika kwa kuwa zaidi ya 80% ya uzalishaji mali mzima hufanyika katika sekta hio. Zaidi, theluthi mbili (⅔) ya uwekezaji mzima barani na robo tatu (¾) ya jumla ya mitaji katika uchumi kati ya mwaka 1996-2008 imeonekana kutokea katika sekta hio binafsi. Vile vile sekta hio inatoa 90% ya ajira zote kwa vijana walio katika umri wa kufanya kazi. Mchango wa biashara za ndani katika sekta binafsi katika GDP ilikua 59% katika nchi za kusini mwa Jangwa la Sahara ukilinganisha na 30% ya nchi za Latin America na Caribbean, 32% Asia Kusini na 42% katika Mashariki ya Kati. Hii inaonyesha kiasi gani Afrika sekta binafsi inalipa maradufu. Umeiona nafasi yako hapa ndugu yangu mfanyabiashara.!?
Kujiimarisha katika Sekta binafsi, huna budi kuwa na uwezo wa kufanya maamuzi sahihi kila mara unapohitajika kufanya hivyo. Unawezaje kufanya maamuzi sahihi katika changamoto zinazokukabili? Tafadhali fuatana nasi katika makala hii hapa FANYA MAAMUZI SAHIHI KATIKA MUDA SAHIHI.
Katika nchi za Uchumi wa kati, kampuni binafsi hufanya kazi katika mfumo wa sekta rasmi, ambapo makampuni makubwa na yale madogo (SME’s) huzalisha hisa za thamani katika uwekezaji na zaidi, ajira kwa vijana ambao ndio kundi kubwa zaidi katika nguvu kazi barani Afrika. Lakini zaidi, sekta binafsi katika nchi hizi hufanya ⅔ ya uzalishaji mzima.
Uchumi huwa na ushindani pale kunapokuwa na ushindani mkali wa kibiashara. Na biashara huwa na ushindani pale:
•Sheria zinapokua sawa na haki.
•Wafanyakazi wana maarifa stahiki.
•Gharama za uendeshaji (umeme, maji, mafuta, usafiri) zinakuwa nafuu.
•Wateja wanafikika kila kona.
ICT INAINGIA VIPI HAPO?
Uchumi wa kidijitali umekuwa dhima kuu ya kidunia na Afrika haijabaki nyuma katika hili. Matumizi ya teknolojia yanazidi kushika kasi barani yakichagizwa na kasi ya ueneaji wa huduma za internet ambapo biashara nyingi zinazidi kuhamia mtandaoni kirahisi. Mpaka kufikia mwaka 2015 tu tayari watu 557 barani walikua wanatumia simu ya mkononi ambayo ni 12% ya watumiaji wote wa simu duniani huku idadi hio ikikusanya 6% ya mapato yote yaliyofanyika duniani wakati huo.
Sasa leo wacha tuone maeneo muhimu ya ICT yanayokuza uchumi zaidi;
1. TELECOMUNICATIONS
Eneo hili linajumuisha makampuni makubwa ya mawasiliano. Kwa kiasi kikubwa hufanya shughuli zake katika utaratibu wa sekta rasmi, hivyo kuwafikia watu wengi na kufanya kazi karibu zaidi na mamlaka za serikali. Makampuni kama Vocacom, MTN, Tigo, Airtel na TTCL yapo hapa. Kutokana na kuwa na watumiaji wengi, makampuni haya huchangia kiasi kikubwa katika mapato ya kiserikali kama kodi na gawio huku yakichangia sehemu kubwa katika kukuza uchumi wa watumiaji wake kutokana na fursa zinazopatikana katika huduma wanazozitoa kama uwakala wa huduma, huduma za kifedha nakadhalika.
2. SOFTWARE AND IT CONSULTING
Hapa ndo utatukuta sisi sasa ambao tunakuhudumia wewe muda huu. Zaidi ya kukupatia taarifa hizi ghafi, pia eneo hili la ICT hutoa huduma za kutengeneza mifumo ya computer, Apps za simu, Ushauri na Uchambuzi wa kiteknolojia katika Biashara na Uchumi. Japokuwa sio maarufu sana lakini sehemu hii inachangia uchumi wa mabiashara mbalimbali, makapuni madogo na yale yanayokuwa (SME’s) pamoja na sekta zingine za uma na binafsi kwa kutoa huduma za matengenezo ya tovuti, mifumo mbalimbali ya kibiashara, huduma za afya, elimu, uhifadhi wa data pamoja na uchambuzi na ushauri wa biashara mbalimbali kiteknolojia zaidi.
3. DIGITAL SERVICES
Hapa utawakuta watu wanaotoa huduma za kidijitali ambao wengi wao hufanya kazi kwa ukaribu na makampuni ya mawasiliano. Watoa huduma hawa pia wanahusika kutengeneza mifumo ya makampuni ya mawasiliano pamoja na kutengeneza/kuendesha mitandao ya kijamii zaidi. Watoa huduma hawa wamekuwa wakitengeneza michezo ya video pamoja na kutoa huduma za WebHosting na Cloud services kwa makampuni ya Kiafrika. Kampuni kama Dudumizi Technologies(Tanzania), ISB North Africa (Morocco), Web4Africa (Ghana) na Domains Africa Technologies (Kenya) zipo hapa.
4. INFORMATION SERVICES
Hapa sasa ndio utazikuta redio na televisheni zote unazozifahamu. Hawa kwa jina lingine wanaitwa Watoaji wa Maudhui, ambapo hutafuta habari na maudhui wanayodhani yanafaa kwa wateja wao na hivyo kukusanya jamii ili ipate maudhui hayo huku yenyewe yakijipatia faida yake katika matangazo mbalimbali ya kibiashara yanayoruka sambamba na maudhui yao. Hapa unaweza kunitajia Redio/TV ambayo ina maudhui unayoyapenda yakienda sambamba na matangazo ya wadhamini wa vipindi vyao. Usishangae ukiona hivyo. Kwenye matangazo ndo wanapopatia pesa wenzio, usione unapata bure maudhui hayo.
Kwa uchache haya ndio mambo ya fahamu mchango wa ICT katika maendeleo ya sekta binafsi barani Africa yanayochangia kwa kiasi kikubwa kukua kwa Uchumi wa Kidijitali na kuboresha biashara nyingi zaidi kila kukicha barani Afrika. Jiulize, unayatumia vipi maeneo haya katika kukuza biashara yako wewe kama mjasiriamali?
Makala hizi hapa chini zitakusaidia kufahamu kwa undani namna sekta binafsi zinachangia uchumi na maendeleo ya wafanyabiashara hasa vijana wa Afrika Mashariki. Gusa links kisha makinika:
- KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE (TOVUTI) RASMI YA BIASHARA YAKO?
- UKIRITIMBA KATIKA BIASHARA, NI ASALI AU SHUBIRI?
- UNAFAHAMU NINI KUHUSU URASINISHAJI (HARMONIZATION) KATIKA BIASHARA
Usisahau kutoa maoni yako kuhusu ukichojifunza katika makala hii ya leo na unaweza kusambaza ili kuhakikisha ulichijifunza kinawafikia wengine. Pia unaweza kutembelea tovuti yetu maridhawa ya https://rednet.co.tz kuhakikisha unaendelea kupata taarifa sahihi kuhusu uchumi na biashara yako kiteknolojia. Asante.
Makala hii ni Kwa Heshima ya Hayati B.W. Mkapa aliyekuwa Rais awamu ya 3 nchini Tanzania. Mzee Mkapa aliongoza Taifa kuelekea zama hizi za maendeleo ya Sekta Binafsi kupitia Sera yake ya Ubinafsishaji wa mali za umma zilizokua mzigo kwa serikali, hivyo kuchochea ukuaji wa sekta binafsi kwa kiasi kikubwa mpaka kufikia hivi ilivyo leo. Mzee aliona mbali sana. #RIPMkapa