Category: Economic Updates

D.R.C NDANI YA E.A.C, MFANYABIASHARA ANAFAIDIKA VIPI?

Hatimaye tar29 March Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ilipata kibali cha kuwa mwanajumuiya wa Afrika Mashariki (EAC) na mwezi July mwaka huo 2022 DRC iliingia rasmi katika Jumuiya ya Afrika Mashariki baada ya kuwasilisha matakwa yote makao makuu ya jumuiya hio jijini Arusha. Hii ni baada ya kuendesha mchakato uliodumu kwa takriban miaka minne. Sasa DRC inapoingia ndani ya EAC mfanyabiashara anafaidika vipi?

DRC inakuwa mwanachama namba 7 wa EAC huku ikiwa ndio nchi kubwa zaidi kijiografia katika ukanda huo. Inasemekana DRC ndio nchi yenye rasilimali (madini, mafuta, misitu n.k) nyingi zaidi duniani. Pia nchi hio ina idadi ya watu takribani milioni 90 ambao ni mtaji muhimu kiuchumi.

MAMBO 10 USIYOYAJUA KUHUSU D.R.C:

Kukubalika kwa DRC kunamaanisha kwamba soko la Afrika Mashariki linatanuka na kuwafikia watu zaidi ya milioni 300 waishio ndani ya jumuiya hio tu, huku uchumi wa jumla ukiwa na thamani ya 250$ bilioni. Sasa DRC ina nini cha ziada usichokijua?

1. MIPAKA YA KIJIOGRAFIA:

Ikiwa ndio nchi ya pili kwa ukubwa wa jiografia barani, DRC inapakana na nchi zingine 9. Nchi hizo ni Angola, Burundi, Jumhuri ya Afrika ya Kati, Rwanda, Jamhuri ya Congo (Brazaville), Sudani Kusini, Uganda, Zambia na Tanzania. Muingiliano wa kibiashara ni mkubwa sana hapa.

Zaidi upande wa magharibi mwa jiji la Kinshasha inapakana na bahari ya Atlantiki. Sasa Kongo kupakana na nchi 9 na kuwa na ufukwe wa bahari ya Atlantiki kunaifanya iweze kutanua fursa kwa wafanyabiashara kupitisha mali kwenda nchi nyingi zaidi barani na hata nje ya bara.

DRC na mipaka yake. Milango ya biashara za kimataifa kwa EAC.

2. KUHUSU VIVUTIO VYA UTALII:

Mbuga ya wanyama kongwe zaidi barani ipo DRC, inaitwa Virunga. Hapo utawakuta wale Sokwe wakubwa (Gorillas), simba na tembo. Lakini mbuga hii ipo kwnye tishio la kutoweka kwa sababu kuna mafuta na kampuni ya Uingereza ya Soco tayari imetia timu kuanza kuchimba mafuta hapo mbugani.

Hawa gorilla ni kivutio kizuri sana cha utalii lakini miaka ya hivi karibuni wamekuwa adimu na kutokana na shughuli za mwanadamu, wanyama hawa wapo kwnye tishio la kutoweka kabisa. Je, DRC kuingia katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kutadhibiti hatari ya sokwe hawa kutoweka?

Kuhusu namna utalii unaweza kuleta manufaa katika biashara tafadhali fuatana na makala hii hapa chini:

3. KUHUSU MTANDAO WA BARABARA NA MIUNDOMBINU:

Ni 1.8% tu ya barabara nchini DRC ndio ina kiwango cha lami, huku chini ya 10% ya nyumba za makazi ndio zina umeme. Hii ni hali mbaya sana katika kukuza uchumi wa Taifa. Hata hivyo Benki ya Dunia imetangaza kifurushi za 1$ bilioni kwa ajili ya miundombinu ya DRC.

Moja kati ya vitu vinavyorudisha nyuma juhudi za wajasiriamali na mashirika kuwekeza nchini DRC ni maendeleo duni ya miundombinu. Ukizingatia ukubwa wa nchi hio, imekuwa ni nafuu kusafiri kwa njia ya anga kuliko barabara. Sasa @jumuiya itachangia vipi maendeleo ya miundombinu?

4. BIASHARA ZA NJE YA NCHI (EXPORTS):

Muziki wa DRC ndio mali inayouzwa zaidi nje ya nchi (export). Kuanzia miaka ya 90 muziki wa Bolingo ndio ulikua unasikilizwa na kupendwa zaidi bara zima la Afrika. Ndio maana wasanii kama Fally Ipupa na Koffi Olomide ni matajiri sana. Madini na malighafi zingine zote chali.

5. LUGHA INAYOTUMIKA ZAIDI:

Jiji la Kinshasa ni la pili kwa matumizi ya lugha ya Kifaransa likitanguliwa na jiji la Paris. Yaani Wakongo hawa wanaongea kifaransa zaidi kuliko hata miji ya nchini Ufaransa. Hata hivyo hii inachangiwa na idadi ya watu wanaoishi kwenye jiji hilo, watu milioni 10 mchezo!

Ukiacha Kifaransa raia wa Kongo pia wanazungumza lugha zingine kama Kilingala, Kiingereza, Kiswahili na lugha za makabila asilia. Hivyo ukiwa kama mfanyabiashara na moja kati ya lugha tajwa unazifahamu vyema basi nafasi ni yako kuingia DRC na kutanua biashara zako.

6. KUHUSU UGONJWA WA EBOLA:

Kwamba kupata Ebola nchini DRC ni rahisi kama kupata mafua ukiwa sehemu nyingine? HAPANA. Baada ya ugonjwa huo kufumuka mwaka 1995 na kuua watu zaidi ya 200, milipuko mingine ya ugonjwa huo imekuwa ikidhibitiwa kwa kiwango kikubwa. Hivyo Congo ni salama.

7. KUHUSU MADINI:

Lile bomu la atomiki lililodondoshwa kwenye miji ya Hiroshima na Nagasaki katika WWII lilitengenezwa kwa madini ya Uranium kutoka mgodi wa Shinkolobwe, mkoani Katanga nchini DRC. Hata hivyo mgodi huo ulifungwa mwaka 2004 kutokana na kuishiwa madini ukiiacha DRC patupu.

Kongo imenyonywa sana katika madini yake. Hali kadhalika nchi zingine katika Jumuiya zimepitia hali hio. Hivyo itakapowekwa sera ya pamoja ya kulinda na kusimamia rasilimali zilizopo ndani ya Jumuiya, bila shaka madini na rasilimali ambazo zipo DRC zitakuwa na manufaa sana.

8. HISTORIA YA UNYONYAJI:

Mfalme Leopold II wa Ubelgiji alijitangazia Kongo kuwa mali yake binafsi kuanzia mwaka 1870. Koloni hilo ndio lilikua mali binafsi kubwa zaidi kuwahi kumilikiwa na mtu mmoja kwenye historia. Umiliki huo ulisababisha vifo vya watu milioni10. Huu ndio mwanzo wa nchi kuharibika.

Mfalme Leopold II aliagiza watu kukusanya zao la mpira ambalo kwa kipindi hiko ndio lilikua zao bora zaidi la kibiashara. Wale walioshindwa kukusanya zao hilo kama kodi waliadhibiwa kwa kunyimwa chakula na kukatwa mikono yao. Ukatili huo ulikua mbaya sana dhidi ya ubinaadam.

9. HALI YA USALAMA NA VITA:

DRC imekuwa ikikumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe na migogoro isiyokwisha ambayo imepelekea vifo vya watu takriban milioni 6. Hali hio ya vita visivyokwisha imepewa jina la “Vita vya Dunia vya Afrika”.

Vita hivyo kwa sehemu kubwa vimekuwa vikisababishwa na vikundi fulani (kampuni, mashirika na raia wa kawaida) kugombania rasilimali katika eneo fulani. Huyu anataka kuchimba, raia wanataka kunufaika. Je, DRC kuingia kwenye @jumuiya itasaidia kumaliza janga la vita visivyokwisha?

10. KUHUSU MTO CONGO:

Ukiwa na urefu wa kilomita 4,700, mto Congo ndio mto mrefu wa pili barani Afrika ukitanguliwa na mto Nile. Pia huo ndio mto wenye kina kirefu zaidi duniani. Cha kufurahisha zaidi, Mto Congo na Mto Nile yote inapatikana katika EAC. Inakupa picha gani hii kiuchumi?

Je, EAC itaweza kuzalisha umeme wa pamoja kupitia sehemu za mto huo? Je shughuli za kiuchumi kama uvuvi, usafiri, utalii biashara ya mazao ya misitu zitaweza vipi kusimamiwa na Jumuiya kuhakikisha faida zinarudi kwa wanachi wa Kongo na wa jumuiya nzima kiujumla?

ZIADA: MSITU WA CONGO

Msitu wa pili kwa ukubwa duniani, msitu wa Congo unapatikana nchini DRC. Hata hivyo msitu huo ni mkubwa kiasi kwamba umeingia kwenye nchi zingine kama Cameroon, Jamhuri ya Afrika Ya Kati, Jamhuri ya Congo(Brazaville), Guinea ya Ikweta na Gabon. Msitu huu ni utajiri mtupu.

msitu wa mvua wa Congo
Msitu wa Congo

Katika msitu huo kuna fursa nyingi zikiwamo biashara ya magogo, madawa ya kutibu watu, mazao na wanyama, mbao, karatasi na bidhaa zote zitokanazo na misitu. Ukiwa kama mfanyabiashara ambaye sasa una uhuru wa kwenda kuwekeza DRC kirahisi, utaitumiaje fursa hii?

Sasa hayo ni baadhi ya mambo ambayo pengine ulikua huyafahamu kuhusu DRC. Mambo hayo kama yakifanyiwa kazi ipasavyo ndani ya @jumuiya basi ni wazi kutapunguza hali ya umasikini na kuimarisha amani kwa watu wa Kongo na kuimarisha uchumi wa Jumuiya nzima. Mapema mwaka 2021 jumuiya ya nchi za Afrika kwa kauli moja ilianzisha eneo huru la biashara barani (AfCFTA) ambapo nchi wanachama wanaweza kufanya biashara kwa uhuru bila ya vizuizi vya mipakani. Zaidi soma hapa chini

Jumuiya hii inatoa uhuru kwa wanachi wake kuishi na kufanya biashara popote ndani ya nchi wanachama. Jambo hili linatoa fursa kwa Wajasiriamali wa aina zote kuzurura na kutafuta masoko yao kirahisi. Ukiweza vema kutumia majukwaaa ya kimtandao kama websites, mitandao ya kijamii ujue unayo nafasi ya kuwafikia watu milioni 300 waishio ndani ya Afrika Mashariki. Sasa tuambie wewe mtu wa Teknolojia, website designer, mtaalam wa kutengeneza android app, mkulima, engineer nk, unataka ufaidike vipi hapa? Tuambie..

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER)5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

M-PESA LIPA NAMBA

MFUMO WA KUWEZESHA MALIPO BARANI AFRIKA (PAPSS)

Umeshawahi kuwaza kufanya biashara na wafanyabiashara wenzako na wateja kutoka nchi yoyote barani Afrika ambapo utaweza kutuma na kupokea fedha bila ya ulazima wa kubadili ziwe za kigeni kwanza? Sasa mfumo wa Kuwezesha malipo barani Afrika(PAPPS) unakwenda kukurahisishia mjasiriamali uwezo wa kutuma na kupokea fedha katika bidhaa/huduma unazotoa kila siku kirahisi zaidi. Leo nakupa fursa ya kufahamu namna mambo yamekuwa mazuri kibiashara barani Afrika. Fuatana nami mpaka mwisho wa makala hii..

Kwetu Moshi bwana ikifika mwezi February mpaka June kila mwaka huwa ni msimu wa parachichi na ndizi ambapo watu huuza sana parachichi ndani na nje ya nchi. Najua umeshawahi kuonja parachichi za Rombo, Marangu, Mwika, Machame nk, right?

Sasa bwana hizo parachichi unazokula ni 20% tu ya parachichi zote zinazovunwa kwenye miteremko ya mlima Kilimanjaro. Zaidi ya 80% ya parachichi hizo huuzwa nchini Kenya na kisha kusafirishwa kwenye barani Ulaya na Asia kupitia bandari ya Mombasa.

Bahati mbaya zaidi pale mpakani Holili kuna madalali wengi sana ambao hununua parachichi kutoka kwa wafanyabiashara kutoka sehemu mbalimbali na kuziingiza nchini Kenya. Hawa jamaa bwana wajanja sana. Wao tayari wana vibali vya kuingia na kufanya biashara kati ya Tanzania na Kenya na zaidi wanafanya pia biashara ya kubadilisha fedha hapo mpakani (japo sina uhakika kama wanafanya hivyo kihalali). Kwa kufanya hivyo hawa Madalali wamekuwa wakijipatia faida kubwa sana hapo mpakani japo kuwa wao hawana mashamba wala parachichi zenyewe. Wao wanaconnect dots tu.

Na bahati mbaya zaidi wafanyabiashara wengi wadogo hawawezi kuvuka mpaka wakakutana na wateja wenyewe huko Kenya na kuuza bidhaa zao direct. So unaweza kuona namna hawa ndugu zangu wanapata tabu kufanikiwa kwenye biashara yao japokuwa wao ndo wanamzigo wote wa parachichi.

Huu ni mfano mdogo tu unaowakuta wafanyabiashara ambao wanauza bidhaa/huduma zao nje ya nchi. Hali hio pia inawakumba wale wa Tunduma, Rusumo, Taveta na maeneo mengine ya mpakani ambapo madalali (watu wa kati) wamekuwa wakitumia fursa hio kujinufaisha zaidi kuliko wakulima.

Kupitia changamoto kama hizo ndio maana nchi wanachama wa AU wakaanzisha Eneo Huru la Biashara barani Afrika (AfCFTA) ili kuhakikisha biashara baina ya nchi wanachama zinafanyika kirahisi, tena bila vikwazo kama kodi na ushuru wa mipakani ambayo imekuwa ikiwaumiza wafanyabiashara.

Kuhusu AfCFTA ni nini na inafanya kazi vipi? tayari nimekuandalia makala murua kabisa kupitia link hii hapa chini:

Ukimalizana na makala hio sasa, tuendelee..

Pia nchi za kusini mwa Afrika kufikia July 2020 zikakubaliana kurasinisha biashara zao ili kuwezesha mazingira ya biashara baina ya nchi wanachama wa SADC kufanya biashara bila mrundikano wa kodi na ushuru. Hapa Prof. Kabudi (waziri wa mambo ya nje) na timu yake walicheza sana.

Kuhusu URASINISHAJI huo wa Kibiashara, ni nini na unafanyika vipi, tayari kuna makala yako kupitia link hii hapa:

Kuna mengi sana ya kujifunza hapo kwenye hio makala hapo.

Lakini licha ya yote hayo, mtaani mambo bado ni magumu kwa wakulima na wafanyabiashara wadogo, kwanini? Kwa sababu taarifa za miamala bado zimetekwa na madalali. Wao ndo wanazuia bidhaa zote pale mpaka na kuzivusha na kufanya biashara nje ya nchi.

Hali hio bado inawatengenezea faida kubwa sana madalali hao na kuwaacha kwenye mataa wakulima na wafanyabiashara wadogo ambao kimsingi ndo wenye mali halisi.

SASA NINI KIFANYIKE ILI KUWEZESHA MALIPO KWA URAHISI?

Wakiwa wanajiuliza serikali, jumuiya za kimataifa na mashirika ya ndani na nje ya nchi, Shirika la African Export-Import Bank (Afreximbank) wakaja na suluhu ambayo inakwenda kumtingisha bwana Dalali na kumtengenezea mazingira mazuri ya kufaidika ndugu Mkulima na mfanyabiashara mdogo. Suluhu hio ni Mfumo wa Kuwezesha Malipo barani Afrika waliouita PAPPS.

Mfumo huu wa PAPSS (Pan-African Payment and Settlement System) ulizinduliwa rasmi tarehe 13 January 2022 katika hafla iliyofanyika nchini Ghana. Kabla ya hapo, mfumo huo ulikua kwenye majaribio tangu mwaka jana 2021 huku ukiwa unatumika ndani ya nchi 6 za Afrika Magharibi. Mtandao wa ICLG unatujuza kwamba mfumo huu unakwenda kuokoa dola bilioni 5 kwa mwaka ambazo hupotea kama makato mbalimbali katika malipo ya kibiashara baina ya wafanyabiashara wa nchi moja na nyingine.

Pia imefahamika kwamba zaidi ya 80% ya miamala inayofanyika maeneo ya mipakani ambayo ilihitaji mifumo ya kimataifa ya kulipa na kubadili fedha, sasa inakwenda kuokolewa na mfumo huu. Imagine wakulima na wafanyabiashara tunavokwenda kunufaika hapa.

UNAJIUNGA VIPI NA MFUMO HUO WA KUWEZESHA MALIPO?

Mfanyabiashara, mteja, mshiriki na mamlaka za serikali ambaye anahitaji kunufaika na mfumo huu kwa sasa anahitajika kujisajili kupitia link hii http://papps.com/connect/ kisha fuata maelekezo.

Changamoto iliyopo ni kwamba mfumo huu bado haujasambaa vya kutosha kiasi cha kuzama katika matumizi ya kila siku ya kibiashara. Hali hio inawalazimu waandaaji kupambana katika kushirikiana na Taasisi za Fedha na Serikali za Mataifa ya Afrika ili kujenga msingi imara wa matumizi.

Mbeleni wafanyabiashara tutaweza kutuma na kupokea fedha ndani ya Jumuiya zetu za kikanda na bara zima kupitia Miundombinu hii ambayo inazidi kuboreshwa katika kutafuta fursa za biashara na maendeleo ya kiuchumi.

Kwa fursa za biashara zinavyofunguka kupitia #AfCFTA pamoja #Urasinishaji unaofanyika katika Jumuiya za Maendeleo (SADC, EAC, COMESA etc) ni wazi mfumo huu wa PAPPS unakwenda kuwezesha malipo yaweze kufanyika kwa haraka na ufanisi wa hali ya juu sana. Hapa hutakiwi kubaki nyuma kabisa ndugu yangu.

NITAIFAIDI VIPI SASA HIO PAPSS NIKIWA MJINI?

Kwanza fahamu mfumo huu ni wa Kimtandao, hivyo, ukiwa popote unaweza kufanya biashara na mteja hasa kupitia ecommerce website yako au Digital Tools zingine kama Instagram, Twita na Whatsapp.

Kufahamu zaidi gusa tweet yetu hii hapa chini

Uzuri wa kuwa na e-commerce website unakuja hapa. Mteja akiwa nchi X anaiona bidhaa kwenye website yako, alipia, kisha wewe mjasiriamali unafanya delivery kupitia Gari, Ndege au Meli na bidhaa inamfikia vema.

Kuna OFA hapa kwa ajili yako. Wasiliana nasi mara moja kuipata:

Umeshawahi kufanya biashara na wateja/wadau walio nje ya nchi yako lakini ndani ya Afrika? Ulipata changamoto gani? Na umejifunza nini? Tushirikishe uzoefu wako kwenye comments Kwa sababu kuna mdau angependa kufahamu kinachoendelea huko nje ya nchi kibiashara, right?

Mfumo huu wa PAPSS unakuja kuleta ushindani katika Kampuni na Mashirika yanayofanya biashara ya fedha kiteknolojia (Fintech) barani Afrika.

Ukiwa kama Mjasiriamali na mdau wa Tech, umejipangaje na ujio wa mfumo huu? Weka majibu na mawazo yako kwenye comments hapo chini.

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER)5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

MPESA LIPA NAMBA YETU
OFA YA KUPATA WEBSITE YAKO

OFA YA KUPATA WEBSITE YAKO LEO!

Tarehe 22 June, wakati natangaza maandalizi ya ujio wa OFA hii kupitia Whatsapp, alinijia rafiki yangu mmoja anaitwa Freddy. Yeye ni mfanyabiashara wa viatu pale magomeni. Akaniuliza, “Mimi huwa napost viatu vyangu kupitia whatsapp na Instagram, sasa hio website mimi itanisaidia vipi?”

Ikabidi nirudi kwenye makala mbili nilizowahi kupost kwenye tovuti yetu ya Rednet Technologies kupitia link https://rednet.co.tz/website-inasaidia-vipi-kuimarisha-biashara-yako/?noamp=mobile yenye kichwa “Website inasaidia vipi kuimarisha biashara yako?”
na link nyingine https://rednet.co.tz/kwanini-ni-muhimu-kuwa-na-websitetovuti-rasmi-ya-biashara-yako/ yenye kichwa “Kwanini umiliki tovuti (website) rasmi ya biashara yako?”

Kwa uchache nilimweleza haya:

  1. Website inakupa Utambulisho halali na kudumu mtandaoni. Yani website ndio ID muhimu ya biashara yako kama ilivyo ID yako ya NIDA.
  2. Website inawafikia watu wengi zaidi ambao wanaweza kuwa wateja wako kuliko whatsapp ama Instagram.

Kumbuka website ikiwa hewani inapatikana dunia nzima na wengi wataoifungua ni wanakuwa na interests na bidhaa/huduma yako.

Zaidi unaweza kutembelea tovuti yetu kupitia link zilizowekwa hapo juu ili kuzipata makala hizo na kuongeza maarifa.

Fast forward.. Sasa bwana Freddy nilipomueleza hayo akapata shauku sana ya kufungua tovuti yake, lakini bahati mbaya hakua na pesa ya kutosha kupata OFA hii, Hivyo nikaamua yafuatayo;

  1. OFA hii itawafikia wafanyabiashara watano TU kutoka watatu waliopangwa kufikiwa mwanzo.
  2. Muda wa kurequest OFA hii ni kwanzia leo Ijumaa mpaka Jumatatu asubuhi. Baada ya hapo hakutakuwa na OFA tena.
  3. Malipo ya kupata OFA hii yatakuwa katika mtindo wa 300k advance, na 200k italipwa kazi itakapokamilika.

OFA ITAKUPATIA HAYA:

  1. Website kamili ya biashara yako.
  2. Maintenance BURE mwaka mzima.
  3. Business Cards 50 BURE.
  4. Tutakufanyia SEO Bure mwaka mzima ili tovuti yako ipatikane Google mtu yeyote atakapokutafuta..

Kama una swali kuhusu chochote, Tafadhali niulize nami nitakuhudumia kama inavyostahili.

Whatsapp/call: 0765834754
Email: info@rednet.co.tz / fvitalice@gmail.com

thamani vs gharama, nafuu iko wapi? fahamu siri za kuweza kushawishi wateja katika biashara yako.

THAMANI vs GHARAMA, NAFUU IKO WAPI?

Ubora wa kazi una thamani kubwa sana kuliko gharama za kuifanya kazi hio. Unaweza lipia mradi kwa milioni 5, lakini usikupe matokeo yale ulijipangia mwanzoni. Pia unaweza lipa laki 5 ya mradi na ukapata matokeo mazuri zaidi. Ufanyeje? Je kati ya thamani vs gharama nafuu iko wapi? Fuatilia makala hii mpaka mwisho kufahamu zaidi.

Warren Buffet ambaye ni mbuji kabisa katika buruji la uwekezaji duniani amewahi kunukuliwa akisema “Price is what you pay, value is what you get.” akimaanisha, “Gharama ndio unayolipa, thamani ndio unayopata”. Kifupi ni kwamba thamani ndio msingi wa bidhaa/huduma huku gharama ikiwa ni makubaliano ambayo yanatangulizwa na muuzaji.

Kujua tofauti kati ya Gharama na Thamani ni moja kati ya mbinu bora zaidi za kufanya Uwekezaji. Zaidi kuhusu uwekezaji tayari tumeshakufahamisha SIRI ZA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA Ukishazifahamu hapo tuendelee..

Je kati ya thamani vs gharama, nafuu iko wapi?

umuhimu wa tehama

jinsi ya kufanikiwa katika biashara za mtandaoni

Unaposhindwa kutofautisha kati ya Gharama na Thamani kama mfanyabishara unajiweka kwenye mtego wa kukosa wateja, kutoaminika kwa Wawekezaji wakubwa, Kupoteza points dhidi ya washindani wako kibiashara na mwisho kuiweka biashara yako katika majanga ya kudhoofika na hatimaye kufa.

Unawezaje kupata bidhaa zinazouzwa kwa gharama za chini kuliko thamani yake halisi?

Jibu ni kufanya tathmini kwa kutumia viwango vya bei ambazo ni tofauti kabisa na gharama zinazotangazwa sasa. Hapa unaweza kuangalia bei, miaka 3 iliyopita ilikuaje na miaka 3 ijayo itakuwaje.

Bwana Phil Town, ameweka zoezi la kufanya Tathmini makini kwa kupitia hatua nne alizoziita “Four M’s“. Tuzione chap chap:

1. MEANING: Hatua ya kwanza kabla hujawekeza katika bidhaa/huduma fulani lazima ujiridhishe kuwa bidhaa/huduma hio ina maana sana kwako. Ikiwa na maana utapata fursa ya kuichunguza na kuielewa vyema, na kujituma ipasavyo katika kufanya biashara hio.

2. MOAT: (Upekee ambao hauwezi kuigwa na wengine): Unapochagua bishara ya kuwekeza ama bidhaa/huduma, unatakiwa uifanye iwe katika mtindo ambao washindani wako hawawezi kukuiga. Mfano: Duniani kuna makampuni mengi tu ya vinywaji laini (soft drinks) lakini Coca cola ni moja na itaendelea kubaki hivyo.

Hivyo hebu tuambie hapa biashara yako ina utofauti gani ambao washindani wako hawawezi kuiga kamwe?

3. MANAGEMENT: Je wajua kuwa Chanzo kikubwa kwa biashara kufa ni watu wanaoiendesha? Hivyo unapofikiria kuwekeza kwenye biashara lazima eneo ya utawala na uendeshaji wa shughuli linasimamiwa na watu wenye Weledi, Waaminifu na wanaojali maisha ya biashara hio.

4. MARGIN OF SAFETY: Kama umeshajiridhisha na hizo hatua 3 zilizopita, sasa hebu tizama pia namna unaweza kuweka mtaji ama kununua hisa bila kupoteza pesa na uhakika wa pesa yako kurudi.

Kila biashara inahitaji kitu fulani ambacho kitaitofautisha na washindani wake wengine sokoni. Sasa mchakato wa kutafuta tofauti hizo inaitwa “Positioning”. Hii mbinu inaziwezesha biashara kukazia sehemu fulani ya soko/wateja ili kujiimarisha zaidi kwenye sehemu hio. Unafanyaje?

MBINU ZA KUFANYA POSITIONING:

1. KUPUNGUZA GHARAMA: Ukifanya uchunguzi vizuri sokoni hasa kwenye mitaa ambayo wanafanya biashara ya aina moja mf: Kariakoo kila mtaa una shughuli yake maarufu zaidi kama mtaa wa livingstone ni maarufu kwa vyombo vya ndani.

So ukijigundua kuwa upo kwenye aina hii ya biashara, mbinu bora hapo ni kupunguza gharama za bidhaa zako kwa kiwango kidogo kuliko washindani wako. Lengo ni kuhakikisha unakuwa na mzunguko wa haraka wa mauzo ya bidhaa/huduma zako kwa faida ndogo ili mzigo wako uishe mapema.

Jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko la Mtandaoni

Je kati ya thamani vs gharama, nafuu iko wapi?

2. UBORA: Kama unataka kujitofautisha na washindani wako, basi mbinu bora na ya kuaminika ni kuhakikisha bidhaa/huduma zako ni za Ubora wa hali ya juu. Unapozingatia Ubora unajiweka kwenye nafasi ya kupata wateja wa kuaminika, wateja wa kudumu na wateja wa uhakika katika biashara.

3. MAKUNDI YA KIJAMII (DEMORGRAPHIC): Baadhi ya biashara huamua kujihusisha na makundi fulani tu ya kijamii ili kujiletea faida zaidi. Mfano: kwenye TV na redio vinatengenezwa vipindi mahsusi kwa Vijana, watu wa makamu na watu wa dini fulani kwa siku zao. Umeshawahi fanya hii?

Mbinu hii inafaa sana pale unapoyapata makundi hayo karibu na eneo lako la biashara au watu wanaokufuatilia zaidi mtandaoni wakawa ni wanamna hio. Vinginevyo unajiweka kwenye hatari ya kukosa soko kubwa nje ya hao uliolenga kuwahudumia.

4. HUDUMA BORA: Huwa inatokea kwa baadhi ya biashara ushindani unakuwa mkubwa sana kiasi kwamba mbinu 3 tulizoziona awali haziwezi kufanya kazi. Yani watu wanashikana kooni haswa. Hapa ndipo mbinu ya kutoa Huduma Bora kwa wateja inapokuja kuleta tofauti.

Zoezi la kutoa Huduma Bora ni pana na linahitaji ubunifu mwingi. Na hii inatoa fursa kwa biashara kubuni namna nzuri ya kuhudumia wateja wake ili kuhakikisha wateja wanafurahia bidhaa/huduma na kuzidisha mauzo. Mfano: unaweza kuanzisha dawati la wateja kutoa maoni live ili waweze kuona mawazo yao yakifanyiwa kazi. Unaweza kuanzisha kurasa za mitandao ya kijamii ili kukusanya kero za wateja na kuzifanyia kazi vizuri. Pia unaweza kutengeneza mzunguko kwa wateja wako kushiriki kama mabalozi wa kuitangaza biashara yako kwa watu wengine. Unaionaje hii?

UNAWEZA VIPI KUDADAVUA NA KUWASILISHA THAMANI YA BIASHARA YAKO KWA MTEJA WAKO?

Tafiti zinaonyesha kuwa watu hawapendi kabisa kutangaziwa ama kulazimishwa kununua kitu hasa huku mtandaoni. Mfano: Tizama unavyopata kero pale unapoangalia vidio YouTube mara katikat linakuja Tangazo Ama pale unataka kufungua ukurasa fulani mara unafunguka ukurasa wa tangazo kwanza kabla hujafika pale ulitaka kwenda. Hio kero ndio inatakiwa ikufanye uitazame biashara yako katika jicho la Kitaalamu kwa kutatua changamoto na si la Kibiashara kwa kuuza Bidhaa/huduma yako.

Unapotoa Elimu katika namna ya Utaalam wa kutatua changamoto fulani, unamfanya mteja atake kuondokana na kero zinazomsumbua kwa kutumia Bidhaa/Huduma zako. Hii ni tofauti kabisa pale unapotaka kuuza bidhaa. Ukifanya hivyo hutatui changamoto bali unakuwa kero kwa mteja.

Uongozi vs Utawala katika miradi/biashara, kipi kinafaa zaidi?

gharama vs thamani, kipi kinafaa zaidi?

Thamani ya Biashara yako inaonekana katika kutatua changamoto za mteja wako na Urahisi wa kutumia bidhaa/huduma yako. Hivyo lazima uhakikishe kuwa unachokitangaza ni Ile Namna na hisia ya Bidhaa zako zinaweza kutatua changamoto fulani ya mteja kwa urahisi.

Pia lazima uhakikishe suluhu yako inakwenda sambamba na hisia za mteja wako. Kwa kuwa kitaalam watu hununua bidhaa/huduma kutokana na hisia walizo nazo muda huo. Mfano kuna watu watakwambia kuwa wakiwa na hasira ama furaha sana kwao huo ndo muda wanafanya shopping kubwa zaidi.

Mzazi anapotaka kununua keki ya birthday ya mwanae hanunui tu keki tamu, lazima pia ahakikishe keki hio inakwenda kum-suprise mtoto kwa muonekano wake wa kuvutia. Ni mbinu ya kihisia hapo inatumika. Hivyo unapotaka kuongeza Thamani ya biashara yako unatakiwa kuzingatia hilo pia.

Umejifunza nini kwenye makala hii kuhusu thamani vs gharama, nafuu iko wapi? Tafadhali weka maoni au mtazamo wako katika sehemu ya comments hapo chini..

Vyanzo: https://www.forbes.com/sites/forbesfinancecouncil/2018/01/04/the-important-differences-between-price-and-value/?sh=133fd5c94237

https://www.weebly.com/inspiration/difference-between-value-and-cost/

https://yourbusiness.azcentral.com/different-types-strategies-business-1348.html

Je wajua kuwa bando lako ni Mtaji unawezaje kutumia Ujasusi katika biashara yako (Business Intelligence)?

JE WAJUA KUWA BANDO LAKO NI MTAJI?

Imagine una ofisi yako (eneo la biashara) na pia unayo akaunti yako ya twita, Instagram au facebook. Lakini hujui namna ya kutengeneza mvuto kwa watu ili wakutafute, wakufollow, wakuamini na wafanye biashara na wewe. Unafanyaje? Je wajua kuwa bando lako ni Mtaji tosha? Fuatilia makala hii mpaka mwisho kufahamu kiundani.

Imagine hujawahi kutengeneza mahusiano ya kibiashara na followers wako, hata mmoja yani, na kila siku upo mtandaoni kufuatilia habari mpya zinazojiri kwenye Bongo Fleva, Bongo Muvi, Mpira, Umbea, Siasa n.k. Kuna muda unatamani biashara yako iwe kubwa lakini hujui mbinu gani unaweza kutumia ili kuhakikisha biashara yako inazidi kuwa Imara kila siku. LEO hii Nazungumza na wewe hapa.

1. CHANGAMKA KIBIASHARA UWAPO MTANDAONI:

Kabla ya yote, fahamu kuwa biashara inafanyika vizuri katika mazingira yaliyojengwa kwa mahusiano imara, hivyo hebu tizama unahusiana vipi na watu waliokuzunguka na followers wako. Hili ni eneo pana ambapo unatakiwa ufahamu saikolojia ya watu wako hasa wateja na kujua namna ya kukabiliana nao positively. Maana mitandaoni kuna kila aina ya watu na tabia zao, kuna wenye kiburi, kuna wababe, wachechi, wajeuri, wanafunzi, wenye hekima, wapole, wenye lugha chafu na micharuko. Sasa jukumu lako ni kuwajua na kukabiliana nao bila kukwazana. Cha kufanya ni kuhakikisha unatumia vizuri bando lako tu hapa.

Mtandao saidizi jinsi ya kukabiliana na hasara kwenye biashara mbinu za kuwa tajiri

Humu mitandaoni wewe kama sio mtu maarufu basi hakikisha unakuwa mchangamfu kwa kadiri ya inavyowezekana. Kuwa “mchangamfu” haina maana uwe mwenye kiherehere, shobo au mtu wa kujipendekeza, lakini ujue namna kuchangia mijadala mbalimbali na kujihusanisha na watu vizuri.

2. JE WAJUA KUWA BANDO LAKO NI MTAJI WA KUJIJENGA KUWA MTAALAM?

Kwenye biashara hili ni eneo muhimu sana, yani sawasawa na uti wa mgongo. Watu wengi hudhani biashara ni kuuza na kununua tu, of course wako sawa. Hata hivyo ili biashara yako iweze kunawiri katika mazingira ya mtandaoni yaliyojaa ushindani wa kila aina, unapaswa kujua zaidi ya “kuuza na kununua”. Humu mtandaoni watu hukwepa sasa matangazo, hivyo “unapoweka tangazo lako hakikisha halionekani kama TANGAZO bali lionekane kama HABARI MPYA kwa yeyote anayesoma.”

Mtego ndo upo hapo. Lazima uwe mtaalam wa kuhudumia faida zinazotokana na bidhaa/huduma zako. Usiuze tu ukaishia hapo, hebu kuwa MLEZI wa mteja wako. Binafsi nina LIST ya wateja wangu ambapo huwa nawatumia updates mbalimbali kuhusu hali ya biashara na uchumi katika muktadha wa teknolojia BURE kabisa. Ungependa kuwa kwenye list hio? Nitumie ujumbe kwa WhatsApp sasa hivi kwa kugusa namba hii hapa 0765834754

3. JE WAJUA KUWA BANDO LAKO NI MTAJI WA KUFUNGUA WEBSITE:

Kwa kasi ambayo teknolojia inakwenda nayo nina uhakika usingependa kupitwa na fursa lukuki zinazokoja na mapinduzi haya ya 4 ya viwanda yanayoendelea duniani. Fikiria, Kusini mwa Jangwa la Sahara kunakadiriwa kuwa na watumiaji wa internet zaidi ya milioni 400. Nchini Tanzania kunaripotiwa kuwa na watumiaji wa internet zaidi ya milioni 29 mpaka kufikia mwaka 2022 Kwa mujibu wa ripoti ya TCRA.

jinsi ya kuanzisha website

Je wajua kuwa bando lako ni Mtaji

Sasa kwa kutumia hilo Bando lako la internet, unalitumiaje kuwafikishia watu hawa bidhaa/huduma yako? Website ni kifaa (Digital tool) muhimu na mahsusi kwa kuwafikia watu wengi ndani ya muda mchache sana. Kwenye website unao uwezo wa kutoa huduma za kushauri na mafunzo nakdhalika. Zaidi unaweza kujua faida za kuwa na website kupitia hapa WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?

Kuweza kupata website yako wasiliana nasi kupitia namba 0765834754 au email info@rednet.co.tz ili tukusaidia kutatua changamoto zinazokukabili. USIBAKI NYUMA.

4. JE WAJUA KUWA BANDO LAKO NI MTAJI WA KUWA MKWELI/AMINIKA UKIWA MTANDAONI:

Moja kati ya eneo ambalo linawapa changamoto wafanyabiashara wengi ni hili la kuwa mkweli na Muaminifu. Wateja wengi huwa wanakwazika sana wanapofanya kazi na wafanyabiashara ambao si wakweli/waaminifu. Hiki ni kitu kibaya sana na hata wewe usingependa kikutokee.

Uongozi vs Utawala katika miradi/biashara, kipi kinafaa zaidi? gharama vs thamani, kipi kinafaa zaidi?

Je wajua kuwa bando lako ni Mtaji

Unapojijenga kwa kuwa mkweli unatengeneza mazingira ya kuaminika ambayo yatakufanya upendwe na watu na wao waweze kufanya biashara na wewe bila wasiwasi. Hata wewe mfanyabiashsra, siku ukiwa mteja usingependa kukutana na mtoa huduma ambaye si mkweli/mwaminifu, si ndio?

Ni matumaini yangu umegundua kwamba Bando lako ni Mtaji muhimu sana katika uendeshaji wa biashara yako katika zama hizi za kidijitali? Lazima ujue namna nzuri ya kuendesha akaunti yako ya mtandao wa kijamii ili ilete tija kiuchumi katika biashara yako. Unahitaji mtu wa kuendesha akaunti yako? Wasiliana nasi mara moja.