Category: Business Updates

mbinu ya ufungani (commitment) katika biashara

JITAFUTE KWANZA ILI UFANIKIWE

Mwaka 2017 wakati tunaanzisha Rednet Technologies tulikua na vision kubwa sana, kama ile watoto wadogo wanavyoota kuwa Marubani na Wanasheria. Hata hivyo kuifanyia kazi vision hio haijawahi kuwa rahisi. Jasho, Damu na Machozi haviepukiki. Mwaka 2020 nikagundua kwamba unatakiwa u jitafute kwanza ili ufanikiwe.

Vision ya Rednet Technologies ilikuwa ni “Kuhakikisha Tunawafikia Wafanyabiashara wote wadogo na wale wa kati wanaofanya shughuli zao katika eneo la Afrika Mashariki na Kati, na kuimarisha Biashara zao kwa matumizi ya Teknolijia za kisasa kutoka kwetu”.

Hio Vision inahitaji Maarifa, Ujuzi, Muendelezo (Consistency), Ubunifu na zaidi, Teamwork. Kama wewe ni mfanyabiashara na una ndoto za kufanikiwa katika shughuli zako basi hili la Teamwork unapaswa kulitazama kwa macho matatu. Leo tutachambua kwa undani hapa kwenye TEAMWORK.

Ile Team yetu ya kwanza tulitamani ingeweza kufanikiwa kuifikisha Rednet pale inatakiwa kufika. Lakini haikuweza kufanya hivyo. Hivyo, mwezi March, 2018 kwa huzuni kubwa Rednet Technologies ilisitisha Operations zake kwa kipindi cha Mwaka mzima mpaka May 2019. Kilikua ni kipindi kigumu mno kwangu binafsi kwa sababu mimi ndiye nilikua Visionary Leader.

Nilitamani sana Rednet Ifanikiwe, roho yangu ilikua ikiniuma sana kuona juhudi zangu hazikuwa zikizaa matunda. Kila mbinu niliyokua naitumia haikunipa majibu ya kufurahisha. Nilikata tamaa kabisa. Hata hivyo hio 2019 tulipata kazi chache za kuwahudumia wateja wetu, lakini bado hatukuweza kutanua vizuri mtandao wa wateja wetu na kushirikiana nao kwenye shughuli zao vile inavyotakiwa.

Hali hii ilikwenda mpaka Octoba, 2020, kabla ya ule Uchaguzi Mkuu ndipo ambapo ndugu yangu wa zamani sana, JEOFFREY alinipa idea ya kimapinduzi sana.

JEOFFREY NI NANI?

Huyu Jeoffrey ni rafiki yangu wa zamani sana. Tulisoma wote shule ya msingi japo yeye alinizidi darasa moja. Na zaidi tuliishi wote mtaa mmoja kwa kipindi kirefu sana katika maisha yetu, zaidi ya miaka 18. Kipindi chote icho sikuwahi kujua kuwa mfumo wake wa biashara utanifaa.

Huyu jamaa ana biashara yake ya kusambaza vifaa vya miundombinu ya maji kama koki, elbows, mabomba n.k. Zaidi yeye amejisajili kwenye mfumo wa manunuzi ya serikali (TaNEPS). Huko anapata tenda nyingi sana kuhusu miradi ya maji ya serikali nchi nzima. Kifupi anafanya vizuri sana sokoni.

Hio siku sasa alinijia akihitaji nimtengenezee ecommerce website ili kusudi aweze kuuza bidhaa zake kwa rejareja kwa wateja wake walio nje ya mfumo wa manunuzi. Hivyo akanipatia nyaraka za wasifu wa kampuni (Company Profile) yake. Sasa wakati naifanya hio kazi yake nikawa najiuliza, hivi mimi nashindwaje kutanuka kama jamaa yangu hapa. Hapa kuna kitu muhimu sana, jitafute kwanza ili ufanikiwe.

Najua hata wewe unayesoma unajiuliza hili swali “NAWEZAJE KUTANUA BIASHARA YANGU?” Well, kupitia vikao vichache nilivyokaa na huyu jamaa yangu, nikaweza kugundua namna ambayo tunaweza kusambaza Bidhaa na Huduma zetu kwa watu wengi na kwa haraka zaidi.

Hivyo, tukaanzisha Huduma ya Kusambaza Vifaa vya Ofisini na Computer kama mafile, diaries , flash disks, antivirus na vitu vya stationery unavyovijua. Wateja wetu wakubwa tuloanza nao walikua ni makampuni na taasisi ambazo kimsingi wametupa ushirikiano mkubwa sana.

Tumekuwa tukipokea Oda kutoka sehemu mbalimbali na tumeweza kukuza mtandao wa wateja wetu haraka na kwa ufanisi mkubwa kupitia huduma hii. Jambo hili likatulazimu kwenda mbele zaidi ambapo sasa kupitia tovuti yetu ya https://rednet.co.tz unaweza ku-request oda na tukakufikia.

Urafiki wetu na Jeoffrey ukazidi kuota mizizi ambapo sasa tunashirikiana kwenye mambo mengi sana ya kikazi. #VijanaWenzangu mimi huwa nawaambia “Tutumiane vizuri katika shughuli zetu za kiuchumi. Delegate your tasks kwa kuwa baraka zipo kwenye KUTOA zaidi kuliko kwenye KUPOKEA“.

Mimi rafiki zangu nawapa michongo mingi sana, ya muda mrefu na ile ya muda mfupi. Kadhalika rafiki zangu wananipa michongo mingi sana, ya muda mrefu na ile ya muda mfupi. Wataalam wanakwambia “Your Network is Your Net worth“. Kuna maana kubwa sana kwenye huo msemo ukitafakari.

Kama connections ulizonazo hazikutumii vizuri sasa usilalamike, watumie wewe kwenye mishe zako. Yes, maana hai-make sense kuwajua watu wazuri wanaoweza kuipush biashara yako halafu huwatumii eti kwa kuwa wao hawakutumii kwenye mishe zao. How? Make sure you get upper hand on it.

KARIBU KATIKA HUDUMA MPYA:

Website yetu sasa tumeiweka ili kusudi kukupa wewe uwezo wa kuchagua huduma unayotaka kisha sisi tutapata request yako, tutakutumia Quotation ukiridhia tunakupatia huduma yako katika muda ambao utapanga wewe. Upewe nini zaidi?

Kwa vifaa vya Ofisini (stationeries) kama wino wa printa, flash disks, rim paper, peni (box) n.k gusa link hii https://rednet.co.tz/services/your-order/… Link hio itakupeleka direct kwenye ukurasa utakaokupa nafasi ya kutuambia huduma unayohitaji ukiwa popote Duniani.

Pia tumekuletea huduma mahsusi kwa ajili yako iitwayo “JIHUDUMIE” kupitia link hii https://rednet.co.tz/services/jihudumie-leo/… ambapo humo ndani utajipatia huduma kama zinavyoonekana kwenye picha hapa.

CHANGAMOTO:

1. KUWA RASMI: Najua watu wengi humu mitandaoni biashara zenu si rasmi, kwa maana ya kwamba hazijasajiliwa katika Mamlaka za Kiserikali (BRELA, TRA, HALMASHAURI, BENKI etc). Sasa mtindo huu wa Usambazaji unakutaka kusajili biashara yako kwa kuwa biashara/kampuni yako sasa inakwenda kufanya kazi na biashara/kampuni zingine (B2B). Matumizi ya Quotations, Proforma Invoice, Tax Invoices, EFD receipts na Delivery Notes kwenye mtindo huu wa Biashara ni kama Katiba katika utawala wa Nchi. Eneo hili kama Mjasiriamali unapaswa kuwalo makini sana yani.

Hivyo ifanye biashara/kampuni yako kuwa rasmi kwanza ili kujihakikishia unafanya shughuli zako bila kubughudhiwa na mtu yeyote.

2. UCHELEWESHWAJI WA MALIPO: Kuwa msambazaji/Supplier maana yake ni kwamba unafanya kazi kwa pesa yako na pesa hio utaingiziwa baada ya mwezi mmoja mpaka miezi sita. Hivyo, kukaa muda mrefu bila kuingiziwa pesa si kazi ndogo, uvumilivu lazima uchukue nafasi yake hapa.

3. MTAJI: Kama ulivyoona hizo changamoto zingine hapo juu, kufanya usambazaji lazima uwe na Mtaji wa kutosha kuweza kuhudumia Wateja wako kikamilifu kabla wao hawajakuingizia pesa siku za mbeleni. Hapa lazima uwe na pesa ya kufanya kazi mkononi ili usije ukatolewa katika game.

Hata hivyo, changamoto hizi hazitakiwi kukurudisha nyuma, katika harakati jitafute kwanza ili ufanikiwe lazima uhakikishe unapambana kwa njia zozote ili kusudi mafanikio yako yakapate kujidhihirisha. #VijanaWenzangu muda wa kupambania future zenu ndio sasa. Pambaneni haswa.

OFA YA MSIMU WA SABASABA

Mwaka 2016 wakati nawaza kufungua kampuni from scratch nilifikiri kupata wateja itakuwa rahisi tu. Nikawaza nikimaliza mchakato wa BRELA, TRA na Leseni basi nikituma proposals zangu kwa watu walau 10 ntakuwa nimeshapata wateja wangu nianze kuingiza pesa.

Sasa nilipoanza kutafuta wateja nikawa nashangaa, kila ninapoenda nasikilizwa tu lakini sitafutwi tufanye kazi. Mteja wangu wa kwanza nilikuja kumpata August, 2018 (mwaka mmoja baada ya kufungua kampuni rasmi mwaka 2017). Sikujua maisha yangekuwa magumu kiasi kile.

ILIKUAJE NIKAPATA MTEJA?

Kutokana na kushamiri kwa vitendo vya Utapeli wa mtandaoni, watu wamekuwa waoga sana katika kufanya biashara mtandaoni. Watu wanatapeliwa jamani, kuweni makini mno na miamala mnayofanya kwenye simu zenu pamoja na humu mtandaoni ndugu zangu.

Ilinichukua muda mrefu, almost miaka miwili mpaka nilipogundua MBINU ya kuchapisha makala zenye maudhui muhimu kwa biashara za wajasiriamali kupitia kurasa zangu za LinkedIn, Instagram na Twitter huku nikiziunga na link ya tovuti ya kampuni ambayo ndipo nilipoweka makala kamili.

Baada ya watu kutembelea kurasa zangu za mtandaoni na tovuti yangu na kuona “Thamani ya maudhui” niliyokua nayatoa ndipo nilipopata mteja wa kwanza wa uhakika ambaye mpaka leo bado tunaendelea kufanya kazi pamoja na wateja wengine wengi kutokea hapo.

NILICHOGUNDUA:

Mpaka mtu afanye kazi/biashara na wewe lazima:

1. Awe anakufahamu au tayari anazo taarifa zako za kutosha.

2. Anakuamini (kwamba utafanya kazi yake kwa viwango anavyotaka na pesa yake haiendi bure).

3. Anakupenda (ni ngumu kufanya biashara na mtu ambaye hampendani).

Jiulize hapo, Unaweza vipi kumshawishi mtu ambaye hakufahamu kabisa (a total stranger) akuamini na akupe kazi zake uwe unamfanyia kwa kiwango anachokitaka? Pitia makala hii hapa kwenye link https://rednet.co.tz/fahamu-siri-ya-kuweza-kushawishi-wateja-katika-biashara-yako/ yenye kichwa “FAHAMU SIRI YA KUWEZA KUSHAWISHI WATEJA KATIKA BIASHARA YAKO”

Nafahamu kuna muda unapitia wakati mgumu sana katika kutafuta wateja wapya katika biashara yako ili kujitanua zaidi, lakini hujui ufanyeje. Hata hivyo, MBINU BORA ya kutanua biashara yako kwa watu usiofahamiana nao kabisa, hasa watu wa mtandaoni (Digital Neighbors) ni hii hapa:

1. Badili matumizi ya Mitandao ya kijamii kwa kupost maudhui kuhusu Thamani ya bidhaa/huduma yako katika maisha ya mtu ili kumvutia awe mteja wako. Weka tips kama Aina za bidhaa/huduma, Bidhaa feki zinajulikana vipi, bidhaa zako zina utofauti gani na zingine, ubora uko vipi nakadhalika.

2. Fungua website ili kujiweka katika mazingira ya kujulikana kwa Utalaam wako mahsusi. Website ndio CV ya biashara yako mtandaoni. NOTE: Mteja atafanya kazi na wewe kiuhakika kwa kuwa wewe ni Mtaalam katika fani fulani na sio salesperson kama wengine pale akiona website yako.

3. Hakikisha mtu aki-search huduma/bidhaa unazouza kupitia google basi anakupata mara moja. Hii kitaalam inaitwa S.E.O (Search Engine Optimization). Hii inakupa fursa bora ya kutanua biashara yako hasa katika matafuto ya mtandaoni ambayo yatawasaidia wateja kukufikia kirahisi.

Sasa, kwa kufahamu hilo, Natoa OFA YA MSIMU WA SABASABA ambapo utakapofungua website yako kwenye msimu huu tutakufanyia SEO, tutakupa tips za kutoa maudhui ya kuvutia wateja kwenye mitandao yako ya kijamii pamoja na kukufanyia Web maintenance BURE kwa mwaka mzima.

Bei ya OFA hii ni laki tano tu (500,000/-) unapata vyote nilivyokutajia. OFA hii itakapokwisha gharama zitarejea kufikia laki tisa elfu hamsini tu (950,000/-) kwa website peke yake. Hivyo wahi kabla OFA haijakwisha. Karibu Tufanye kazi.

Kwa maswali au maulizo yoyote tafadhali tumia mawasiliano yetu yanayopatikana katika tovuti hii.

OFA YA KUPATA WEBSITE YAKO

OFA YA KUPATA WEBSITE YAKO LEO!

Tarehe 22 June, wakati natangaza maandalizi ya ujio wa OFA hii kupitia Whatsapp, alinijia rafiki yangu mmoja anaitwa Freddy. Yeye ni mfanyabiashara wa viatu pale magomeni. Akaniuliza, “Mimi huwa napost viatu vyangu kupitia whatsapp na Instagram, sasa hio website mimi itanisaidia vipi?”

Ikabidi nirudi kwenye makala mbili nilizowahi kupost kwenye tovuti yetu ya Rednet Technologies kupitia link https://rednet.co.tz/website-inasaidia-vipi-kuimarisha-biashara-yako/?noamp=mobile yenye kichwa “Website inasaidia vipi kuimarisha biashara yako?”
na link nyingine https://rednet.co.tz/kwanini-ni-muhimu-kuwa-na-websitetovuti-rasmi-ya-biashara-yako/ yenye kichwa “Kwanini umiliki tovuti (website) rasmi ya biashara yako?”

Kwa uchache nilimweleza haya:

  1. Website inakupa Utambulisho halali na kudumu mtandaoni. Yani website ndio ID muhimu ya biashara yako kama ilivyo ID yako ya NIDA.
  2. Website inawafikia watu wengi zaidi ambao wanaweza kuwa wateja wako kuliko whatsapp ama Instagram.

Kumbuka website ikiwa hewani inapatikana dunia nzima na wengi wataoifungua ni wanakuwa na interests na bidhaa/huduma yako.

Zaidi unaweza kutembelea tovuti yetu kupitia link zilizowekwa hapo juu ili kuzipata makala hizo na kuongeza maarifa.

Fast forward.. Sasa bwana Freddy nilipomueleza hayo akapata shauku sana ya kufungua tovuti yake, lakini bahati mbaya hakua na pesa ya kutosha kupata OFA hii, Hivyo nikaamua yafuatayo;

  1. OFA hii itawafikia wafanyabiashara watano TU kutoka watatu waliopangwa kufikiwa mwanzo.
  2. Muda wa kurequest OFA hii ni kwanzia leo Ijumaa mpaka Jumatatu asubuhi. Baada ya hapo hakutakuwa na OFA tena.
  3. Malipo ya kupata OFA hii yatakuwa katika mtindo wa 300k advance, na 200k italipwa kazi itakapokamilika.

OFA ITAKUPATIA HAYA:

  1. Website kamili ya biashara yako.
  2. Maintenance BURE mwaka mzima.
  3. Business Cards 50 BURE.
  4. Tutakufanyia SEO Bure mwaka mzima ili tovuti yako ipatikane Google mtu yeyote atakapokutafuta..

Kama una swali kuhusu chochote, Tafadhali niulize nami nitakuhudumia kama inavyostahili.

Whatsapp/call: 0765834754
Email: info@rednet.co.tz / fvitalice@gmail.com

thamani vs gharama, nafuu iko wapi? fahamu siri za kuweza kushawishi wateja katika biashara yako.

THAMANI vs GHARAMA, NAFUU IKO WAPI?

Ubora wa kazi una thamani kubwa sana kuliko gharama za kuifanya kazi hio. Unaweza lipia mradi kwa milioni 5, lakini usikupe matokeo yale ulijipangia mwanzoni. Pia unaweza lipa laki 5 ya mradi na ukapata matokeo mazuri zaidi. Ufanyeje? Je kati ya thamani vs gharama nafuu iko wapi? Fuatilia makala hii mpaka mwisho kufahamu zaidi.

Warren Buffet ambaye ni mbuji kabisa katika buruji la uwekezaji duniani amewahi kunukuliwa akisema “Price is what you pay, value is what you get.” akimaanisha, “Gharama ndio unayolipa, thamani ndio unayopata”. Kifupi ni kwamba thamani ndio msingi wa bidhaa/huduma huku gharama ikiwa ni makubaliano ambayo yanatangulizwa na muuzaji.

Kujua tofauti kati ya Gharama na Thamani ni moja kati ya mbinu bora zaidi za kufanya Uwekezaji. Zaidi kuhusu uwekezaji tayari tumeshakufahamisha SIRI ZA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA Ukishazifahamu hapo tuendelee..

Je kati ya thamani vs gharama, nafuu iko wapi?

umuhimu wa tehama

jinsi ya kufanikiwa katika biashara za mtandaoni

Unaposhindwa kutofautisha kati ya Gharama na Thamani kama mfanyabishara unajiweka kwenye mtego wa kukosa wateja, kutoaminika kwa Wawekezaji wakubwa, Kupoteza points dhidi ya washindani wako kibiashara na mwisho kuiweka biashara yako katika majanga ya kudhoofika na hatimaye kufa.

Unawezaje kupata bidhaa zinazouzwa kwa gharama za chini kuliko thamani yake halisi?

Jibu ni kufanya tathmini kwa kutumia viwango vya bei ambazo ni tofauti kabisa na gharama zinazotangazwa sasa. Hapa unaweza kuangalia bei, miaka 3 iliyopita ilikuaje na miaka 3 ijayo itakuwaje.

Bwana Phil Town, ameweka zoezi la kufanya Tathmini makini kwa kupitia hatua nne alizoziita “Four M’s“. Tuzione chap chap:

1. MEANING: Hatua ya kwanza kabla hujawekeza katika bidhaa/huduma fulani lazima ujiridhishe kuwa bidhaa/huduma hio ina maana sana kwako. Ikiwa na maana utapata fursa ya kuichunguza na kuielewa vyema, na kujituma ipasavyo katika kufanya biashara hio.

2. MOAT: (Upekee ambao hauwezi kuigwa na wengine): Unapochagua bishara ya kuwekeza ama bidhaa/huduma, unatakiwa uifanye iwe katika mtindo ambao washindani wako hawawezi kukuiga. Mfano: Duniani kuna makampuni mengi tu ya vinywaji laini (soft drinks) lakini Coca cola ni moja na itaendelea kubaki hivyo.

Hivyo hebu tuambie hapa biashara yako ina utofauti gani ambao washindani wako hawawezi kuiga kamwe?

3. MANAGEMENT: Je wajua kuwa Chanzo kikubwa kwa biashara kufa ni watu wanaoiendesha? Hivyo unapofikiria kuwekeza kwenye biashara lazima eneo ya utawala na uendeshaji wa shughuli linasimamiwa na watu wenye Weledi, Waaminifu na wanaojali maisha ya biashara hio.

4. MARGIN OF SAFETY: Kama umeshajiridhisha na hizo hatua 3 zilizopita, sasa hebu tizama pia namna unaweza kuweka mtaji ama kununua hisa bila kupoteza pesa na uhakika wa pesa yako kurudi.

Kila biashara inahitaji kitu fulani ambacho kitaitofautisha na washindani wake wengine sokoni. Sasa mchakato wa kutafuta tofauti hizo inaitwa “Positioning”. Hii mbinu inaziwezesha biashara kukazia sehemu fulani ya soko/wateja ili kujiimarisha zaidi kwenye sehemu hio. Unafanyaje?

MBINU ZA KUFANYA POSITIONING:

1. KUPUNGUZA GHARAMA: Ukifanya uchunguzi vizuri sokoni hasa kwenye mitaa ambayo wanafanya biashara ya aina moja mf: Kariakoo kila mtaa una shughuli yake maarufu zaidi kama mtaa wa livingstone ni maarufu kwa vyombo vya ndani.

So ukijigundua kuwa upo kwenye aina hii ya biashara, mbinu bora hapo ni kupunguza gharama za bidhaa zako kwa kiwango kidogo kuliko washindani wako. Lengo ni kuhakikisha unakuwa na mzunguko wa haraka wa mauzo ya bidhaa/huduma zako kwa faida ndogo ili mzigo wako uishe mapema.

Jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko la Mtandaoni

Je kati ya thamani vs gharama, nafuu iko wapi?

2. UBORA: Kama unataka kujitofautisha na washindani wako, basi mbinu bora na ya kuaminika ni kuhakikisha bidhaa/huduma zako ni za Ubora wa hali ya juu. Unapozingatia Ubora unajiweka kwenye nafasi ya kupata wateja wa kuaminika, wateja wa kudumu na wateja wa uhakika katika biashara.

3. MAKUNDI YA KIJAMII (DEMORGRAPHIC): Baadhi ya biashara huamua kujihusisha na makundi fulani tu ya kijamii ili kujiletea faida zaidi. Mfano: kwenye TV na redio vinatengenezwa vipindi mahsusi kwa Vijana, watu wa makamu na watu wa dini fulani kwa siku zao. Umeshawahi fanya hii?

Mbinu hii inafaa sana pale unapoyapata makundi hayo karibu na eneo lako la biashara au watu wanaokufuatilia zaidi mtandaoni wakawa ni wanamna hio. Vinginevyo unajiweka kwenye hatari ya kukosa soko kubwa nje ya hao uliolenga kuwahudumia.

4. HUDUMA BORA: Huwa inatokea kwa baadhi ya biashara ushindani unakuwa mkubwa sana kiasi kwamba mbinu 3 tulizoziona awali haziwezi kufanya kazi. Yani watu wanashikana kooni haswa. Hapa ndipo mbinu ya kutoa Huduma Bora kwa wateja inapokuja kuleta tofauti.

Zoezi la kutoa Huduma Bora ni pana na linahitaji ubunifu mwingi. Na hii inatoa fursa kwa biashara kubuni namna nzuri ya kuhudumia wateja wake ili kuhakikisha wateja wanafurahia bidhaa/huduma na kuzidisha mauzo. Mfano: unaweza kuanzisha dawati la wateja kutoa maoni live ili waweze kuona mawazo yao yakifanyiwa kazi. Unaweza kuanzisha kurasa za mitandao ya kijamii ili kukusanya kero za wateja na kuzifanyia kazi vizuri. Pia unaweza kutengeneza mzunguko kwa wateja wako kushiriki kama mabalozi wa kuitangaza biashara yako kwa watu wengine. Unaionaje hii?

UNAWEZA VIPI KUDADAVUA NA KUWASILISHA THAMANI YA BIASHARA YAKO KWA MTEJA WAKO?

Tafiti zinaonyesha kuwa watu hawapendi kabisa kutangaziwa ama kulazimishwa kununua kitu hasa huku mtandaoni. Mfano: Tizama unavyopata kero pale unapoangalia vidio YouTube mara katikat linakuja Tangazo Ama pale unataka kufungua ukurasa fulani mara unafunguka ukurasa wa tangazo kwanza kabla hujafika pale ulitaka kwenda. Hio kero ndio inatakiwa ikufanye uitazame biashara yako katika jicho la Kitaalamu kwa kutatua changamoto na si la Kibiashara kwa kuuza Bidhaa/huduma yako.

Unapotoa Elimu katika namna ya Utaalam wa kutatua changamoto fulani, unamfanya mteja atake kuondokana na kero zinazomsumbua kwa kutumia Bidhaa/Huduma zako. Hii ni tofauti kabisa pale unapotaka kuuza bidhaa. Ukifanya hivyo hutatui changamoto bali unakuwa kero kwa mteja.

Uongozi vs Utawala katika miradi/biashara, kipi kinafaa zaidi?

gharama vs thamani, kipi kinafaa zaidi?

Thamani ya Biashara yako inaonekana katika kutatua changamoto za mteja wako na Urahisi wa kutumia bidhaa/huduma yako. Hivyo lazima uhakikishe kuwa unachokitangaza ni Ile Namna na hisia ya Bidhaa zako zinaweza kutatua changamoto fulani ya mteja kwa urahisi.

Pia lazima uhakikishe suluhu yako inakwenda sambamba na hisia za mteja wako. Kwa kuwa kitaalam watu hununua bidhaa/huduma kutokana na hisia walizo nazo muda huo. Mfano kuna watu watakwambia kuwa wakiwa na hasira ama furaha sana kwao huo ndo muda wanafanya shopping kubwa zaidi.

Mzazi anapotaka kununua keki ya birthday ya mwanae hanunui tu keki tamu, lazima pia ahakikishe keki hio inakwenda kum-suprise mtoto kwa muonekano wake wa kuvutia. Ni mbinu ya kihisia hapo inatumika. Hivyo unapotaka kuongeza Thamani ya biashara yako unatakiwa kuzingatia hilo pia.

Umejifunza nini kwenye makala hii kuhusu thamani vs gharama, nafuu iko wapi? Tafadhali weka maoni au mtazamo wako katika sehemu ya comments hapo chini..

Vyanzo: https://www.forbes.com/sites/forbesfinancecouncil/2018/01/04/the-important-differences-between-price-and-value/?sh=133fd5c94237

https://www.weebly.com/inspiration/difference-between-value-and-cost/

https://yourbusiness.azcentral.com/different-types-strategies-business-1348.html

thamani vs gharama, nafuu iko wapi? fahamu siri za kuweza kushawishi wateja katika biashara yako.

FAHAMU SIRI YA KUWEZA KUSHAWISHI WATEJA KATIKA BIASHARA YAKO

Umeshajiuliza, mtu mmoja anaweza vipi kuweka kitu mtandaoni akapata wateja wengi sana au kuzua mjadala kubwa sana, lakini wewe kila ukijaribu kuweka bidhaa/huduma zako bado hupati muitikio unaotakiwa? Nini huwa kinafanyika? Leo sasa fahamu siri ya kuweza kushawishi wateja katika biashara yako. Uko tayari?

Kuwa na mafanikio katika biashara kuna maana kwamba Mfanyabiashara ambaye ndiye mhusika mkuu ameweza kushawishi wateja kuweza kununua bidhaa/huduma zake kwa wingi. Hivyo mfanyabiashara lazima awe na maarifa/skills za kutosha ili kuweza kushawishi na kuuza kwa mafanikio.

MAARIFA HAYO NI YEPI?

Iwe ni kwenye mitandao ya kijamii, serikalini au mtaani, ili kuweza kuwa na ushawishi popote pale alipo mfanyabiashara, basi hana budi kuhitimu mafunzo katika nyanja ya kushawishi na kuuza (copywriting and closing skills). Mafunzo hayo si lazima uyapate darasani, leo hii utayapata hapa, soma makala hii mpaka mwisho tu:

1. MBINU YA MUITIKIO (RECIPROCITY): Kisaikolojia binadamu hujihisi kuwa na umuhimu pale anapouliza jambo fulani na kupata majibu ya kupendeza. Majibu mazuri humfanya mteja kuhitaji kuuliza/kuchimba zaidi ili aweze kupata hitaji lake ambalo mwishoni huangukia kwenye kununua. Unachotakiwa kukifanya hapa kama mfanyabiashara ni KUMSAIDIA mteja wako KUNUNUA na sio KUMUUZIA tu ilimradi upate pesa. Ukiuza tu unakuwa huna tofauti na wauzaji wengine unaowaona huko barabarani. Wewe unataka kuwa tofauti nao, si ndio?

Mfano: Kwenye mtandao wa twitter kuna watu wanaojiita “mabroo” (wale wenye followers wengi) ambao watumiaji wengi wa kawaida huwalalamikia kwa kushindwa kushiriki kwenye midahalo ya watu wengine isipokuwa wao wenyewe kwa wenyewe.

Sasa ukiwa mfanyabiashara hasa wa mtandaoni, sio lazima uwe na followers wengi ndo uwe na mafanikio, cha msingi ni kuwa na uwezo wa kumjengea mteja aitikie kile unakitoa kwake, na muitikio huo huanzia kwako kwa kujihusanisha nao kwenye mijadala na changamoto wanazokushirikisha kila mara. Hii ni kwasababu silaha kubwa unayoweza kuitumia kunasa wateja wengi zaidi ni kutengeneza MAHUSIANO mazuri na wateja wako. Hapo ndipo unapo fahamu siri ya kuweza kushawishi wateja katika biashara yako sasa.

mbinu ya muitikio katika biashara (reciprocity)
fahamu siri ya kuweza kushawishi wateja katika biashara yako

2. UFUNGANI (Commitment): Mara nyingi mtu akishajifunga kwenye jambo fulani, hubaki hapo akichuma anachokitaka. Sasa lazima uhakikishe biashara yako inakuwa kama Mgodi kwa wateja wako kuendelea kufaidi madini ambayo yamo kwenye biashara. Kwamba, lazima biashara yako itengeneze sumaku ya aina yake ili kuweza kushawishi na kunasa wateja wengi kila siku. Hizi ni zile Mbinu za kuweza kulifikia soko kubwa zaidi mtandaoni. Mfano wa sumaku muhimu ni TAARIFA, yaani ikiwa unauza viazi, basi wape wateja wako taarifa nyingi kuhusu viazi, kama unauza spare za magari waelimishe kuhusu spares mbalimbali za magari, kadhalika kwenye biashara zingine. Hii inapasawa kuwa inafanyika mara kwa mara, tena inaleta tija zaidi ikiwa itakuwa inatolewa BURE.

mbinu ya ufungani (commitment) katika biashara

Yaani hakikisha taarifa kuhusu unachouza au kuhudumu hazikauki kwa wateja wako. Kwa njia hii ndipo unapoweza kutengeneza sumaku ya kushawishi wateja wengi zaidi kujifunga katika biashara yako na kukuletea mafanikio unayoyaota. Na njia bora ya kutoa taarifa ni kupitia Website. Biashara yako ina website? Kama unayo hakikisha unaitumia vyema kwa ukuaji imara wa biashara yako. Zaidi unaweza kujua namna ya kutumia website kikamilifu kupitia hapa WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?.

3. KUWA NA MAMLAKA: Hii ni siri muhimu sana. Watu hufuata na kusikiliza ushauri kutoka kwa mbobevu/mtaalam katika jambo fulani kuliko mtu yeyote tu asiyefahamika kwa utaalam fulani. Yaani ili uwe mtaalam lazima usome sana, uwe na uelewa mpana juu ya jambo fulani na uwe na confidence katika uwasilishaji wako ambayo itakupa mamlaka ya kutengenezea ushawishi unaotakiwa.

Hivyo, unapoongelea kuhusu bidhaa/huduma zako, ongea kama Mtaalam na sio muuzaji. Ukiongea kama mtaalam kwanza utajiamini zaidi, halafu zaidi utakuwa na mamlaka katika uwasilishaji wako jambo ambalo linavuta watu wengi kufanya biashara na wewe. Jaribu hii utanipa majibu yake.

4. UFANANO: Katika mbinu kongwe zaidi ambayo imetumika kutengeneza ushawishi duniani ni hii. Hata kwa waamini wa dini ya Kikristu mfano, imeandikwa “Neno wa Mungu akatwaa mwili, akakaa kwetu, nasi tukauona utukufu wake“. Yani Neno wa Mungu akajitwalia mwili ili afanane na watu ili lile kusudio lake la kuwaokomboa watu likapate kutimia.

Hali kadhalika katika biashara yako, lazima uhakikishe unatengeneza ufanano kati ya biashara yako, wewe mwenyewe pamoja na wateja wako. Hii hufanyika ili mteja ajiamini na kujihisi huru anapokujia ili aweze kutimiza hitaji lake.

mbinu ya ufanano katika biashara. Unafanana vipi na mteja wako?
fahamu siri ya kuweza kushawishi wateja katika biashara yako

Kumbuka biashara sio sehemu pa kujimwambafai kama wafanyavyo baadhi ya watu wa mitandaoni. Biashara ni watu, na watu lazima ujumuike na ufanane nao katika midahalo yao ya mara kwa mara ili kusudi waweze kukwambia mahitaji yao ambayo wewe ndiye mwenye dhamana ya kuyatimiza.

5. UADIMU (SCARCITY): Mara nyingi watu hupenda kumiliki vitu ambavyo wanavyovipenda na hawana. Mifano ipo mingi tu huko mtaani, jazia hapo. Unapouza bidhaa/kutoa huduma adimu/ambayo itakwenda kuisha baada ya muda fulani, watu hufanya haraka kununua ili wasije wakaikosa pindi itapopotea. Hivyo unapaswa kuzifanya bidhaa/huduma zako kuwa katika kiwango fulani cha uadimu ili kusudi umtengenezee mteja wako kiu ya kutaka kununua haraka iwekanavyo.

6. MKUMBO (BANDWAGON): Nadhani umeshawahi kuona hii. Hutokea pale bidhaa/huduma fulani inapotumiwa sana na watu fulani ambapo husababisha watu wengine kuitumia huduma hio. Mbinu hii imekuwa ikitumiwa sana na makampuni makubwa kwa kuwatumia wasanii/watu wenye ushawishi kwenye jamii ili wawe mabalozi na kutengeneza hali ya “mkumbo” ambao utasaidia bidhaa/huduma yao ikapate kutumika kwa wingi zaidi katika jamii. Kitaalamu mbinu hii hufanya kazi sana kuanzia maeneo ya Uswazi. Kama ulikua hufahamu, yaani fasheni zote kali za mjini huwa zinaanzia uswazi, mitindo ya kusuka, vyakula vizuri vipo huko, misemo, bidhaa nakadhalika.

Aina hii ya ushawishi si wafanyabiashara wote wanaiweza kuifanya na wala si dhambi ila ukiiweza ni moja ya mbinu bora kabisa katika kuhakikisha biashara yako inakuwa na ushawishi wenye tija kwa wateja wako. Unaweza kutengeneza mkumbo ili upate kutengeneza ushawishi wenye tija? Hebu tuone majibu yako..

SASA KWANINI MTEJA AKUCHAGUE WEWE?

Sio siri tena kuwa hisia ni silaha muhimu sana katika kujenga ushawishi katika biashara yako. Lazima uhakikishe unazijua vyema hisia za wateja wako na kuzitendea haki ipasavyo. Ufanyaje sasa ili kutibu hisia za wateja wako? Hakikisha una fahamu siri ya kuweza kushawishi wateja katika biashara yako hizi hapa.

1. WAFANYE WAJIHISI WAKIPEKEE: Kiafrika, mgeni anapokuja kwako hata kama kuna vita humo nyumbani, basi ni muda wa kuzika tofauti zote ili kuhakikisha mgeni anakirimiwa inavyotakiwa. Hii hufanyika ili mgeni huyo ajisikie vizuri na kwenda kutangaza yale mema aliyoyapata kwako.

Kunazo mbinu nyingi za kumfanya mteja akajihisi wa kipekee. Mfano kutabasamu na kusalimiana vizuri na watu kabla ya kwenda direct kwenye mambo ya kuuziana. Lengo ni kuendeleza ukarimu na hali ya urafiki makini katika kuhudumia mteja wako mara zote. Jambo hili ndilo huvutia zaidi.

unawezaje kupata wateja mtandaoni?
fahamu siri ya kuweza kushawishi wateja katika biashara yako

2. MSHIRIKISHE MTEJA KWENYE MAAMUZI: Moja kati ya vitu vinavyoweza kumfanya mtu yeyote awe mteja wako ni kitendo cha kumshirikisha katika maamuzi hasa yale yanayohusu namna ya kumhudumia kwa viwango. Washirikishe kwa njia ya kushikana mikono, bega au simu zenu za mikononi. Maamuzi ni muhimu sana na yanaathiri mwenenedo wa biashara kwa kiasi kikubwa sana. Hakikisha muda wote unafanya maamuzi sahihi. Unawezaje kufanya hivyo? Fuatana na mada hii hapa chini;

Jambo hili hutengeneza hali ya umiliki wa huduma/bidhaa kwa mteja hata kabla manunuzi hayajafanyika, kitu ambacho huchangia kiasi kikubwa mteja kuchagua kufanya biashara nawewe. Unaweza kucomment “viatu hivi unavyoviona vinakwenda sambamba na hio suruali yako, unaonaje ukakichukua hiki?” inachagiza sana mauzo mbinu hii.

mteja mshirikishe kwenye maamuzi. Msaidie aweze kununua huduma au bidhaa yako.
fahamu siri ya kuweza kushawishi wateja katika biashara yako

3. SIMULIA STORI: Mteja angependa kufahamu vitu kama, uliweza vipi kuanzisha hio biashara unayoifanya? Ulianzia wapi? Lini? Mteja wako wa kwanza ulimpata vipi? Umepitia changamoto zipi mpaka sasa na changamoto gani huwezi kuisahau? Stori yako inashawishi kwa kiasi kikubwa sana. Unatakiwa ujifunze namna nzuri ya kusimulia stori ili kuvutia wateja wengi zaidi. Stori hizo unaweza kuwa unazisimulia mara kwa mara kupitia akaunti zako za mitandao ya kijamii.

Kwenye hili mitandao ya kijamii ina nguvu ya ajabu sana. Unaweza vipi kuipata na kuitumia nguvu hio? Fuatana na makala hii hapa mpaka mwisho;

4. TOA AHADI ZA UKWELI: Unapomhudumia mteja ni vema ukamhudumia katika misingi ya uwazi na ukweli katika utoaji huduma zako au bidhaa. Kama kuna kasoro yoyote ni heri ukaiainisha mapema kwa mteja ili ajue namna ya kukabiliana na bidhaa/huduma hio. Haipendezi kutokuwa mkweli.

5. TOA HUDUMA KWA VIWANGO VYA JUU: Siku zote huduma bora huenda sambamba na Heshima kwa mteja, kuzingatia muda na kufuatilia kazi. Wasiliana na mteja wako mara kwa mara ili kujua muda wa kumpatia huduma. Cha msingi ni kutoa taarifa muda wowote inapotakiwa kufanya hivyo.

Hizi ndio siri za kushawishi wateja katika biashara yako wazidi kumiminika kila siku. Hakuna miujiza dunia ya leo. Hata hivyo si lazima utumie mbinu zote ulizozipata leo kwenye biashara yako. Unaweza kutumia mbinu moja au mbili au kadhaa ambazo kwa upande wako utaona zinakufaa zaidi. Ukiwa na swali, ushuhuda au changamoto tafadhali share nasi kupitia comments hapo chini nasi kwa pamoja tutajadili ili kuzitatua. Karibu sana Rednet Technologies.

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

mrahisishie mteja wako huduma za kifedha. Dunia ya leo si ya jana.