Mfumo wa mawasiliano ya simu (mobile ecosystem) huchangia shemu muhimu sana katika uchumi wa nchi zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara? Uchumi wa nchi hizo kwa pamoja umefikia thamani ya dola za kimarekani bilioni 110 ($110 b) ambayo ni sawa na 7.1% ya pato la taifa (GDP) katika mwaka 2017. Hii inajumuisha faida za moja kwa moja za mfumo huo, faida zisizo za moja kwa moja (indirect impact) pamoja na ukuaji wa uzalishaji unaoletwa na matumizi ya huduma za simu na teknolojia.
Tukigusia faida za moja kwa moja za mfumo huu wa mawasiliano ambao unajumuisha makampuni ya simu, watengenezaji wa huduma za miundombinu ya kiteknolojia, wasambazaji wa huduma/ bidhaa za simu, wafanyabiashara wa reja reja, watengenezaji wa simu na vifaa vyake pamoja na watengenezaji wa maudhui/applications/huduma za mtandaoni; mchango wao katika uchumi hukadiriwa kwa kupimwa thamani wanayochangia katika uchumi wa nchi husika ambayo hujumuisha bima ya wafanyakazi, faida ya ziada ya biashara pamoja na kodi.
Mwaka 2017, thamani iliyozalishwa na mfumo huu wa mawasiliano katika ukanda huu wa kusini mwa jangwa la Sahara ulikuwa dola bilioni 40 ambayo ni sawa na 2.5% ya pato la Taifa (GDP) ambapo makampuni ya simu peke yake yalijumuisha takribani 75% ya mchango huu.
Ukiachana na faida za moja kwa moja, zipo pia faida ambazo si za moja kwa moja (indirect impact) ambapo sekta hii hununua vifaa/huduma mbali mbali kutoka sekta nyingine. Kwa mfano makampuni ya simu hulazimika kununua umeme kutoka sekta ya nishati hali kadhalika wasambazaji na wafanya biashara wa reja reja wa vifaa/huduma za simu huhitaji usafiri kuwafikia wateja wao.
Kwa pamoja uzalishaji huu wa faida isiyo ya moja kwa moja ulitengeneza takribani 60$ mwaka 2017 (ambayo ni takribani 4% ya pato la taifa). Kiujumla ukiongezea na faida za moja kwa moja, sekta hii ya mawasiliano ya simu ilitengeneza 110$ bilioni sawa na 7.1% ya pato la taifa katika ukanda huu.
Hii inaleta picha gani Kibiashara?
Matumizi ya teknolojia ya simu pamoja na maendeleo ya simu za rununu (smartphones) huendesha uchumi kwa kuboresha uzalishaji, kupunguza costs za uendeshaji pamoja na kurahishisha upatikanaji wa huduma/bidhaa za kibinadamu.
Chanzo: Ripoti ya shirika la mawasiliano ya simu duniani la GSMA toleo la mwaka 2019.
Pia unaweza kupitia makala hizi hapa chini ambazo zinarandana na somo ulilolipata kwenye makala ya leo. Zitakusaidia sana ukimaliza kuzisoma zote.
Kwa watumiaji wengi wa simu za mkononi waishio Kusini mwa jangwa la Sahara, simu ya mkononi si kwamba ni kifaa cha mawasiliano tu, lakini zaidi ni kifaa muhimu cha kuperuzi mtandaoni na kupata huduma mbalimbali za msingi za kibinadamu. Ujio wa simu za rununu (Smartphones) eneo hilo umekuwa maradufu katika miaka ya hivi karibuni. Watumiaji wa simu za rununu wameongezeka kutoka 25% mwanzoni mwa muongo huu (2010’s) mpaka kufikia 44% mwishoni mwa mwaka 2017. Hii ni chini ya wastani wa kidunia wa 66% katika ongezeko hilo la watumiaji wa simu za mkononi. Hii ni kwa mujibu wa utafiti wa shirika la kimataifa la mfumo wa mawasiliano ya simu GSMA.
Watumiaji hao wa simu ambao ni 44% ya jumla watu waishio katika eneo hilo sawa na watu milioni 444 ambao pia ni aslimia 9% tu ya watumiaji wote wa simu za mkononi duniani wanatajwa kupatikana katika eneo hilo la kusini mwa jangwa la Sahara.
Pia inatajwa kwamba ongezeko hilo la watumiaji litakuwa katika kiwango cha CAGR (Compound Annual Growth Rate) kwa 4.8 katika kipindi cha mwaka 2017 hadi 2022, ambacho ni zaidi ya mara mbili ya CAGR ya dunia nzima katika kipindi hicho hicho.
Moja ya vitu vinavyotoa nguvu katika ongezeko hili ni pamoja na uwezo wa simu za rununu (janja) kuunganisha watu wengi kupitia huduma za intaneti na mitandao ya kijamii ambapo katika mitandao hio ndipo panapotumiwa na watu wengi kama sehemu ya kukutana, kubadilishana mawazo, kuburudika na kufanya biashara. Hivyo kufanya mitandao hio ya kijamii kuzidi kuwa na umuhimu kadiri muda unavyokwenda.
Kibiashara hii ina maana gani?
Ripoti hio ya GSMA iliyochapishwa mwaka 2018 inataja kwamba ukuaji wa teknolojia umerahisisha mambo mengi muhimu yakiwemo utolewaji wa elimu, maswala ya afya na tiba na pia kuwezesha mazingira bora ya kufanyika biashara katika kutunza na kuonyesha kumbukumbu mbalimbali, miamala ya kifedha na jinsi bora ya kumhudumia mteja hata akiwa mbali na mzalishaji kupitia majukwaa ya huduma za kifedha za kimtandao na IoT (Internet of Things). Ripoti hio pia inaakisi kasi ya ukuaji wa matumizi ya simu za rununu (samrtphones) pamoja na vifaa vya kiteknolojia mpaka kufikia mwaka 2025 katika utendaji na utoaji wa huduma mbalimbali za kibinadamu pamoja na shughuli za kibiashara katika ukanda wa kusini mwa jangwa la Sahara.
Pia unaweza kupitia makala hizi hapa chini ambazo zinarandana na somo ulilolipata kwenye makala ya leo. Zitakusaidia sana ukimaliza kuzisoma zote.
Bila kujali unafanya biashara ya aina gani, teknolojia ya intaneti na kompyuta imekuwa kwa kiwango kikubwa sana duniani hivyo kupelekea kuathiri mfumo mzima wa uendeshaji biashara duniani. Mwaka 2011 mwandishi Marc Andreessen alinukuliwa akisema, “Softwares are eating the world” akiwa na maana ugunduzi wa programu za kompyuta unarahisisha shughuli nyingi za kibinadamu kufanyika kwa haraka, kwa unafuu na kwa ufanisi zaidi kila siku zinavyozidi kwenda mbele. Sasa unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako? Leo tufahamu kwa undani.
Kufikia Octoba, mwaka 2018 tovuti ya Lifehacks (lifehacks.io) iliripoti kwamba jumla ya tovuti bilioni 1.9 zilithibitika uwepo wake kwenye intaneti pamoja na kuripotiwa kuwepo kwa machapisho (posts) zaidi ya milioni tano (5) ya blogu mbali mbali duniani kila siku. Tafiti hii ya kimtandao inakupa sababu mbali mbali za kukuwezesha kufanya biashara kwa kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta. Fuatana nasi.,
1. KUWA NA MPANGO WA BIASHARA ILI KUJUA KIUNDANI UNAWEZAJE KUTUMIA TEKNOLOJIA YA INTANETI NA KOMPYUTA:
Ukiwa na ndoto za kufanya biashara yako iwe na mafanikio maradufu, huna budi kuwa na mpango madhubuti wa kibiashara ambao utaainisha aina ya biashara unayoifanya, Jina la biashara linaloendana na aina ya bidhaa/huduma unayotoa, maudhui bora ya tovuti, soko unalolilenga na mbinu stahiki za kulikamata soko la kudumu.
2. TAFUTA NA CHAGUA JINA ZURI LA TOVUTI YA BIASHARA YAKO MTANDAONI:
Unapofikiria kuanzisha biashara, fikiria soko kwanza kabla ya aina ya biashara unayoitaka. Yaani tizama kwenye jamii, changamoto zilizopo ambazo hazijatatuliwa au hazionekani kama ni changamoto sana kwa muda huo, halafu tafuta suluhisho la changamoto hizo. Suluhisho hilo liendane na Jina zuri la kuwasilisha kile unachotaka kutatua kwenye jamii.
Uza suluhisho na si bidhaa kama bidhaa. Ukishapata Jina zuri, tengeneza tovuti yako au tafuta wataalamu waliobobea kwenye ujenzi na uendelezaji wa tovuti bora za kibiashara. KUMBUKA Tovuti sio Bidhaa bali ni Jukwaa la kufanyia biashara zako kama ilivyo ofisi yako, Fremu au Meza ya kuuzia bidhaa zako kila siku. Tofauti na ofisi, fremu au meza., tovuti ni jukwaa la kimtandao linalokuwezesha kuonyesha bidhaa/huduma zako dunia nzima kiurahisi zaidi mara moja. Kuhusu Umuhimu na faida za tovuti (website) katika biashara yako tayari nimekuwekea makala hizi hapa. Zitakufaa sana katika kuimarisha biashara yako ukizipitia zote.
3. TANGAZA NA WEKA UTARATIBU WA KUFUATILIA BIASHARA YAKO:
Dunia inakadiriwa kuwa na watu zaidi ya bilioni 7 mpaka sasa. Kati ya hao watumiaji wa mitandao ya kompyuta wanakadiriwa kufika bilioni 4 ikiwa ni takwimu zilizowasilishwa na yovuti ya lifehacks. Katika watu zaidi ya bilioni 4 ambao ni watumiaji mubashara wa mitandao ya kompyuta na simu, zaidi ya watu bilioni 2.234 wamegundulika kuwa ni watumiaji wa mtandao wa kijamii wa facebook peke yake.
Mfumo wa kimtandao wa kompyuta uitwao Internet Live Stats (ILS) unatumika kufuatilia watumiaji mubashara wa watumiaji wa Intaneti duniani kote kila siku. Hii ina maana kwamba zaidi ya nusu ya jumla ya watumiaji wote wa mitandao ya kompyuta na simu duniani wanapatikana facebook. Vilevile asilimia thelathini (30%) ya jumla ya idadi nzima ya watu wanaoishi duniani ni watumiaji wa facebook.
Kwa kusema hivyo, tayari tumekuwekea makala maalum itakueleza kwanini ni muhimu uitangaze biashara yako kila siku. Tafadhali ipitie makala hio mpaka mwisho kupitia link hii hapa yenye kichwa KWANINI UITANGAZE BIASHARA YAKO.
Hivyo kwa kuutumia vyema mtandao wa facebook peke yake kibiashara unajiweka kwenye nafasi ya kuwafikia zaidi ya watu bilioni 2 ambao wanaweza kuwa wateja wazuri katika biashara unayoifanya. Vile vile watu zaidi ya bilioni 1 wamefahamika kuwa ni watumiaji wa mtandao unaoshika kasi wa Instagram.
Zaidi ya hayo pia kama mfanyabiashara mwenye kiu ya mafanikio una wajibu wa kufuatilia maendeleo ya biashara/kampuni/taasisi yako katika muktadha wa kuichumi na masoko. Biashara inabidi iwe inakua katika viwango vinavyohitajika kulingana na kasi ya soko la dunia.
Hivyo baada ya kujiuliza unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?, sasa unao uwezo wa kufuatilia biashara yako kwa kutumia takwimu sahihi kama ongezeko la wateja ndani ya muda fulani (wiki, mwezi au mwaka), ongezeko la faida, taarifa za mapato na matumizi na zaidi, usalama wa taarifa zako kibiashara.
Pia katika ufuatiliaji unaweza kuongeza njia kusambaza taarifa kuhusu biashara yako. Moja ya njia hizo ni Search Engine Optimization ambayo ni huduma inayotolewa na makampuni ya programu za kompyuta na mitandao. Huduma hii hukupatia nafasi ya kusambaza links za tovuti au mifumo yako ya kompyuta ambapo mtu yeyote anapotafuta bidhaa au huduma zako katika mtandao, basi inakuwa rahisi zaidi kukupata kwa kuandika maneno yanayohusu huduma hio unayotoa.
4. JIBU KWA WAKATI NA KWA UWELEDI ILI UNAPOJIULIZA UNAWEZAJE KUTUMIA TEKNOLOJIA YA INTANETI NA KOMPYUTA MTANDAONI UPATE ULE MVUTO WA KIBIASHARA
Unapokuwa mfanyabiashara au mhusika katika kampuni/taasisi fulani maana yake upo hapo kwa ajili ya wateja wako, hivyo unapaswa kutoa majibu na ufafanuzi wowote unaofika kwako kutokea kwa wateja wako. Aina ya majibu au ufafanuzi wako huchangia kwa kiasi kikubwa kupata wateja wapya kila siku au kupoteza wateja kila siku. Waswahili wanasema “Kauli Njema ni Silaha.” Hivyo kwenye kauli zako za kuhudumu ni lazima uweke uweledi wa hali ya juu ili kumvutia na kumridhisha mteja na bidhaa/huduma zako.
Kulingana na elimu ya wanasaikolojia mtu yeyote hupenda kujibiwa mara moja pale anapokuwa na shauku ya kujua jambo fulani. Hivyo unaposhindwa kujibu au kutoa ufafanuzi wa jambo fulani kuhusu bidhaa/huduma kwa wakati, unajiweka kwenye nafasi mbaya ya kupoteza wateja wengi kila siku.
5. BADILIKA KULINGANA NA SOKO LINAVYOKUHITAJI KUBADILIKA:
Dhana ya Biashara na masoko inafanana na dhana ya muziki na mtu anayeucheza muziki huo. Yaani unapaswa kuendana na mdundo wa muziki pale unapokuhitaji. Hali kadhalika unapokuwa katika ulimwengu wa biashara kwa kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta soko lako linakuwa ni kuwafikia watu bilioni 7 waliopo duniani.
Na bahati ni kwamba duniani wapo watu/kampuni/taasisi nyingi ambazo zinafanya biashara unayoifanya wewe, hivyo unapaswa kuwa mbunifu kila siku, unapaswa kuongeza ubora wa bidhaa na huduma, kuongeza mtandao wa washirika wako duniani, bidhaa/huduma mpya na mambo mengi ambayo hujitokeza kila siku kulingana na uhitaji wa wateja. Hapa inakubidi uwe mwanafunzi mwenye uwezo wa kunyumbulika wakati wowote kwa ajili ya wateja wako.
Kwanini ufanye hivyo? Majibu zaidi yanapatikana kupitia makala hizi hapa:
Zaidi, tambua Tovuti ya kwanza kabisa kuundwa duniani bado ipo hewani (info.cern.ch). Tovuti hii ilitengezwa kwa lugha ya kuundia mifumo ya kimtandao ya HTML na inaonyesha mistari michache tuu. Lakini sasa mambo ni tofauti sana katika uwanda wa usanifu na uendelezaji wa programu za kompyuta na tovuti. Kama mwandishi Marc Andreessen alivyonukuliwa mwaka 2011 akisema programu za kopyuta zinaila dunia.
Je unajiandaa vipi kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako? Tafadhali toa maoni yako kupitia comments hapo chini..
Iwe ni shirika binafsi, taasisi za uma(serikali), mashirika ya dini au biashara binafsi, matangazo ni muhimu sana katika maisha ya taasisi au biashara binafsi. Kutuma barua pepe, kuanzisha kurasa katika mitandao ya kijamii au kufikisha taarifa za ana kwa ana kwa uma ni bure (haijumuishi gharama za moja kwa moja). Lakini kutangaza biashara ni gharama zaidi, hata hivyo inakulazimu kuitangaza biashara yako. Makampuni na mashirika duniani hutumia gharama kubwa sana katika kujitangaza japokuwa tayari wana majina makubwa na bidhaa/huduma zao zinajulikana duniani kote. Sasa swali la msingi, kwanini uitangaze biashara yako? Makinika hapa leo kupata majawabu.
Coca cola Company kwa mfano, mwaka 2015 walitumia dola bilioni 3.96, 2016-dola bilioni 4, 2017-dola bilioni 3.96. Kwa upande mwingine Pepsi ambao ni mpinzani wa kibiashara wa Coca cola duniani wao mwaka 2015 walitumia dola bilioni 2.4 kufanya matangazo yao, mwaka 2016- dola bilioni 2.5, mwaka 2017 dola bilioni 2.4. Hii ni kwa mujibu wa tovuti ya Investopedia (http://www.investopedia.com). Sasa, jiulize Kwanini ni muhimu uitangaze biashara yako.!?
1. MASOKO: Katika muktadha wa ulimwengu wa kibiashara, masoko ndiyo moyo wa biashara haswa. Yaani ili biashara yoyote iweze kuendelea kufanya vizuri, haina budi kuwa na soko la kutosha la kuhudumia. Jiulize, bidhaa unazosambaza/unazouza au huduma unayotoa, kuna kampuni au biashara ngapi ambazo zinafanya kitu hicho hicho unachokifanya.!? Kama hauko peke yako, basi hauna budi kutafuta masoko kwa hali na mali ili biashara yako ipate hadhira ya kuhudumia.
2. KUTAMBULISHA BIDHAA/HUDUMA MPYA: Ukuaji wa biashara/kampuni au taasisi yako hujumuisha kwa kiasi kikubwa ubunifu kila siku. Sehemu ya ubunifu huo pia huchagiza utambulisho wa huduma/bidhaa mpya kwa wateja wako. Ili uweze kuwafikishia taarifa wateja wako kuhusu huduma/bidhaa mpya unayoongeza katika biashara/kampuni au taasisi yako, unalazimika kuitangaza huduma/bidhaa hio mpya ili ifike kwa urahisi na usahihi kwa wateja wako.
3. ELIMU KUHUSU BIDHAA/HUDUMA ZITOLEWAZO NA TAASISI:Taasisi yako inapotoa huduma/bidhaa zake kwa mlaji wa mwisho au mteja wako hujumuisha zaidi sana elimu ya jinsi ya kutumia bidhaa/huduma hio. Sio watu wote watajua jinsi au njia za kuipata na kutumia kwa usahihi bidhaa/huduma zinazotolewa na taasisi yako. Vile vile ili elimu hio kuhusu bidhaa/huduma zako ipate kufika kwa mlaji wa mwisho au mteja wako huna budi kufanya tangazo. Hivyo matangazo ya namna hii yenye lengo la kutoa elimu ni muhimu sana katika kuhakikisha huduma/bidhaa zako zinafika kwa wateja lakini zaidi zinatumika kwa usahihi ule unaohitajika.
4.KUTENGENEZA MVUTO WA KIBIASHARA:
Matangazo ni njia bora zaidi kutengeneza mvuto wa kibiashara. Hapa kuna namna nyingi sana katika kutengeneza mvuto huu wa kibiashara kwa kutumia teknolojia ya matangazo. Aina ya mavazi au sare zinazohimizwa kuvaliwa katika taasisi yako, muundo wa rangi rasmi za taasisi, logo ya taasisi pamoja na jina la taasisi linavyohusiana na aina ya bidhaa/taasisi inayotolewa. Mvuto huu wa kibiashara hufanya matangazo ya kiautomatiki yanayokwenda moja kwa moja katika maisha ya kila siku ya mlaji wa mwisho au mteja. Huku mtandaoni tunatumia teknolojia ya SEO kutengeneza mvuto huu. Sasa kufahamu zaidi kuhusu SEO fuatana na makala hii hapa;
Matangazo ni sauti ya taasisi kuhusu bidhaa/huduma zake kwa wateja wao. Hivyo taasisi inavyofanya matangazo ndivyo inavyozidi kujiongezea wigo wa sauti yake kufika duniani kote. Duniani kuna kadiriwa kuwa na watu zaidi ya bilioni 7, hivyo unapofanya tangazo moja ni ngumu sana kuwafikia watu wote hao zaidi ya bilioni 7 duniani. Hivyo unapofanya matangazo kwa ajili ya wateja wako duniani mara kwa mara, unaimarisha jina la kampuni kitu ambacho huimarisha bidhaa/huduma zako zaidi pia.
6. KUJIKITA KWA WATEJA MAALUM TAASISI INAYODHAMIRIA KUWAPATA:
Kwa kawaida unapojihusisha na biashara ya kuuza nguo kama taasisi, wateja wako wakubwa watakuwa ni wauzaji wa nguo wadogo wadogo, wanamitindo na watu wengine wanaopenda kuvaa nguo za aina mbali mbali kila siku. Hivyo unapofanya matangazo ya taasisi yako, unajiweka kwenye nafasi ya kuwapata wateja haswa wale ambao taasisi imedhamiria kuwafikia.
7. UWEZO WA TAASISI KUHUDUMU:
Kwa kiasi kikubwa matangazo huimarisha uwezo wa taasisi kuhudumu. Hivyo taasisi yako inapofanya matangazo inajiweka kwenye nafasi ya kujiweka tayari kuhudumu kwa wateja wale wote wanaoletwa na matangazo hayo. Hivyo taasisi inayofanya matangazo hujiweka kwenye nafasi ya kuwa na ufanisi zaidi kwenye utendaji wake wa kila siku.
Hivyo kwa ufupi hayo ni baadhi ya mambo muhimu kuhusu Umuhimu wa Ufanyaji wa Matangazo katika taasisi/kampuni au biashara yako. Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi tukupatie usaidizi pale unapohisi kukwama katika biashara zako katika muktadha wa teknolojia ya habari na mawasiliano.
Namna bora ya kuitangaza biashara yako ni kupitia matumizi ya tovuti rasmi ya biashara yako pamoja na matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii ili kuhakikisha biashara yako inabaki katika akili za wateja wako kila siku. Hivyo pitia makala kupitia links hizo hapo chini ili uzidi kufahamu mambo muhimu kwa ajili ya afya ya biashara yako.
Una maoni au lolote kuhusu makala hii ya leo? Tafadhali, acha comment yako hapo chini na changia hoja yako. Karibu sana.
Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?
Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?
Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.
Mwaka 2017 Makampuni ya CISCO na Microsoft yalitoa ripoti yao ya mwaka kuhusu Usalama wa masuala ya Kimtandao ambapo ilionekana kwamba matukio ya udukuzi yaliongezeka maradufu katika maeneo ya kibiashara/kampuni na taasisi mbali mbali. Zaidi ya hayo iligundulika kwamba biashara nyingi licha ya kuingia katika majanga ya kudukuliwa taarifa zao, zilijikuta zikipoteza vitu vingine vingi kwa wadukuzi wa kimtandao na wezi zaidi hata ya pesa na taarifa zao.Sasa leo tuone kuhusu hifadhi mbadala ya nyaraka (Data Backup), ni nini na inafanya kazi vipi. Fuatana na makala hii mpaka mwisho.
Kulingana na Shirika la Acromis, zaidi ya nusu ya biashara zote duniani ni muhanga wa matukio ya udukuzi wa kimtandao na wizi wa taarifa muhimu za taasisi. Matukio hayo yanahofiwa kusababisha hasara kwa kampuni kutokana na kuharibu taswira ya taasisi katika jamii, kushusha heshima ya wateja kwa taasisi na kupunguza uaminifu wa taasisi kwa wateja wake na jamii kwa ujumla. Kuhusiana na udukuzi na namna unavyoweza kupambana nao bila shaka utataka kujifunza kupitia makala hii hapa chini.
Ripoti hiyo ya CISCO na Microsoft pia imetaja kwamba zaidi ya aslimia ishirini na tisa (29%) ya biashara ambazo ni muhanga wa mashambulio ya udukuzi hupoteza mapato yao na takribani asilimia arobaini (40%) ya biashara hizo hupoteza asilimia ishirini (20%) ya jumla ya mapato yao kwa mwaka.
Kati ya biashara zilizopo duniani, takribani robo ya biashara hizo hupoteza nafasi muhimu sana za kuongeza wigo wa kibiashara kufuatia kupotea kwa taarifa zake kuishia mikononi mwa wadukuzi na matukio ya wizi wa nyaraka. Na zaidi ya 20% ya biashara zinazopitia katika janga ya kupotea kwa nyaraka zao muhimu hupoteza pia wateja wao. Na 40% kati yao hupoteza zaidi ya 20% ya wateja wao kila mwaka.
Zaidi ya wadukuzi wa kimtandao na matukio ya wizi wa nyaraka, Majanga ya kiasili yanayotokea duniani pia huchangia kwa kiasi kikubwa upotevu wa nyaraka muhimu za taasisi. Mafuriko, Majanga ya Moto, Hali ya unyevu unyevu, Kimbunga na Tetemeko la ardhi husababisha athari kubwa zaidi katika uhifadhi wa taarifa muhimu za taasisi. Kutokana na kuongezeka kwa matukio ya upotevu wa taarifu hizo muhimu za taasisi na biashara mbalimbali, wataalamu wa masuala ya uhifadhi wa taarifu na nyaraka muhimu za kibaishara na taasisi duniani kupitia katika ripoti ya mwaka ya makampuni ya CISCO na Microsoft, njia mbali mbali za hifadhi mbadala ya nyaraka (Data Backup) zilishauriwa:
1. NJIA YA 3-2-1:
Njia hii ni kanuni bora sana ya kuhifadhi nyaraka na taarifu za kampuni/taasisi au biashara kwa urahisi na wepesi zaidi. Inafanya kazi kama ifuatavyo., • Tengeneza nakala tatu (3 copies) kaika kila nyaraka zako unazozifanyia kazi kila siku. Hapa unajihakikishia kwamba hakuna tukio lolote ambalo litaweza kuziharibu nakala zote tatu kwa urahisi.
• Katika nakala zako tatu, mbili (2) zihifadhi katika mitindo (formats) tofauti ambayo inaweza kuwa disk format, tape, cloud na kadhalika.
• Nakala moja (1) iweke mbali kabisa na mahali unafanyia kazi (inaweza kuwa nyumbani, mkoani, nchi nyingine n.k) ili kuepuka hatari ya majanga ya moto, unyevu unyevu, mafuriko, vimbunga na wezi.
2. NJIA YA MTANDAO WA KOMPYUTA:
Njia hii pia imethibitika kuwa na ubora katika uhifadhi mzuri wa nyaraka. Hapa nyaraka zinahifadhiwa katika kompyuta zaidi ya moja ambazo zimeunganishwa katika mtandao fulani( inaweza kuwa LAN, MAN au WAN). Njia hii huhakikisha usalama wa nyaraka za taasisi au biashara yako kuongeza uwezo wa upatikanaji wa nyaraka kwa wahusika wale tuu waliokusudiwa kushirikiana katika kufanyia kazi na kuhifadhi nyaraka hizo katika muda muafaka.
3. NJIA YA INTANETI (CLOUD BACK UP):
Hii ni njia rahisi na ya kisasa zaidi katika nyanja ya uhifadhi mbadala wa Nyaraka za taasisi/kampuni au biashara yako. Katika njia hii kanuni kubwa inayotumika ni kupandisha nyaraka zako katika majukwaa ya kimtandao ambayo yanatoa huduma hio ya uhifadhi kwa njia ya Intaneti.
Mpaka kufikia mwaka 2022 katika intaneti inakadiriwa kutakuwa na zaidi ya Terabite (TB) bilioni 2 za nyaraka zitakazohifadhiwa. Mashirika na Makampuni ya kimataifa ya NASA na GOOGLE yanajipanga kila siku kuongeza nafasi ya uhifadhi katika majukwaa yao ya huduma za intaneti. Hali kadhalika makampuni mengi zaidi yanaibuka duniani na kutoa huduma hii ya uhifadhi wa nyaraka kwa intaneti ambapo huduma hii inazidi kuboreshwa kila siku.
Kampuni la Microsoft kwa mfano, limeanzisha huduma ya Office 365 ambayo ni mageuzi ya Programu ya Microsoft Office ambayo watu wengi duniani wamezoea kuitumia katika kazi zao za kila siku. Hata hivyo huduma hii ya office 365 ni ya kimtandao zaidi ambapo sasa mtu unaweza kufanya kazi zako ukiwa popote na katika vifaa mbali mbali vya kielektroniki kama simu janja na kompyuta mpakato ikiwa tuu tayari umeshajipatia huduma hii kutoka Microsoft. Hali kadhalika kampuni ya Google nayo imeanzisha huduma ya Google Drive ambapo inawezesha kuhifadhi nyaraka zako vizuri, kwa muda mrefu na kwa usalama wa hali ya juu. Vile vile duniani yameanzishwa majukwaa mengine mengi ya huduma za uhifadhi nyaraka kwa intaneti kama Dropbox, Acronis Data Backup na kadhalika.
Lengo kuu la huduma hizi za hifadhi mbadala ya nyaraka (Data Backup) zako ni kuhakikisha Usalama wa taarifa zako za kibiashara au taasisi/kampuni unakuwa wa hali ya juu na hivyo kuongeza ufanisi wa huduma/bidhaa zako kila siku.
Kama una la ziada usisite kuwasiliana nasi kuweza kupata huduma bora na za kisasa za kimtandao ili kuimarisha biashara yako ili iweze kuendana na kasi ya kidunia. Wasiliana nasi kupitia mawasiliano yetu hapa au komenti hapa chini. Karibu sana.