Archive: 23 October 2019

FAHAMU KUHUSU UVUVI NA BIASHARA YA SAMAKI BARANI AFRIKA

Japokuwa inafanyika zaidi maeneo ya vijijini na katika hali duni ya zana za utendaji, elimu pamoja na teknolojia, sekta ya uvuvi na biashara ya samaki bado inahangaika katika kujiboresha huku ikifichwa katika kivuli cha shughuli za Kilimo na Ufugaji. Mbaya zaidi sekta ya uvuvi na biashara ya samaki bado haijapewa umuhimu inayostahili barani humo. Zaidi sekta hio hutoa chakula cha kuwalisha watu zaidi ya milioni 200 barani humo na nje ya bara la Afrika. Leo sasa fahamu kuhusu Uvuvi na biashara ya samaki barani Afrika. Twende mpaka mwisho.

Benki ya Dunia inaripoti kwamba shughuli za uvuvi na biashara ya samaki huchangia moja kwa moja dola za kimarekani $24 bilioni katika uchumi wa Afrika kwa ujumla, ikiwakilisha 1.3% ya jumla ya pato la ndani (GDP) la Afrika katika mwaka 2011. Vile vile sekta hio imezalisha ajira kwa zaidi ya watu milioni 12 ambapo 58% kati yao ni wavuvi na 42% wanajihusisha na kuandaa samaki waliovuliwa kabla ya kuwapeleka sokoni. Tanzania peke yake, sekta ya uvuvi imetoa ajira kwa watu 183,000 mpaka kufikia mwaka 2014 (chanzo: Wizara ya Kilimo, Ufugaji na Uvuvi) Ikionekana kwamba shughuli za uvuvi hufanywa zaidi na wanaume, 59% ya shughuli za kuandaa samaki kabla ya kuwaingiza sokoni hufanywa na wanawake.

Ukiachana na faida za samaki kama chakula katika kupatikana kwa virutubisho muhimu kama vitamini, protini na mafuta, zaidi, sekta ya Uvuvi na biashara ya samaki inachangia sehemu muhimu sana katika kuendesha maisha ya watu haswa vijana ikiwa watachukua angalizo katika fursa zilizopo kwenye sekta hio.

Changamoto; Je, kuna fursa zipi katika kufanya shughuli hii ya uvuvi na biashara ya samaki katika kukuza uchumi? Teknolojia ina mchango gani katika kuboresha uchumi wa mtu mmoja mmoja kupitia setka hii?

Tishio kubwa katika shughuli za uvuvi na biashara ya samaki ni athari zinazotokea katika mazalio ya samaki baharini, mtoni, ziwani au kwenye mabwawa. Umoja wa Mataifa na nchi  jumuishi duniani zimeingia uwoga juu ya upatikanaji wa hazina ya samaki katika soko la dunia. Shirika linaloshughulikia maswala ya Chakula duniani, FAO, limetabiri kwamba zaidi ya 70% ya aina (species) za samaki zinakaribia kuangamia au zimevunwa sana ambapo aina za samaki kama Tuna, Swordfish, Haddock na Flounder zipo katika tishio la kuangamia. Zaidi, uvuvi unaotumia chandarua au baruti huweza kusababisha kunaswa au kuuwawa kabisa kwa samaki na viumbe wengine wa baharini ambao hawajapangwa kuvuliwa kama ngasa, pomboo na papa.

Hata hivyo, shughuli za uvuvi zina faida gani katika maisha ya mwanadamu ikijumuisha?

  1. CHAKULA;  Samaki ni chanzo cha vitamini na protini katika lishe haswa ya mwanadamu ambapo madaktari na wadau wa sekta ya afya hushauri ulaji wa nyama nyeupe mfano samaki zaidi katika mlo. ulaji wa samaki kwa wingi huchochea ukuaji bora wa afya ya akili pamoja na wingi wa protini katika nyama hio huku ikiwa na kiasi kidogo cha lehemu (cholesterol) zaidi kuliko nyama nyekundu mfano ng`ombe, mbuzi na kadhalika.Ripoti zinaonyesha kwamba wakazi wa nchi za ukanda wa bahari ya Pacific peke yake hupata zaidi ya 25% na 69% ya protini za wanyama wanaokula kila siku kutoka katika samaki. Hii imepelekea shughuli za uvuvi na biashara ya samaki kukua kwa kiasi kikubwa kama shughuli rasmi ya kiuchumi ambayo imeajiri watu takribani milioni 200 dunia nzima na ikizalisha pato la dola za kimarekani zaidi ya 80 bilioni kwa mwaka.
  2. UKUAJI WA UCHUMI; Sekta hii ya uvuvi inachangia kwa kiasi kikubwa sana katika ukuaji wa uchumi barani Afrika mpaka dunaini kote ambapo watu zaidi wa milioni 200 wamejipatia ajira kupitia sekta hio. Nchini Uganda kwa mfano, uvuvi wa ziwani umekuwa na thamani ya zaidi ya dola $200 milioni  kwa mwaka ikiwa ni mchango wa 2.2% katika pato la taifa (GDP) la nchi hio. Vile vile watu zaidi ya 135,000 wamepata ajira kama wavuvi katika sekta hio na wengine 700,000 zaidi katika mchakato wa kuandaa samaki kabla hawajafikishwa sokoni na hivyo kuzalisha zaidi ya dola $87.5 milioni kama mapato ya biashara za nje ya nchi (exports earnings). Hapa miundombinu ya barabara na reli ina mchango mkubwa sana katika kuhakikisha kitoweo hiki kinamfikia mlaji kikiwa katika ubora wa hali ya juu. Kufahamu zaidi kuhusu mchango wa miundombinu pitia makala hii hapa;
  1. Vile vile nchini Tanzania kupitia katika mabwawa, maziwa, mito na bahari vilivyomo nchini humo, sekta ya uvuvi na biashara ya samaki imetoa ajira za moja kwa moja kwa watu takribani 183,800 na wengine zaidi ya 4,000,000 wakijihushisha kama watengenezaji wa vyombo vya uvuvi (ngalawa, boti, ndoano, neti n.k), waaandaaji wa samaki kabla hawajafikishwa sokoni, wachuuzi na wafanyabiashara wa samaki wa jumla na rejareja. Sekta hii ya uvuvi na biashara ya samaki inawapatia watu kipato cha fedha za kigeni, pamoja na kitoweo kwa watu waishio pwani ya bahari ya hindi pamoja wa walaji wa samaki kutoka sehemu zingine katika nchi hio ambapo sekta hio huchangia katika pato la taifa takribani 2.4%. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya Wizara ya Kilimo, Ufugaji na Uvuvi katika mwaka 2016.

Kiujumla, mpaka kufikia mwaka 2001 uta fahamu kuhusu Uvuvi na biashara ya samaki barani Afrika katika masoko ya kimataifa ilikuwa na thamani ya dola $2.7 bilioni ambayo ni 5% ya jumla ya thamani ya sekta nzima ya uvuvi na biashara ya smaki duniani ambayo ni dola $56 bilioni. Kwa mujibu wa shirika la FAO, bidhaa za samaki zimejumuisha zaidi ya 10% ya jumla ya biashara za kimataifa (exports) katika nchi 11 barani Afrika.

Sasa Baada ya kuyajua Hayo Yote, Kwanini Ufanye biashara hii ya Uvuvi na samaki?

Mwaka 2019 watumiaji wa huduma za intaneti nchini Tanzania waliongezeka kufikia milioni 23, ongezeko la watumiaji takribani milioni 1 kutoka mwaka jana 2018. Vile vile watumiaji wa huduma za kifedha kwa njia ya simu za mkononi wamefikia takribani milioni 20 hadi kufikia mwaka huu 2019. Hii ni kwa mujibu wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini TCRA.

Hivyo kupitia ripoti hio ya TCRA mfanyabiashara anaweza kuhamishia shughuli zake kupitia simu mkononi na simu janja (smartphones) katika kuhakikisha biashara yake inawafikia watu wengi zaidi katika muda mfupi kwa njia ya Teknolojia. Hata hivyo mfanyabiashara anaweza kutengeneza majukwaa ya kimtandao kama tovuti za kibiashara (online shops na ecommerce websites) ambayo anaweza kuuza bidhaa zake za samaki kirahisi katika masoko ya ndani na hata yale ya kimataifa kwa gharama nafuu zaidi kuliko ulivyokua hapo kabla.

Jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko la Mtandaoni

Kwa kutambua hilo, biashara ya mtandaoni imekuwa ikizidi kufanikiwa sana nyakati hizi huku ikichochewa na maboresho katika miundombinu ya uchukuzi na usafirishaji. Hivyo ni muhimu kufungua tovuti rasmi ya biashara yako ili kuipa utambulisho usio na shaka ukiwa mtandaoni. Vilevile ni muhimu kufungua akaunti za mitandao ya kijamii ili kusudu uzidi kujiweka karibu na wateja wako na kujua namna nzuri ya kuwahudumia.

Link zifuatazo zitakusaidia sana uweze fahamu kuhusu Uvuvi na biashara ya samaki barani Afrika kupitia mtandaoni iwe na mafanikio zaidi na zaidi:

  1. WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?
  2. KWANINI NI MUHIMU KUWA NA TOVUTI RASMI YA BIASHARA YAKO?
  3. IFAHAMU NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO

Je umepata nini katika mada ya leo katika ku fahamu kuhusu Uvuvi na biashara ya samaki barani Afrika?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?

UMUHIMU WA TAKWIMU KATIKA UTOAJI WA HUDUMA BORA KWA WATEJA

Mteja hakosei na mteja ni mfalme. Hizi ni kauli maarufu sana katika biashara duniani, lakini haswa biashara zinazofanyika kusini mwa jangwa la Sahara. Maana yake ni kwamba, Mteja anatakiwa kusikilizwa na kuridhishwa na huduma/bidhaa zinazotolewa na mfanyabiashara. Je, wewe unatumia mbinu zipi ili kuhakikisha huduma/bidhaa zako zinawaridhisha wateja wako? Katika makala yetu ya leo utakwenda kufahamu kwa undani siri na umuhimu wa takwimu katika utoaji wa huduma bora kwa wateja. Twende pamoja mpaka mwisho.

Sasa ripoti ya mwaka 2019 kutoka shirika la kimataifa la ukaguzi wa mahesabu la PwC imeonyesha kwamba 64% ya Wakurugenzi wa Makampuni na Wafanyabiashara barani Afrika hawana data na takwimu kuhusu mwenendo wa wateja wao. Inashangaza eeh?

Kwa upande mwingine ripoti ya McKinsey imeonyesha kwamba makampuni yanayotumia data na takwimu sahihi kuhusu mwenendo wa wateja wao huyazidi yale yasiyofanya hivyo kwa 85% katika ushindani wa masoko na 25% zaidi katika kuingiza mapato kila mwaka.

Zaidi 95% ya wateja huongelea zaidi huduma mbovu walizokutana nazo katika kampuni/biashara fulani (Mtandao wa American Express), hali kadhalika 89% kati yao huacha kabisa kufanya biashara na kampuni/biashara fulani baada ya kukumbana na huduma/bidhaa zisizokidhi mahitaji/viwango walivyotegemea (ripoti ya Huduma kwa wateja ya mtandao wa RightNow). Kama unaijali biashara yako na ungependa kuona inazidi kukua, makala haya ni kwa ajili yako.

Sasa Changamoto; Kuna umuhimu gani katika kumridhisha mteja wako katika biashara unayofanya baada ya kujua takwimu sahihi kuwahusu?

1. KUONGEZA MAHUSIANO MAZURI NA MTEJA; Mteja aliyeridhishwa na huduma/bidhaa zako atabaki kuwa mteja wako kwa muda mrefu zaidi kutokana na huduma bora anazopata kutoka katika kampuni/biashara yako. Hakikisha unamshirikisha mteja kufanya maamuzi katika mchakato mzima wa kuhudumia. Muulize maswali kama Unaonaje ikiwa hivi au ikionekana vile, Unajiskiaje. Mpeti peti mteja wako muda wote kama unataka aendee kutumia huduma/bidhaa zako.

2. Waswahili wanasema, Kauli Njema ni silaha. Yaani unapokuwa na Kauli njema katika kusambaza huduma/bidhaa zako, unaiweka bishara/kampuni yako katika nafasi nzuri ya kuishindani dhidi ya washindani wako katika soko. Kauli njema ni kama sumaku ambayo inawaleta pamoja wateja na huduma/bidhaa zako na hivyo kufanya wateja wako kuendelea kuwa wako, lakini zaidi kauli njema huwavuta pia wateja wapya kuanza kutumia huduma/bidhaa zitokazo katika biashara/kampuni yako.

umuhimu wa takwimu katika utoaji wa huduma bora kwa wateja

3. KUPUNGUZA GHARAMA ZA MATANGAZO; Kampuni/biashara yako inapotoa huduma bora kwa wateja wake huwafanya wateja hao kuwa mawakala ambao hutangaza huduma bora wanazopata katika kampuni/biashara hio. Kama tulivyoona hapo mwanzo, 95% ya wateja duniani hueleza katika jamii zao jinsi walivyokutana na huduma mbovu/dhaifu walizokutana nazo katika kampuni/biashara fulani. 89% kati yao huacha kabisa kujihusisha na bishara/kampuni ambayo haikuwapatia huduma bora au haujali wateja wake. Hata hivyo bado ni muhimu sana uendelee kuitangaza biashara yako. Gusa hapa kufahamu kwanini.

Na njia bora kabisa ya kutoa huduma bora na kwa wakati huo huo ukipunguza gharama za matangazo ni kwa kutumia teknolojia kama website iliyounganishwa na huduma za S.E.O. Kwanini uwe na website? Majibu yanapatikana kwenye makala hii hapa kufahamu kwanini ni muhimu kuwa na website rasmi ya biashara yako.

4. MAFANIKIO KATIKA BIDHAA/HUDUMA ZIJAZO; Kampuni/biashara hujiweka katika nafasi nzuri ya kufanikiwa katika kusambaza huduma/bidhaa zake mpya pale inapokuwa na kumbukumbu nzuri katika kutoa huduma bora kwa wateja wake.

Matokeo yake, kampuni/biashara hulenga wateja wake wa kudumu katika kusambaza huduma/bidhaa zao mpya ambapo hujihakikishia mafanikio kabla ya kuwasambazia wateja wapya. Hata hivyo wateja wanaoridhishwa na huduma bora zitolewazo hupendelea bidhaa/huduma mpya zitokazo katika kampuni/biashara walizowahi kuhudumiwa vizuri hapo mwanzo.

5. MTEJA WA KUDUMU NI LULU; Kwa mujibu wa Ikulu ya Marekani (#WhiteHouse) Ofisi inayoshughulikia maswala ya wateja, kwa wastani, mteja aliyeridhika na huduma/bidhaa (mteja wa kudumu) katika biashara ana thamani mpaka mara 10 zaidi kuliko thamani ya manunuzi yake ya kwanza.

Tafiti zingine zimeonyesha kwamba ni ghali zaidi ya mara 6 mpaka 7 kumpata mteja mpya kuliko kumtunza mteja wa aliyepo/wa kudumu. Taasisi za kifedha, mabenki na makampuni ya simu kwa mfano, yamejifunza sana katika hili, hivyo hawaoni tabu kuchukua hatua za ziada kuhakikisha mteja ambaye hakuridhishwa na huduma anapatitwa suluhu mbadala haraka sana kuendana na mahitaji yake. Hapa ndio utauona umuhimu wa takwimu katika utoaji wa huduma bora kwa wateja.

6. WANAWEZA KUACHA KUWA WATEJA WAKO MUDA WOWOTE; Si jambo la ajabu hasa katika zama hizi za usasa mteja kuhamia kampuni yoyote atakayopenda kutumia huduma/bidhaa zake. Hii huchochewa zaidi na huduma mbovu/dhaifu za wateja wanazopatiwa zikiwemo kusubirishwa muda mrefu katika kupatiwa huduma/bidhaa/mrejesho/maoni kutoka kwenye kapuni/biashara fulani. Ni jambo lisolopendeza kabisa, lakini bado mambo kama hayo yanaendelea kutukia.

“Mteja anapokwambia hitaji lake, hakwambii tu kuhusu maumivu yake, anakwambia pia jinsi ya kutengeneza bidhaa/huduma itakayomfaa pamoja na biashara yenye ubora. Huduma kwa wateja zinatakiwa kubuniwa katika namna inayotambua changamoto hizo.” Anasema Kristin Smaby katika mtandao wa https://alistapart.com.

Huwezi kupata wateja watakaoridhika na bidhaa/huduma zako milele. Hivyo yakubidi kama mfanyabiashara kuzitafuta changamoto zinazowakabili wateja wako kwa; kuzungumza nao, waulize maswali kuhusu vile wanataka kujiskia ukiwahudumia, wape msaada pale watakapohitaji, wape ofa, punguzo la bei na mambo kama hayo. Utakapowahudumia vizuri wateja wako utakidhi mahitaji ya wote; biashara yako na wateja pia. Wao wanapata huduma bora, biashara inapata mapato na kila mmoja anabaki na furaha.

Njia bora zaidi ya kuhakikisha unazipata changamoto zinazowakabili wateja wako ni Kwa kutumia vizuri mitandao ya kijamii. Mitandao ya kijamii ni kiungo muhimu sana cha kuunganisha mfanyabiashara na wateja wake katika kuimarisha viwango vya utaoji huduma. Sasa unawezaje kuitumia mitando hii kwa usahihi? Tafadhali fuatana na link hii hapa.

Ni matumaini yangu leo umefahamu kwa undani umuhimu wa takwimu katika utoaji wa huduma bora kwa wateja. Utakwenda kuzitumia vipi mbinu hizi za leo? Niambie kwenye comment hapo chini..

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo kuhusu umuhimu wa takwimu katika utoaji wa huduma bora kwa wateja.

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu(website design, logo design, Digital consultacy n.k) BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?
mapinduzi ya viwanda

FAHAMU KUHUSU MAPINDUZI YA 4 YA VIWANDA KATIKA BIASHARA DUNIANI

Japokua ilipitwa na zama 3 tayari, lakini sasa Afrika imedhihirisha kwamba haitaki kupitwa tena katika Mapinduzi ya 4 ya viwanda Duniani. Hii ni kutokana na kukua na kuimarika katika sekta za Afya, Elimu, Biashara, Teknolojia pamoja na Mahusiano na Muingiliano wa kijamii ikichagizwa na maendeleo katika miundombinu, usafirishaji na mitandao ya kijamii. Leo tuta fahamu kuhusu Mapinduzi ya 4 ya viwanda katika biashara duniani. Ni nini na yanaashiria nini kwenye maendeleo ya biashara zingine? Makninika mpaka mwisho.

Mwezi September, 2019, jijini Cape Town Afrika Kusini ulifanyika mkutano wa kiuchumi wa WEF (World Economic Forum) ambao unazishirikisha nchi mbali mbali duniani, wafanyabiashara pamoja na wadau wa uchumi.

Mwaka huo 2019 viongozi waliokutana kujadili mustakabali wa Afrika walikua na jambo la msingi sana ambalo linatumainiwa kuleta maendeleo katika uchumi barani ambalo ni Utekelezaji wa Kuanzishwa kwa Eneo Huru la Biashara Barani (African Continental Free Trade Area AfCFTA). Baada ya miaka mingi ya mazungumzo, makubaliano yamefikiwa ya jinsi ya kuvunja vikwazo vya kibiashara, kukuza uchumi na kuunganisha nchi ambazo katika historia zilikuwa na mahusiano mazuri ya kibiashara na bara Ulaya, Amerika na Asia. Kufahamu zaidi gusa hapa chini:

Changamoto; Afrika (wafanyabiashara, kampuni na mashirika) imejifunza nini katika Kongamano hilo la Kiuchumi (WEF)? Na zaidi, Afrika inajiandaa vipi na Mapinduzi ya 4 ya viwanda yanayoendelea duniani?

Kufikia mwaka 2018 Afrika peke yake iliripotiwa kuwa na vijana takribani milioni 200 wenye umri wa kati ya miaka 15 hadi 24. Na namba hio inatajwa kuongezeka mara mbili kufikia mwaka 2050.

Sasa “Kuwa na bara lililosheheni vijana ni fursa adhimu sana, lakini vile vile ni tishio kubwa.” alitahadharisha Albert Zeufack, Mchumi Mkuu wa Benki ya Dunia barani Afrika. “Ni tishio kama hatutohakikisha idadi hio ya vijana hawaanzi kufanya kazi inavyotakiwa.” Sasa kufikia Mapinduzi ya 4 ya viwanda, maeneo kadhaa yaliangaziwa na kituo cha mabadiliko ya kiuchumi barani (Africa Center for Economic Transformation, ACET) kwa niaba ya Benki ya maendeleo barani AfDB.

africa na mapinduzi ya viwanda

1. MACHINE LEARNING/ARTIFICIAL INTELLIGENCE/ROBOTICS;

Fikiria kuhusu gari inayojiendesha bila dereva na kufuata sheria na alama za barabarani ipasavyo ikijumuisha foleni. Watu wengi wangesita kupanda katika gari inayojiendesha yenyewe bila dereva, lakini hayo ndio mapinduzi halisi ya viwanda kupitia teknolojia.

Pia eneo hili limeshuhudiwa na ubunifu mwingi ukiwemo; mashine za kisasa za kuvuna na kupembua nafaka na madini, mifumo ya kiautomatiki inayoendesha ndege, meli pamoja na Teknolojia ya kupima udongo. Ni wazi mashine zinaweza kufanya kazi zifanywazo na binadamu katika zama hizi za mapinduzi ya 4 viwanda.

Swali, umejiandaeje kulinda taaluma yako dhidi ya zama hizi za mashine kujifunza (machinelearning) pamoja na teknolojia ya akili isiyo ya asili (ai)?

2. INTERNET OF THINGS (IoT);

Vifaa vingi vya kielektroniki vinavyotumiwa na mwanadamu sasa vinao uwezo wa kuingiliana na vifaa vingine kirahisi katika kurahisisha utendaji. Fikiria pale unarudi nyumbani na kuwasha feni yako kwa kutumia simu yako ya rununu (smartphone). Au kuweza kuendesha jokofu lako kwa kutumia teknolojia ya RFID. Kuunganishwa vifaa vya kielektroniki na huduma za intaneti imerahisisha sana mfumo wa mawasiliano na manunuzi ambao umeinua uchumi japo faida zake bado hazijasambaa sana barani Afrika.

Fikiria vile unaweza nunua bidhaa katika duka bila kumwona hata muuzaji. Hii inawezeshwa na teknolojia za biashara za kielektroniki (ecommerce) ambapo mteja anaweza kulipia kwa kutumia kadi yake ya benki au huduma za kifedha za simu ya mkononi kama MPESA na tigopesa. Katika bara ambalo muingiliano ni mkubwa kama Afrika, hili ni jambo la kutilia maanani sana, haswa wakati huu ambapo unajaribu ku fahamu kuhusu Mapinduzi ya 4 ya viwanda katika biashara duniani. (Ambapo sisi kama Rednet Technologies ni wadau wakubwa kuhakikisha hupitwi na huduma za kisasa kwa kutumia teknolojia).

Kufahamu mapinduzi ya IoT katika biashara na maisha kwa ujumla tayari tumekuwekea makala maalum kupitia link hii hapa MAGEUZI YA INTANETI (IoT) KATIKA BIASHARA NA MAISHA

3. DATA MINING/DATA SCIENCE TECHNOLOGIES;

Kituo cha ACET katika mwaka 2018 kiligundua kwamba “kuvua taarifa nyingi mtandaoni, kwa kutumia kompyuta zenye uwezo mkubwa na kanuni za mifumo ya Akili isiyo ya Asili (AI), huwezeshwa kupatikana kwa ripoti bora ya taarifa sahihi.” Fikiria mifumo ya tiketi za ndege, hoteli, mifumo ya kulipa kodi na taarifa za mteja wa benki.

Sekta ya Takwimu inafurahia sana ujio wa teknolojia ya Kuvua/Kuvuna Taarifa na Sayansi ya Taarifa. Jinsi ya utendaji katika teknolojia hii ni fursa adhimu sana katika kuimarisha biashara kwa kutumia takwimu sahihi zilizovunwa kutokana na taarifa mbalimbali za watu. Mifumo ya tiketi za ndege, Usajili wa vyumba vya Hoteli, taarifa za wateja wa benki na hata mfumo wa Kulipa kodi (Tax returns), hivi ni baadhi ya vyanzo vya ukusanyaji wa taarifa muhimu katika kufanya Uvunaji wa Data na Sayansi ya Data. Serikali za Africa zinamiliki kiwango kikubwa cha taarifa hizi. Je, italeta manufaa kwa Umma au itafanywa kama biashara na wajasiriamali? (Tafiti na ripoti tunazokuwekea kwenye makala zetu hizi zitakupa majibu.😋)

4. 3D PRINTING;

Ama kwa hakika mapinduzi ya viwanda yanakuja na mengi. Hebu buni bidhaa yako kwenye kompyuta halafu ichapishe kama ilivyo. Kutoka ubunifu uliotengenezwa kimchoro mpaka uhalisia katika kuchapisha tu, hii inakwenda kubadili hata namna ya uendeshwaji wa viwanda barani Africa ambapo ugunduzi huu unaleta matumaini katika uwanda wa ubunifu na ujenzi ambao unatazamiwa kuleta maendeleo katika nchi za Afrika. Viwanda vinawezaje kuendana na teknolojia hii ya Uchapishaji? Vimal Shah mkuu wa shirika la viwanda vya BIDCO nchini Kenya mwaka 2017 alinukuliwa akitania, “Tunaweza kuchapisha pizza wakati ujao.”😂

Sasa watunga sera na sheria barani walishaona uhalisia huu kama kuchapisha mfano wa kitu halisi (3D-Printing) katik mipango yao ya muda mrefu?

5. BLOCKCHAIN/TRUST TECHNOLOGIES;

Mwaka 2018 kituo cha ACET kiligundua kwenye uchunguzi wake kwamba teknolojia ya Blockchain inawafanya watu hata wasiaminiana au kujuana, kuweza kushirikiana bila ya kuwa na haja ya kwenda kwenye mamlaka za serikali. Yaani Blockchain ni jalada huru linalosajili miamala ya kifedha kati ya watu wawili au zaidi kwa usahihi na njia bora zaidi. (Tulishaelezea kuhusu Blockchain na cryptocurrencies kwenye makala zetu zilizopita). Sasa itakuaje kwa huduma za kibenki, wanasheria, wakala wa fedha (brokerage firms) na wahusika wa kiserikali katika maswala ya kifedha? Kitawakuta nini, tutajadili kwenye athari ya mapinduzi ya viwanda mbeleni.

mapinduzi ya viwanda

Si ajabu, teknolojia ya Blockchain inaonekana kama mkombozi dhidi ya vitendo vya Rushwa kutokana na undeshwaji wake ulio sahihi na wa haki. Kwa inavyoonekana teknolojia hii ya Blockchain inakwenda kuwa pigo kubwa kwa watu wenye misuli ya kiutawala, madikteta wa waendeshaji wa siasa chafu. Itakapofika siku Teknolojia hii imefikia matumizi yale yaliyonuiwa wakati inaanzishwa, basi wahafidhina na mawakala wa kifedha wa serikali na mashirika binafsi watapoteza nguvu zao. Hakutakuwa na haja ya mihuri, wala sahihi, wala zile nenda urudi kesho tukuhudumie. Blockchain itakwenda kuiweka Afrika huru dhidi ya kero za huduma za kifedha na usalama wake kuwa katika ukuaji mzuri. Haya ndio mapinduzi ya 4 ya viwanda duniani.

5. BIOPHYSICS AND BIOENGINEERING;

Eneo la 5 ambalo kituo cha ACET imeliacha ni kuhusu mtandao wa mifumo ya kibaolojia na kifizikia. Utahitaji mkono wa bandia unaoweza kuendeshwa na ubongo wako kwa usahihi ikitokea mkono wako halisi umekatika? Hebu fikiria hapo. Tunakubali kwamba asili ni bora sana kuliko sisi, hivyo ni bora kujifunza kwayo, kwasababu mapinduzi haya ya viwanda kwa kuchagizwa na ukuaji wa kiteknolojia duniani yatafanya taaluma ziweze kunyumbulika kwa namna nyingi sana hapo baadaye. Je, mifumo ya elimu imejiandaa na hili katika maandalizi ya mitaala yake ya muda mrefu?

Sasa tumeshajua yanayokuja na Mapinduzi ya 4 ya viwanda duniani. Afrika, bara ambalo ajira bado ni tatizo kubwa kwa vijana, wataweza vipi kupambana na athari za mapinduzi haya? Kuna nadharia tatu (3) katika kukabiliana na hali hii;

1. Afrika inaweza kuketi chini na kubaki kutizama dunia nzima ikipambana katika Mapinduzi haya. Hii ilishafanyika katika zama 3 zilizopita za Mapinduzi ya viwanda ambapo Mapinduzi ya Kwanza yaliegemea katika kutengeneza mifumo ya Kimekanika na matumizi ya Injini za mvuke katika kutengeneza bidhaa kama nguo.

Mapinduzi ya pili yakiwa ni kuhamasisha Uzalishaji mkubwa (mass production) wa bidhaa viwandani yakichagizwa na Henry Ford na awamu ya 3 ya mapinduzi ikiwa ni zama za kidijitali katika uzalishaji.

Ukitizama elimu ya msingi ya kuunda Injini ni ile ile iliyokuwepo tangu mwanzo, lakini bado Afrika haijaweza kutengeneza magari yake yenyewe.

2. Afrika inaweza kufanya kile ilichokifanya katika kuingia kwenye zama za Kidijitali, mtindo wa kuruka kama chura (leapfrog). Kwa mfano nchini Kenya watu hawakuwa na huduma za simu za mezani miaka ya 1990’s kurudi nyuma, hali kadhalika ilikuwa hivyo nchini Tanzania pamoja na nchi nyingi za kusini mwa jangwa la Sahara katika ku fahamu kuhusu Mapinduzi ya 4 ya viwanda katika biashara duniani.

Lakini baada ya mwaka 2000 watu wengi katika eneo hilo wameweza kumiliki simu za mkononi hata kama hawakuwahi kumiliki simu za mezani. Simu za mkononi zimekuja na teknolojia kubwa zaidi baada ya kuunganishwa na huduma za kifedha kama MPESA, huduma za internet, GPS na ramani, huduma za kiafya pamoja na biashara za kielektroniki ecommerce.

Mazingira ya Uchumi jumuishi (social economy) yanafanya iwe rahisi kukaribisha zama za Mapinduzi ya 4 ya viwanda. Watu wengi duniani hawapendi kusoma vitabu, hivyo sasa tunaweza kuziachia mashine kufanya kazi mbalimbali badala yetu. Kama Blockchain inatazamwa kwenda kuangamiza kabisa changamoto ya rushwa, Teknolojia ya 3D-Printing itafanya hata nyumba zetu kuwa viwanda vidogo katika kubuni bidhaa mbalimbali.

Taarifa zote zilizo kwenye mashirika ya Serikali na binafsi ikijumusha taasisi za dini zinaweza kuvunwa kwa ajili ya kupata takwimu mbadala katika chunguzi mbalimbali. Hii inatazamwa kuwa njia mbadala kuyafikia mapinduzi ya viwanda ya 4. Unahitaji kuLeapfrog biashara yako (kuepuka gharama kubwa za matangazo)? Tunalo suluhisho, wasiliana nasi mara moja tukupatie.

3. Vile vile, Afrika inaweza kukuza thamani ya uzalishaji na ubunifu wake ili kuwa mshindani halisi duniani katika kutengeneza na kusambaza bidhaa na huduma za kiteknolojia, kama inavyofanyika mahali kwingine duniani.

Japan imeweza kufanya hivyo katika sekta ya magari na India inafanya vizuri katika sekta ya Famasia na Programu za Kompyuta. Sasa kwanini Tanzania isiwe kinara katika Sayansi ya Data(Data Science) duniani. (maana mbongo mpe picha tuu, vingine utaona atakapovipata😂. Natania.) Sekta hizi za teknolojia zinataka matumizi ya akili zaidi, sio kama viwanda vya saruji na chuma ambavyo vinahitaji mtaji mkubwa wa kifedha.

Mfanyabiashara, umejiandaa vipi kuyapokea Mapinduzi haya ya 4 ya Viwanda katika eneo lako la biashara? Pitia makala hizi ili kupata taarifa zaidi:

  1. IFAHAMU NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO
  2. BANDO LAKO NI MTAJI
  3. FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA
  4. KUANZISHWA KWA ENEO HURU LA BIASHARA BARANI AFRIKA, KUNA MANUFAA GANI KWAKO?

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

mapinduzi ya 4 viwanda katika biashara duniani
Archiedee Co limited

UMUHIMU WA TEKNOLOJIA BORA KATIKA KILIMO

Kwa mujibu wa Shirika la Chakula na Kilimo duniani (FAO) mpaka mwaka 2050 watu wataongezeka mpaka kufikia bilioni 9.1 na kulisha namba hii ya watu, uzalishaji wa chakula duniani utahitajika kukuwa kwa 70% angalau. Kwa Afrika ambayo inatarajiwa kuwa na jumla ya watu bilioni 2 kufikia 2050, uzalishaji wa chakula kupitia sekta ya kilimo inabidi ukue haraka zaidi ya wastani wa dunia ili kupunguza dalili za baa la njaa. Sasa leo tuangazie umuhimu wa teknolojia bora katika kilimo. Teknolojia ina mchango gani? Makinika mpaka mwisho wa makala hii kufahamu.

Mpaka nyakati hizi bado sekta ya kilimo inakumbwa na majanga ambayo hayajapatiwa suluhu ya kudumu kama kudhoofu maendeleo maeneo ya vijijini ambapo kilimo ndipo hufanyika kwa kiasi kikubwa, kutokuwa na soko mbadala kwa mazao yatokanayo na kilimo, miundombinu mibovu, vita vya wenyewe kwa wenyewe, magonjwa kama UKIMWI, majanga ya kiasili pamoja na ukataji ovyo wa misitu.

Sasa katika zama hizi za Kidijitali, Teknolojia ina mchango gani katika kukuza sekta ya kilimo na kuboresha uchumi wa mkulima?

Simu za rununu (smartphones), mfumo wa GPS, vifaa vya RFID na barcode scanners ni baadhi ya vifaa vinavyotumika katika sekta ya kilimo katika juhudi za kuboresha uzalishaji ambapo picha za satelaiti kwa mfano, huweza kutumika kupima ukubwa wa eneo sahihi la kufanyia shughuli za kilimo kwa ubora wa hali ya juu. Vile vile vifaa maalum vinavyoweza kuhisi hali ya udongo (soil sensors) hutumika kujua ni aina gani ya mazao inafaa kulimwa kuendana na udongo wa mahala husika. Zaidi mamlaka za hali ya Hewa pia hutoa mrejesho bora kuhusu utabiri wa hali ya hewa kwa kutumia vifaa vya kisasa na teknolojia bora kwenye vipimo vyao.

Ugunduzi wa Programu za kompyuta na Applications za simu unaongeza chachu zaidi katika kufanya kilimo cha kisasa na kudhibiti taarifa muhimu katika utendaji wa hatua kwa hatua, kufanya miamala ya kifedha pamoja na kutafuta masoko. Applications maalum ziitwazo Mobile App for Agriculture and Rural Development (m-ARD) hutumika kwa usahihi katika kufanya miamala na kudhibiti maswala ya kifedha katika ufanyaji wa kilimo. Kupitia MPESA nchini Kenya, taasisi ya kilimo ya Kilimo Salama Agriculture Insurance imeongeza thamani ya bidhaa za wakulima kwa wastani wa 50% kwa bidhaa za kilimo, sawa na $150 kwa mwaka.

CHANGAMOTO KATIKA BIASHARA MPYA/INAYOANZA, FUNZO LISILOEPUKIKA.
Kwa mujibu wa Shirika la Chakula na Kilimo duniani (FAO) mpaka mwaka 2050 watu wataongezeka mpaka kufikia bilioni 9.1 na kulisha namba hii ya watu, uzalishaji wa chakula duniani utahitajika kukuwa kwa 70% angalau. Kwa Afrika ambayo inatarajiwa kuwa na jumla ya watu bilioni 2 kufikia 2050, uzalishaji wa chakula kupitia sekta ya kilimo inabidi ukue haraka zaidi ya wastani wa dunia ili kupunguza dalili za baa la njaa. Sasa leo tuangazie umuhimu wa teknolojia bora katika kilimo. Teknolojia ina mchango gani? Makinika mpaka mwisho wa makala hii kufahamu.

Je, wajua kwamba takribani theluthi moja (1/3) ya mazao yote yanayovunwa duniani kwa mwaka hupotea kwa kushambuliwa na wadudu waharibifu, magugu na magonjwa?

Sasa kwa kuligundua hili wataalam walibuni mbegu maalum katika maabara za kisayansi kwa kuboresha vinasaba (DNA) Za mazao na kufanikiwa kupata kitu walichoita Genetic Modified Organism (GMO). Kitaalam mbegu na mimea itokanayo na GMO imekuwa na faida nyingi katika kilimo zikiwemo; kuwa na uhakika wa kupata mazao mengi kwa kutumia mbegu kidogo tu. Vilevile GMO hizi zimetengenezwa zikiwa na ustahimilivu dhidi ya wadudu waharibifu na magonjwa jambo linalozipa uhakika wa kukuwa, kumea na kuzaa ipasavyo. Hata hivyo kinga hio dhidi ya wadudu waharibifu haiwazuii wadudu kama nyuki, vipepeo, minyoo wa ardhini na baadhi ya bakteria ambao huwa na jukumu muhimu katika uchavushaji wa mimea na hivyo kuleta mazao stahiki. Faida zingine ni kutunza na kuboresha rutuba ya udongo pamoja na kusaidia kuhifadhi maji ardhini, mambo ambayo yanaondoa hatari ya kutokea kwa baa la njaa duniani lakini zaidi, kuboresha uchumi wa mkulima.

Je unaamini kwamba wingi ni Faida?

Sasa majibu ya wataalam wa maswala ya kilimo duniani ni kwamba si mara zote wingi unaweza kuleta faida. Hii inajidhihirisha katika matumizi ya mbolea zinazotengenezwa maabara kiteknolojia katika kufanya kilimo ambapo kiasi kikubwa cha mbolea huweza kupelekea kudhoofisha mimea na kutishia kufifia kwa mazao kutokana na mlundikano wa kemikali zilizopo kwenye mbolea ambazo zikizidishwa ni hatari. Hivyo inashauriwa mbolea inayotumika iendane sawia na aina ya udongo, kiasi cha maji katika umwagiliaji na aina ya mazao yanayolimwa ili kuhakikisha mazao yanayotoka yanakuwa bora zaidi. Hata hivyo taarifa nyingi kuhusu matumizi ya mbolea za kisasa hupatikana kupitia applications za simu mahsusi kwa shughuli za kilimo ziitwazo m-ARD’s.

Shirika la maswala ya kilimo la M-Farmer Initiative Fund lilianzishwa mwaka 2011 kwa ushirikiano wa Mfuko wa hifadhi ya jamii wa Bill and Melinda Gates Foundation ili kuratibu, kufadhili na kukuza sekta ya kilimo barani Afrika. Shirika hili limepanga kufikia wakulima walioko katika nchi za Ethiopia, Malawi, Rwanda, Kenya, Zambia na Tanzania.

Hilo ni mojawapo la mashirika makubwa kuonyesha nia ya dhati katika kuendeleza shughuli za kilimo duniani, kuchochea umuhimu wa teknolojia bora katika kilimo na kupunguza baa la njaa, kuboresha biashara za mazao ya kilimo pamoja na kukuza uchumi wa mkulima mmoja mmoja. Mashirika hayo yanazindua mifumo ya kimtandao ya malipo, mikopo na bima za kidijitali. Kwa mfano shirika la FarmDrive la nchini Kenya limezindua huduma za kifedha mahsusi kwa ajili ya wakulima ambapo kupitia shirika hilo wakulima hata wasio na akaunti za benki na wakulima wadogo kabisa hupata mikopo huku ikisaidia taasisi za kifedha kuongeza huduma za mikopo ya kilimo kwa gharama nafuu.

Kwa wafanyabiashara na kampuni zilipo ukanda wa Afrika Mashariki hii ni fursa kwao kuelekeza macho yao katika sekta ya kilimo kama inavyofanya FarmDrive nchini Kenya na shirika la kimataifa la M-Farmer.

Unalionaje hili? (tafadhali share kwenye comments) Hivyo kupitia jitihada za mashirika hayo, wakulima sasa wanaweza kupata mbolea, mbegu bora na mifumo mizuri ya umwagiliaji ili kukuza shughuli zao. Mchakato huo huboresha kasi ya uzalishaji katika kilimo na kupunguza changamoto kwa kutumia takwimu sahihi katika utendaji wa shughuli za kilimo kwa kutumia data za kisayansi na hivyo, umuhimu wa teknolojia bora katika kilimo unazidi kuonekana. Kwa mfano matumizi ya vifaa vya umwagiliaji vinavyotumia nishati ya jua kusukuma maji kutoka katika chanzo chake kama mto, ziwa, bwawa au bahari. Vifaa hivi vimerahisisha sana swala zima la umwagiliaji.

Vilevile kwa kuzingatia ukweli kwamba mashamba mengi yapo maeneo ambayo ni mbali na huduma za mitandao ya simu na intaneti, hivyo kufanya huduma hizo kuwa hafifu, nchi kama Ethiopia imerusha satelaiti yake na kufanya wakulima kuwa katika nafasi nzuri kunufaika na mradi huo. Serikali za nchi zingine za Afrika Mashariki zinakwama wapi kwenye hili?

umuhimu wa teknolojia bora katika kilimo.

matumizi ya TEHAMA katika Satellite

Hata hivyo zama hizi kutokana na kuimarika kwa miundombinu ya uchukuzi na usafirishaji, pamoja na maendeleo katika sekta ya sayansi na teknolojia ya Habari na mawasiliano, imekuwa rahisi sana kupata taarifa kuhusu Hali ya Hewa, Hali ya soko na ushindani, mazingira ya miundombinu ya uchukuzi, mfumuko wa bei na uelekeo wa mahitaji ya wateja. Kilimo kimeja kufanyika katika namna rahisi sana katika kuuza mazao baada ya kuvuna, shukrani umuhimu wa teknolojia bora katika kilimo cha kisasa na chenye tija.

Kufahamu zaidi namna unavyoweza kuimarisha shughuli zako za kilimo kwa kutumia teknolojia tafadhali pitia makala zilizomo kwenye links hizi hapa:

  1. IFAHAMU NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO
  2. FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWUWEKEZA
  3. UNAWEZA VIPI KUKABILIANA NA HASARA KATIKA BIASHARA YAKO MWAKA HUU 2021

TEKNOLOJIA KATIKA KUKUZA BIASHARA KUPITIA SEKTA YA UTALII

Inasemekana binadamu anajua zaidi mazingira ya mwezini kuliko ajuavyo mazingira ya ndani/chini ya bahari. Sasa kampuni ya usafirishaji ya Uber tarehe 23 May 2019 ilizindua manuwari ndogo iitwayo ScUber kwa ajili ya kutalii ambapo mradi huo umeanzia jijini Queensland, Australia. Moja kati ya sababu ikiwa ni kutoa fursa kwa wageni/watalii kuweza kuzuru eneo maarufu la bahari liitwalo The Great Barrier Reef nchini humo. Sasa tunaweza vipi kutumia teknolojia katika kukuza biashara kupitia sekta ya utalii? Kumbuka Tanzania ina vivutio vingi sana vya utalii na vijana wengi wamejikita katika kuhudumia watalii hao, watumieje teknolojia kujiletea manufaa? Twende sambamba mpaka mwisho wa makala hii kufahamu zaidi.

utalii na teknolojia

Turudi Australia, manuwari hio ndogo yenye uwezo wa kubeba watu watatu kwa wakati mmoja ni ya kwanza kabisa duniani kufanya shughuli za kutalii kwa mtu yeyote anayehitaji kufanya hivyo na ambayo huduma yake inapatikana kirahisi kupitia Application ya Uber inayopatikana Playstore ya Google na Appstore ya iOS (Je, wewe ni mmoja kati ya wale waliozoea kuziona manuwari kwenye muvi na kusikia manuwari za kivita tu? 😂). Haya ni mapinduzi makubwa katika kufanya biashara kupitia nyanja nyingine ya kichumi (kutoka usafirishaji mpaka utalii).

Sekta ya utalii inatajwa kuwa ni sekta muhimu sana katika ukuaji wa uchumi na kutengeneza ajira duniani kote. Sekta hio inatajwa kujumuisha 8.8% ya ajira zote duniani, sawa na watu milioni 258. Vile vile 9.1% ya wastani wa pato la taifa GDP inatokea katika sekta hii ambayo ni sawa na $6 trilioni. Zaidi, 5.8% ya bidhaa zinazosafirishwa nje ya nchi (exports) huhusishwa na sekta hii ambayo ni takribani $1.1 trilioni. Hata hivyo, sekta hii ya utalii huchochea sana uwekezaji ambapo 4.5% ya uwekezaji wote unaofanywa duniani hupitia katika sekta hii ambayo ni sawa na $652 bilioni za kimarekani.

Tukiangazia eneo la kusini mwa jangwa la Sahara inakadiriwa kwamba ajira 3.8 milioni zikijumuisha ajira 2.4 ambazo si za moja kwa moja (indirect jobs) zinakadiriwa kutengenezwa katika miaka 10 ijayo. Hii ni kwa mujibu wa Baraza la usafiri na utalii duniani (WTTC).

Sasa changamoto; Sekta hii ya utalii inachangia vipi katik kukuza biashara barani Afrika? Teknolojia inachangia vipi katika maendeleo haya ya utalii na biashara?

Kutoka ziara za watalii 6.7 milioni mwaka 1990, nchi za ukanda wa kusini mwa jangwa la Sahara zilitembelewa na watalii 33.8 milioni kufikia mwaka 2012 kwa pamoja ambapo stakabadhi za wageni mwaka huo 2012 peke yake zilionyesha zaidi ya dola za kimarekani 36 bilioni zilipatikana huku mchango wa moja kwa moja ukiwa ni 2.8% katika pato la ndani la taifa GDP (Jumla ya mchango ikiwa ni mchango wa moja kwa moja na ule usio wa moja kwa moja, ilifikia 7.3% ya GDP). Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya baraza la WTTC mwaka 2013.

Lakini, ili kufanikiwa zaidi katika kufanya Utalii na kuendeleza biashara, ukanda huo wa SSA (Subsaharan Area) inabidi ujidhatiti katika mambo yafuatayo; upatikanaji wa ardhi, ruhusa ya wawekezaji katika maswala ya fedha, matangazo ya utalii, kodi za uwekezaji katika utalii, utaalamu na ujuzi katika utalii, ulinzi na usalama, maswala ya afya, mahitaji ya viza na ukiritimba. Sasa teknolojia inaleta mchango gani katika kukuza biashara kwa kupitia utalii? Kuhusu namna unavyoweza kuitangaza biashara yako katika nyanja hii ya utalii fuatana na makala hii hapa

Tuzione baadhi ya njia za kiteknolojia zinazotumika katika nyanja hio;

E-TOURISM:

Huduma za intaneti zimeleta mapinduzi makubwa sana kwenye sekta hii ya utalii ambapo watalii na wageni sasa wanaweza kupata taarifa muhimu kuhusu mahali wanapotaka kwenda kutalii kama mbuga za wanyama, bidhaa za kiasili na utamaduni, hoteli, majumba ya makumbusho na historia mbalimbali kwa kutumia vifa vyao vya kielekroniki vilivyoungwa na huduma za intaneti kama simu za rununu na kompyuta mpakato (laptop). Matokeo yake wageni na watalii wamekuwa na mahitaji makubwa kwa bidhaa za kiasili na utamaduni pamoja na kujali thamani ya pesa zao pamoja na thamani ya muda wao. Hii imerahisisha sana ufanyaji wa biashara haswa kupitia majukwaa ya ecommerce (ambayo unaweza kuyapata kwetu Rednet Technologies kirahisi sana., gusa link hii kupata huduma zetu zenye ubora Our Services🙋).

E-HOSPITALITY;

Teknolojia ya ICT imepenya mpaka katika mifumo ya huduma kwa wageni kwa haraka mno, huku ikizama katika utendaji wa hoteli, kuunda upya shughuli za masoko, kukuza huduma kwa wateja, kuimarisha huduma za kifedha, huduma za usafiri wa anga pamoja na huduma za kuwezesha ufanyaji wa biashara mtandaoni. Hii imeleta mafanikio zaidi baada ya kugunduliwa mifumo ya Computerized Reservetion Systems (CRS‘s) kuchukua nafasi ya mfumo wa zamani wa kuandikisha wageni katika mahoteli na katika vituo vya afya.

E-TRAVEL AGENCIES:

Teknolojia ya ICT imeleta maendeleo makubwa katika uendeshaji wa shughuli za taasisi mbalimbali na wakala wa kusafirisha na kutembeza wageni na watalii ambapo imeimarisha sana shughuli za ndani kama uhasibuukaguzi na rasilimali watu pamoja na shughuli za nje kama huduma kwa wateja, mifumo ya tiketi na mawasiliano ya wabia. Licha ya kuwa na 15% ya idadi yota ya watu duniani, Afrika ilikuwa ikihudumia 4% tu ya abiria wa safari za ndege duniani. Hata hivyo huduma hio ilipanda kufikia 6.5% katika kipindi cha mwaka 1998-2009 huku Carpe Verde, Msumbiji, Ethiopia na Tanzania(kabla ya kuimarishwa kwa AirTanzania) zikikuwa kwa makumi ya asilimia (WorldBank report). Maendeleo haya yanaakisi ukuaji wa matumizi ya teknolojia katika eneo hilo ambapo kumekuwepo pia na matumizi ya mifumo ya kudhibiti tiketi (OTS) na mifumo ya kuwasiliana na wateja (CRM‘s). Zaidi mifumo ya kudhibiti tiketi imekuwa muhimu katika kuratibu idadi ya wageni pamoja na kudhibiti maswala ya fedha kiteknolojia.

E-DESTINATION:

Hii ni maalum kwa waendeshaji wa Hoteli, Nyumba za wageni (Guest Houses & Lodges) pamoja na migahawa ya chakula. Sasa teknolojia imeleta mifumo mahsusi kwa ajili ya kurahisisha huduma katika kutafuta soko na kusajili wageni/watalii kirahisi wakiwa popote duniani kwa kutumia simu za rununu au kompyuta. Mfumo wa Destination Management System (DMS) umekuwa muhimu sana licha ya 10% tu ya vyumba vya hoteli 390,000 zinazopatikana katika ukanda wa kusini mwa jangwa la Sahara kuwa na hadhi ya kimataifa, huku Afrika Kusini ikishikilia nusu ya vyumba hivyo. Hata hivyo Kenya, Mauritius, Shelisheli na Tanzania zinaonyesha kuwekeza zaidi katika huduma za hoteli na teknolojia.

E-COMMERCE:

Jukwaa maarufu zaidi duniani katika kufanya biashara kwa njia ya mtandao kielektroniki. Hii ni muhimu kwa wafanyabiashara wa bidhaa za kiasili na kitamaduni kama shangavinyago na batiki ambapo sasa wanaweza kuweka bidhaa zao katika majukwaa hayo na kufikisha bidhaa zao duniani kote kirahisi zaidi, hivyo kukuza mauzo yao (Majukwaa haya ya ecommerce yanapatikana hapa Rednet Technologies, pitia tovuti yetu kwa kugusa link hii Rednet Technologies).

Kufahamu zaidi kuhusu e-commerce tafadhali fuatilia makala hii hapa kwenye link https://rednet.co.tz/unafahamu-nini-kuhusu-biashara-za-kielektroniki-e-commerce-businesses/ yenye kichwa “UNAFAHAMU NINI KUHUSU BIASHARA ZA KIELEKTRONIKI?”

Una la zaidi? Tafadhali, weka comment yako hapo chini ili tuweze share mawazo na hoja kuhusu makala haya juu ya unaweza vipi kutumia teknolojia katika kukuza biashara kupitia sekta ya utalii? Kazi kwako mfanyabiashara.

Je umependezwa na makala zetu zilizomo katika website yetu hapa?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) na QR CODE ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA kwenye picha hapa muda wote 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?